< Yeremia 26 >
1 Mwanzoni mwa utawala wake Yehoyakimu mwana wa Yosia, neno likaja kutoka kwa Yeremia, likisema,
Au commencement du règne de Jéhojakim, fils de Josias, roi de Juda, cette parole fut adressée à Jérémie de la part de l'Éternel, en ces termes:
2 “Yahwe anasema hivi: Simama katika uwanja wa nyumba yangu na sema kuhusu miji yote ya Yuda ambao huja kuabudu katika nyumba yangu. Tangaza maneno yote niliyokuamuru kuyasema kwao. Usipunguze neno lolote!
Ainsi a dit l'Éternel: Tiens-toi debout dans le parvis de la maison de l'Éternel, et dis à toutes les villes de Juda, qui viennent pour se prosterner dans la maison de l'Éternel, toutes les paroles que je t'ai commandé de leur dire; n'en retranche pas un mot.
3 Labda watasikiliza, kwamba kila mtu ataziacha njia zake mbaya, ili nighairi majanga ninayokusudia kuyaleta juu yao kwa sababu ya uovu wa matendo yao.
Peut-être qu'ils écouteront, et reviendront chacun de sa mauvaise voie, et je me repentirai du mal que je pense à leur faire, à cause de la malice de leurs actions.
4 Kwa hiyo lazima useme kwao, 'Yahwe anasema hivi: Kama hamtanisikiliza ili mtembee katika sheria yangu ambayo nimeiweka mbele yenu—
Tu leur diras donc: Ainsi a dit l'Éternel: Si vous ne m'écoutez pas, pour marcher dans ma loi, que j'ai mise devant vous;
5 kama hamsikilizi maneno ya watumishi wangu manabii ambao naendelea kuwatuma kwenu—lakini hamjasikiliza! —
Pour obéir aux paroles des prophètes, mes serviteurs, que je vous envoie, que je vous ai envoyés dès le matin, et que vous n'avez pas écoutés;
6 kisha nitaifanya nyumba hii kuwa kama Shilo; nitaifanya nyumba hii kuwa laana katika macho ya mataifa yote juu ya dunia.
Je traiterai cette maison comme Silo, et je livrerai cette ville à l'exécration de toutes les nations de la terre.
7 Makuhani, manabii, na watu wote wakamsikia Yeremia akitangaza maneno haya katika nyumba ya Yahwe.
Or, les sacrificateurs, et les prophètes, et tout le peuple, entendirent Jérémie qui prononçait ces paroles dans la maison de l'Éternel.
8 Kwa hiyo ikatokea kwamba Yeremia alipomaliza kutangaza aliyokuwa Yahwe alimwwamuru kuyasema kwa watu wote, makuhani, manabii, na watu wote wakamsimamisha na kusema, “Hakika utakufa!
Et il arriva, aussitôt que Jérémie eut achevé de prononcer tout ce que l'Éternel lui avait ordonné de dire à tout le peuple, que les sacrificateurs, et les prophètes, et tout le peuple, le saisirent, en disant: Tu vas mourir!
9 Kwa nini umetabiri katika jina la Yahwe na kusema kwamba nyumba hii itakuwa kama Shilo na mji huu utakuwa ukiwa, pasipo wakaaji?” Kwa maana watu wote wameunda kundi dhidi ya nyumba ya Yeremia.
Pourquoi prophétises-tu au nom de l'Éternel, en disant: Cette maison sera comme Silo, et cette ville sera désolée, privée d'habitants? Et tout le peuple s'attroupa contre Jérémie dans la maison de l'Éternel.
10 Kisha wakuu wa Yuda wakasikia maneno haya na wakapanda kutoka nyumba ya mfalme kwenda kwenye nyumba ya Yahwe. Wakakaa katika njia ya lango katika Lango Jipya la nyumba ya Yahwe.
Mais les chefs de Juda, ayant entendu ces choses, montèrent de la maison du roi à la maison de l'Éternel, et s'assirent à l'entrée de la porte neuve de la maison de l'Éternel.
11 Makuhani na manabii wakasema kwa wakuu wa Yuda na kwa watu wote. Wakasema, “Ni haki kwa mtu huyu kufa, kwa maana ametabiri juu ya mji huu, kama mlivyosikia kwa masikio yenu!”
Alors les sacrificateurs et les prophètes parlèrent aux chefs et à tout le peuple, et dirent: Cet homme mérite la mort; car il a prophétisé contre cette ville, comme vous l'avez entendu de vos oreilles.
12 Kwa hiyo Yeremia akasema kwa wakuu wote na watu wote, “Yeremia amenituma kutabiri juu ya nyumb hii na mji wake, kusema maneno yote ambayo mmeyasikia.
Mais Jérémie parla à tous les chefs et à tout le peuple, en disant: C'est l'Éternel qui m'a envoyé pour prophétiser, contre cette maison et contre cette ville, toutes les paroles que vous avez entendues.
13 Kwa hiyo sasa, imarisheni njia zenu na matendo yenu, na sikilizeni sauti ya Yahwe Mungu wenu kwamba ataghairi kuhusu janga ambalo ametangaza dhidi yenu.
