< Yeremia 25 >

1 Hili ndilo neno ambalo lilimjia Yeremia juu ya watu wote wa Yuda. Ikawa mwaka wa nne wa Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda. Huo ndio mwaka wa kwanza wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli.
The word that came to Jeremiah concerning all the people of Judah in the fourth year of Jehoiakim the son of Josiah, king of Judah, that was the first year of Nebuchadrezzar king of Babylon;
2 Yeremia nabii aliwahubiria watu wote wa Yuda na wenyeji wote wa Yerusalemu.
which Jeremiah the prophet spoke unto all the people of Judah, and to all the inhabitants of Jerusalem, saying:
3 Akasema, “Kwa miaka ishirini na mitatu, tangu mwaka wa kumi na tatu wa Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda mpaka leo, maneno ya Bwana yamekuja kwangu. Nimewahubiria ninyi. Nilikuwa na nia ya kutangaza, lakini hamkunisikiliza.
From the thirteenth year of Josiah the son of Amon, king of Judah, even unto this day, these three and twenty years, the word of the LORD hath come unto me, and I have spoken unto you, speaking betimes and often; but ye have not hearkened.
4 Bwana akawapeleka watumishi wake wote manabii kwako. Walikuwa na nia ya kwenda, lakini hukusikiliza wala kutega masikio.
And the LORD hath sent unto you all His servants the prophets, sending them betimes and often — but ye have not hearkened, nor inclined your ear to hear —
5 Manabaii hawa walisema, 'Kila mtu auache uovu wake na udhalimu wa matendo yake na kurudi kwenye nchi ambayo Yahwe aliitoa wakati wa zamanai kwa ajili ya babu zenu na ninyi, kama zawadi ya kudumu.
saying: 'Return ye now every one from his evil way, and from the evil of your doings, and dwell in the land that the LORD hath given unto you and to your fathers, for ever and ever;
6 Kwa hiyo msiifuate miungu mingine ili kuiabudu au kuiinamia chini, na msimkasirishe kwa kazi ya mikono yenu ili kwamba awaumize.
and go not after other gods to serve them, and to worship them, and provoke Me not with the work of your hands, and I will do you no hurt.'
7 Lakini hamkunisikiliza-hili ndilo tamko la Bwana-kwa hiyo umenikasirisha kwa kazi ya mikono yako ili kujidhuru nafsi zemu.
Yet ye have not hearkened unto Me, saith the LORD; that ye might provoke Me with the work of your hands to your own hurt.
8 Basi, Bwana wa majeshi asema hivi, 'Kwa kuwa hukusikiliza maneno yangu,
Therefore thus saith the LORD of hosts: Because ye have not heard My words,
9 tazama, nitaagiza amri ya kukusanya watu wote wa kaskazini- asema Bwana- na Nebukadreza, mtumishi wangu, mfalme wa Babeli, na kuwaleta juu ya nchi hii na wenyeji wake, na juu ya mataifa yote yaliyo karibu nawe. Kwa maana nitawaangamiza. Nitawageuza kuwa na hofu, kuwa kitu cha kuzomewa na ukiwa wa daima.
behold, I will send and take all the families of the north, saith the LORD, and I will send unto Nebuchadrezzar the king of Babylon, My servant, and will bring them against this land, and against the inhabitants thereof, and against all these nations round about; and I will utterly destroy them, and make them an astonishment, and a hissing, and perpetual desolations.
10 Sauti ya furaha na sherehe-sauti ya bwana arusi na bibi arusi, sauti ya mawe ya kusagia na mwanga wa taa-nitafanya mambo yote haya kutoweka kutoka kwa mataifa haya.
Moreover I will cause to cease from among them the voice of mirth and the voice of gladness, the voice of the bridegroom and the voice of the bride, the sound of the millstones, and the light of the lamp.
11 Ndipo nchi hii yote itakuwa ukiwa na hofu, na mataifa haya watamtumikia mfalme wa Babeli kwa miaka sabini.
And this whole land shall be a desolation, and a waste; and these nations shall serve the king of Babylon seventy years.
12 Kisha miaka sabini itakapokamilika, nitamuadhibu mfalme wa Babeli na taifa hilo, nchi ya Wakaldayo-hili ndilo tamko la Bwana-kwa uovu wao na kuifanya kuwa ukiwa milele.
