< Yeremia 28 >

1 Ilitokea katika mwaka ule, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne na mwezi wa tano, Hanania mwana wa Azuri nabii, alikuwa wa Gibeoni, alisema kwangu katika nyumba ya Yahwe mbele za makuhani na watu wote. Alisema,
And it came about in that year, when Zedekiah first became king of Judah, in the fourth year, in the fifth month, that Hananiah, the son of Azzur the prophet, who came from Gibeon, said to Jeremiah in the house of the Lord, before the priests and all the people,
2 “Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeivunja nira iliyowekwa na mfalme wa Babeli.
These are the words of the Lord of armies, the God of Israel: By me the yoke of the king of Babylon has been broken.
3 Ndani ya miaka miwili nitavirudisha katika sehemu hii vyombo vyote vya nyumba ya Yahwe ambavyo Nebukadreza mfalme wa Babeli livichukua kutoka sehemu hii na kuvisafirisha hadi Babeli.
In the space of two years I will send back into this place all the vessels of the Lord's house which Nebuchadnezzar, king of Babylon, took away from this place to Babylon:
4 Kisha nitawarudisha katika sehemu hii Yekonia mwana wa Yehotakimu, mfalme wa Yuda, na mateka wote wa Yuda ambao walipelekwa Babeli—hili ni tangazo la Yahwe—kwa maana nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.”
And I will let Jeconiah, the son of Jehoiakim, king of Judah, come back to this place, with all the prisoners of Judah who went to Babylon, says the Lord: for I will have the yoke of the king of Babylon broken.
5 Kwa hiyo Yeremia nabii akasema kwa Hanania nabii mbele ya makuhani na kwa watu wote waliosimama katika nyumba ya Yahwe.
Then the prophet Jeremiah said to the prophet Hananiah, before the priests and all the people who had come into the house of the Lord,
6 Yeremia nabii akasema, “Yahwe afanye hivi! Yahwe ayathibitishe maneno ambayao ulitabiri na kuvirudisha katika sehemsu hii vyombo vya nyumb a ya Yahwe, na mateka wote kutoka Babeli.
The prophet Jeremiah said, So be it: may the Lord do so: may the Lord give effect to the words which you have said, and let the vessels of the Lord's house, and all the people who have been taken away, come back from Babylon to this place.
7 Vile vile, sikilizeni neno ambaloo ninalitangaza katika masikio yenu na katika masikio ya watu wote.
But still, give ear to this word which I am saying to you and to all the people:
8 Manabii ambao walikuwepo mbele yangu na na mbele yenu muda mrefu uliopita pia walitabiri kuhusu mataifa mengi na juu ya falme kuu, kuhusu vita, njaa, na mapigo.
The prophets, who were before me and before you, from early times gave word to a number of countries and great kingdoms about war and destruction and disease.
9 Kwa hiyo nabii anayetabiri kwamba kutakuwa na amani—kama neno lake litatimia, basi itajulikana kwamba yeye ni nabii kweli aliyetumwa na Yahwe.”
The prophet whose words are of peace, when his words come true, will be seen to be a prophet whom the Lord has sent.
10 Lakini Hanania nabii akaichukua nira kutoka kwenye shingo ya Yeremia na kuivunja.
Then Hananiah the prophet took the yoke from the neck of the prophet Jeremiah and it was broken by his hands.
11 Kisha Hanania akanena mbele ya watu wote na kusema, “Yahwe anasema hivi: Kama hivi tu, ndani ya miaka miwili nitaivunja nira iliyowekwa na Nebukadreza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo ya kila taifa.” Kisha Yeremia nabii akaenda njia yake.
And before all the people Hananiah said, The Lord has said, Even so will I let the yoke of the king of Babylon be broken off the necks of all the nations in the space of two years. Then the prophet Jeremiah went away.
12 Baada ya Hanania nabii kuivunja nira kutoka kwenye shingo ya Yeremia nabii, neno la Yahwe likamjia Yeremia. likisema,
Then after the yoke had been broken off the neck of the prophet Jeremiah by Hananiah the prophet, the word of the Lord came to Jeremiah, saying,
13 Nenda na ukaseme kwa Hanania na useme, Yahwe anasema hivi: Uliivunja nira ya mbao, lakini badala yake nitafanya nira ya chuma.'
Go and say to Hananiah, This is what the Lord has said: Yokes of wood have been broken by you, but in their place I will make yokes of iron.
14 Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeweka nira ya chuma shingoni mwa mataifa haya yote ili wamtumikea Nebukadreza mfalme wa Babeli, na watamtumikia. Pia nimempa wanyama wa mashambani awatawale.”
For the Lord of armies, the God of Israel, has said: I have put a yoke of iron on the necks of all these nations, making them servants to Nebuchadnezzar, king of Babylon; and they are to be his servants: and in addition I have given him the beasts of the field.
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia Hanania nabii, “Sikiliza Hanania! Yahwe hajakutuma, bali wewe mwenyewe umewasababisha watu hawa kuamini katika uongo.
Then the prophet Jeremiah said to Hananiah the prophet, Give ear, now, Hananiah; the Lord has not sent you; but you are making this people put their faith in what is false.
16 Kwa hiyo Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kukutuma nje ya dunia. Mwaka huu utakufa.”
For this reason the Lord has said, See, I will send you away from off the face of the earth: this year death will overtake you, because you have said words against the Lord.
17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, Hanania nabii akafa.
So death came to Hananiah the prophet the same year, in the seventh month.

< Yeremia 28 >