Et maintenant, amendez vos voies et vos actions, et écoutez la voix de l'Éternel votre Dieu, et l'Éternel se repentira du mal qu'il a prononcé contre vous.
14 Mimi mwenyewe—niangalieni! —niko mikononi mwenu. Nitendeeni yaliyo mema na sahihi katika macho yenu.
Pour moi, me voici entre vos mains; faites de moi comme il vous semblera bon et juste.
15 Lakini kwa hakika lazima mjue kwamba kama mtaniua mimi, basi mnaiweka damu isiyo na hatia juu yenu wenyewe na juu ya mji huu na wakaaji wake, kwa maana Yahwe amenituma kweli kwenu ili nitangaze maneno yote kwa ajili ya masikio yenu.”
Seulement sachez bien que si vous me faites mourir, vous mettrez du sang innocent sur vous, sur cette ville, et sur ses habitants. Car, en vérité, l'Éternel m'a envoyé vers vous, pour prononcer à vos oreilles toutes ces paroles.
16 Kisha wakuu na watu wote wakasema kwa makuhani na manabii, “Si vyema kwa mtu huyu kufa, kwa maana ametangaza mambo haya kwetu katika jina la Yahwe Mungu wetu.”
Alors les chefs et tout le peuple dirent aux sacrificateurs et aux prophètes: Cet homme n'a pas mérité la mort; car c'est au nom de l'Éternel notre Dieu qu'il nous a parlé.
17 Kisha watu kutoka wazee wa nchi wakasimama na kusema kwa kusanyiko lote la watu.
Et quelques-uns des anciens du pays se levèrent, et parlèrent à toute l'assemblée du peuple, en disant:
18 Wakasema, “Mikaya Mmorashi alikuwa akitabiri katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda. Alinena kwa watu wote wa Yuda na kusema, 'Yahwe wa majeshi anasema hivi: Sayuni utalimwa kama shamba, Yerusalemu utakuwa lundo la magofu, na mlima wa hekalu utakuwa kilima kilichoota vichaka.' Hezekia mfalme wa Yuda na Yunda wote walimuua?
Michée de Morésheth prophétisait aux jours d'Ézéchias, roi de Juda, et il parla à tout le peuple de Juda, en disant: “Ainsi a dit l'Éternel des armées: Sion sera labourée comme un champ; et Jérusalem sera changée en un monceau de ruines, et la montagne du temple en une haute forêt. “
19 Hakumwogopa Yahwe na kuutaka radhi uso wa Yahwe ili kwamba Yahwe angeghairi kuhusu janga ambalo alilitangaza kwao? Kwa hiyo tutafanya maovu makubwa zaidi juu ya maisha yetu sisi wenyewe?”
Ézéchias, roi de Juda, et tout Juda, le firent-ils mourir? Ézéchias ne craignit-il pas l'Éternel; et ne supplia-t-il pas l'Éternel? Et l'Éternel se repentit du mal qu'il avait prononcé contre eux. Et nous, chargerions-nous nos âmes d'un si grand crime?
20 Wakati huo huo palikuwa na mtu mwingine ambaye alitabiri katika jina la Yahwe—Uria mwan wa Shemaya kutoka Kiriath Yearimu—pia alitabiri juu ya mji na nchi hii, akikubaliana na maneno yote ya Yeremia.
Il y eut aussi un homme qui prophétisait au nom de l'Éternel: Urie, fils de Shémaja, de Kirjath-Jéarim. Il prophétisa contre cette ville et contre ce pays, les mêmes choses que Jérémie.
21 Lakini Mfalme Yohoyakimu na wanajeshi wake wote na watumishi wake wote waliposikia maneno yake, kisha mfalme alijaribu kumuua, lakini Uria alisikia na kuogopa, kwa hiyo alikimbia na akaenda Misiri
Et le roi Jéhojakim, avec tous ses guerriers et tous les chefs, entendit ses paroles; et le roi voulut le faire mourir; mais Urie, l'ayant appris et ayant eu peur, s'enfuit et s'en alla en Égypte.
22 Kisha mfalme Yehoyakimu alituma watu kwenda Misiri—Elnathani mwana wa Achbori na watu kwenda Misiri kumfuata Uria.
Mais le roi Jéhojakim envoya des gens en Égypte: Elnathan, fils d'Acbor, et quelques autres avec lui, en Égypte;
23 Wakamtoa Uria nje kutoka Misiri na kumleta kwa Mfalme Yehoyakimu. Kisha Yehoyakimu akamuua kwa upanga na kumpeleka nje kwenye makaburi ya watu wa kawaida.
Et ils firent sortir d'Égypte Urie, et l'amenèrent au roi Jéhojakim, qui le fit mourir par l'épée et jeta son cadavre dans les tombeaux des enfants du peuple.
24 Lakini mkno wa Ahikamu mwana wa Shapni alikuwa pamoja na Yeremia, hivyo hakutiwa mikonono mwa watu ili auawe.
Cependant la main d'Achikam, fils de Shaphan, fut avec Jérémie, et empêcha qu'on ne le livrât aux mains du peuple pour le faire mourir.