And it shall come to pass, when seventy years are accomplished, that I will punish the king of Babylon, and that nation, saith the LORD, for their iniquity, and the land of the Chaldeans; and I will make it perpetual desolations.
13 Nami nitaleta juu ya nchi hiyo maneno yote niliyosema, na kila kitu kilichoandikwa katika kitabu hiki ambacho Yeremia ametabiri juu ya mataifa yote.
And I will bring upon that land all My words which I have pronounced against it, even all that is written in this book, which Jeremiah hath prophesied against all the nations.
14 Kwa maana pia mataifa mengi na wafalme wakuu watapata watumwa kutoka mataifa haya. Nitawalipa kwa matendo yao na kazi za mikono yao.'”
For many nations and great kings shall make bondmen of them also; and I will recompense them according to their deeds, and according to the work of their own hands.
15 Kwa kuwa Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, “Chukua kikombe hiki cha divai ya ghadhabu kutoka mkononi mwangu, ukawanyweshe mataifa yote niliyokutuma.
For thus saith the LORD, the God of Israel, unto me: Take this cup of the wine of fury at My hand, and cause all the nations, to whom I send thee, to drink it.
16 Kwa maana watakunywa na kisha watalewa na kufanya wazimu mbele ya upanga ambao nitaupeleka kati yao.”
And they shall drink, and reel to and fro, and be like madmen, because of the sword that I will send among them. —
17 Basi, nikakichukua kikombe mkononi mwa Bwana, nikawanywesha mataifa yote ambayo Bwana alinituma:
Then took I the cup of the LORD'S hand, and made all the nations to drink, unto whom the LORD had sent me:
18 Yerusalemu, miji ya Yuda, na wafalme wake, na wakuu wake, na kuwafanya kuwa ukiwa na kitu cha kutisha, na kuwa kitu cha kuzomewa na laana, kama ilivyo hata leo.
Jerusalem, and the cities of Judah, and the kings thereof, and the princes thereof, to make them an appalment, an astonishment, a hissing, and a curse; as it is this day;
19 Mataifa mengine pia walipaswa kunywa: Farao mfalme wa Misri na watumishi wake; maafisa wake na watu wake wote;
Pharaoh king of Egypt, and his servants, and his princes, and all his people;
20 watu wote wa urithi wa mchanganyiko na wafalme wote wa nchi ya Uzi; na wafalme wote wa nchi ya Wafilisti, na Ashkeloni, na Gaza, na Ekroni, na mabaki ya Ashdodi;
and all the mingled people; and all the kings of the land of Uz, and all the kings of the land of the Philistines, and Ashkelon, and Gaza, and Ekron, and the remnant of Ashdod;
21 Edomu na Moabu na wana wa Amoni.
Edom, and Moab, and the children of Ammon;
22 Wafalme wa Tiro na Sidoni, wafalme wa pwani ng'ambo ya pili ya bahari,
and all the kings of Tyre, and all the kings of Zidon, and the kings of the isle which is beyond the sea;
23 Dedani, Tema, na Busi pamoja na wale wanyoao nywele zao upande wa pili wa vichwa vyao, pia walipaswa kukinywa.
Dedan, and Tema, and Buz, and all that have the corners of their hair polled;
24 Watu hawa pia walitakiwa kukinywa; wafalme wote wa Uarabuni na wafalme wote wa watu wa asili mchanganyiko wanaoishi nyikani;
and all the kings of Arabia, and all the kings of the mingled people that dwell in the wilderness;
25 wafalme wote wa Zimri, wafalme wote wa Elamu, na wafalme wote wa Wamedi;
and all the kings of Zimri, and all the kings of Elam, and all the kings of the Medes;
26 wafalme wote wa kaskazini, wale wa karibu na wale wa mbali—kila mmoja na ndugu zake na falme zote za ulimwengu ambazo ziko chini ya uso wa dunia. Hatimaye mfalme wa Babeli atakunywa baada yao wote.
and all the kings of the north, far and near, one with another; and all the kingdoms of the world, which are upon the face of the earth. — And the king of Sheshach shall drink after them.
27 Bwana akaniambia, “Basi, uwaambie, 'Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi kunywa na kulewa, kisha tapika, uanguke, wala usisimame mbele ya upanga nitakaoutuma kati yenu.'
And thou shalt say unto them: Thus saith the LORD of hosts, the God of Israel: Drink ye, and be drunken, and spew, and fall, and rise no more, because of the sword which I will send among you.
28 Kisha itatokea kwamba ikiwa wanakataa kuchukua kikombe mkononi mwako ili kunywa, utawaambia, 'Bwana wa majeshi asema hii lazima mnywe.
And it shall be, if they refuse to take the cup at thy hand to drink, then shalt thou say unto them: Thus saith the LORD of hosts: Ye shall surely drink.
29 Kwa maana, tazama, nitaleta janga juu ya mji ulioitwa kwa jina langu, je ninyi mtaachiliwa msiadhibiwe? Hutakuwa huru, kwa maana nitaita upanga juu ya wenyeji wote wa nchi! - ndilo tamko la Bwana wa majeshi.'
For, lo, I begin to bring evil on the city whereupon My name is called, and should ye be utterly unpunished? Ye shall not be unpunished; for I will call for a sword upon all the inhabitants of the earth, saith the LORD of hosts.
30 Basi wewe mwenyewe, Yeremia, tabiri kwao maneno haya yote. Uwaambie, 'Bwana atanguruma kutoka juu, naye atapaza sauti yake toka makao yake matakatifu, na radi kutoka mahali pake patakatifu; naye atapiga kelele kama wale wakanyagao zabibu dhidi ya wote wanaoishi duniani.
Therefore prophesy thou against them all these words, and say unto them: The LORD doth roar from on high, and utter His voice from His holy habitation; He doth mightily roar because of His fold; He giveth a shout, as they that tread the grapes, against all the inhabitants of the earth.
31 Kelele huja mpaka mwisho wa nchi, kwa sababu mgogoro kutoka kwa Bwana utaleta mashtaka dhidi ya mataifa. Ataleta haki kwa wote wenye mwili. Yeye atawatia waovu katika upanga-hili ndi'o tamko la Bwana.'
A noise is come even to the end of the earth; for the LORD hath a controversy with the nations, He doth plead with all flesh; as for the wicked, He hath given them to the sword, saith the LORD.
32 Bwana wa majeshi asema hivi, 'Tazameni, taabu itatokea toka kwa taifa hadi taifa, na dhoruba kubwa itatokea toka pande za mwisho za dunia.
Thus saith the LORD of hosts: Behold, evil shall go forth from nation to nation, and a great storm shall be raised up from the uttermost parts of the earth.
33 Kisha wale waliouawa na Bwana watakuja kutoka upande mmoja wa dunia hadi mwingine; hawataomboleza, kukusanyika, au kuzikwa. Watakuwa kama samadi chini.
And the slain of the LORD shall be at that day from one end of the earth even unto the other end of the earth; they shall not be lamented, neither gathered, nor buried; they shall be dung upon the face of the ground.
34 Pigeni Yowe, wachungaji, na pigeni kelele ya kuomba msaada! Gaagaa katika ardhi, enyi mlio hodari katika kundi. Kwa kuwa siku yako ya kuuawa na kutawanywa imekuja. Utaanguka kama kondoo waliochaguliwa.
Wail, ye shepherds, and cry; and wallow yourselves in the dust, ye leaders of the flock; for the days of your slaughter are fully come, and I will break you in pieces, and ye shall fall like a precious vessel.
35 Wachungaji hawatakuwa na pa kukimbilia. Hakuna kutoroka kwa watu walio hodari katika kundi.
And the shepherds shall have no way to flee, nor the leaders of the flock to escape.
36 Kuna mlio wa wasiwasi wa wachungaji na milio ya kulalama kwa watu walio hodari katika kundi, kwa kuwa Yahweh anayaharibu malisho yao.
Hark! the cry of the shepherds, and the wailing of the leaders of the flock! For the LORD despoileth their pasture.
37 Kwa hiyo, malisho ya amani yataharibiwa kwa sababu ya hasira ya Bwana.
And the peaceable folds are brought to silence because of the fierce anger of the LORD.
38 Kama simba, ameacha shimo lake, kwa kuwa ardhi yao itakuwa kitu cha kushangaza kwa sababu ya hasira ya muonevu, kwa sababu ya ghadhabu yake kali'”
He hath forsaken His covert, as the lion; for their land is become a waste because of the fierceness of the oppressing sword, and because of His fierce anger.

< Yeremia 25 >