< Yeremia 24 >

1 Bwana alinionyeshea kitu. Tazama, vikapu viwili vya tini viliwekwa mbele ya hekalu la Bwana. (Maono haya yalitokea baada ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, kumchukua mateka Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, maofisa wa Yuda, mafundi na wafua vyuma kutoka Yerusalemu na kuwapeleka Babeli.)
to see: see me LORD and behold two pot fig to appoint to/for face: before temple LORD after to reveal: remove Nebuchadnezzar king Babylon [obj] Jeconiah son: child Jehoiakim king Judah and [obj] ruler Judah and [obj] [the] artificer and [obj] [the] locksmith from Jerusalem and to come (in): bring them Babylon
2 Kikapu kimoja cha tini kilikuwa nzuri sana, kama tini za kwanza zilizoiva, lakini kikapu kingine cha tini zilizokuwa mbaya sana zisizoweza kuliwa.
[the] pot one fig pleasant much like/as fig [the] early fig and [the] pot one fig bad: harmful much which not to eat from evil
3 Bwana akaniambia, “Unaona nini Yeremia?” Nikasema, “Tini. Tini ambazo ni nzuri sana na tini ambazo ni mbaya sana haziwezi kuliwa.”
and to say LORD to(wards) me what? you(m. s.) to see: see Jeremiah and to say fig [the] fig [the] pleasant pleasant much and [the] bad: harmful bad: harmful much which not to eat from evil
4 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
and to be word LORD to(wards) me to/for to say
5 “Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: nitawaangalia mateka wa Yuda kwa manufaa yao, kama vile tini hizi nzuri, nilipowatoa mateka kutoka hapa mpaka nchi ya Wakaldayo.
thus to say LORD God Israel like/as fig [the] pleasant [the] these so to recognize [obj] captivity Judah which to send: depart from [the] place [the] this land: country/planet Chaldea to/for welfare
6 Nitaweka macho yangu kwao wapate mema na kuwarejeshea nchi hii. Nitawajenga, wala sitawaangamiza.
and to set: make eye my upon them to/for welfare and to return: return them upon [the] land: country/planet [the] this and to build them and not to overthrow and to plant them and not to uproot
7 Nitawapanda, wala sitawang'oa. Ndipo nitawapa moyo wa kunijua; kwa kuwa mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu na mimi nitakuwa Mungu wao, hivyo watanirudia kwa moyo wao yote.
and to give: give to/for them heart to/for to know [obj] me for I LORD and to be to/for me to/for people and I to be to/for them to/for God for to return: return to(wards) me in/on/with all heart their
8 Lakini kama vile tini mbaya ambazo ni hazifai kuliwa - asema Bwana - nitatenda hivi kwa Sedekia, mfalme wa Yuda, pamoja na viongozi wake, na pamoja na wengine wa Yerusalemu ambao wanabaki katika nchi hii au kwenda kukaa katika nchi ya Misri.
and like/as fig [the] bad: harmful which not to eat from evil for thus to say LORD so to give: make [obj] Zedekiah king Judah and [obj] ruler his and [obj] remnant Jerusalem [the] to remain in/on/with land: country/planet [the] this and [the] to dwell in/on/with land: country/planet Egypt
9 Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha, wapate maafa, mbele ya falme zote duniani, aibu na somo kwa mithali, matusi, na laana mahali pote nitakapowafukuza.
and to give: make them (to/for horror *Q(K)*) to/for distress: evil to/for all kingdom [the] land: country/planet to/for reproach and to/for proverb to/for taunt and to/for curse in/on/with all [the] place which to banish them there
10 Nitatuma upanga, njaa, na tauni dhidi yao watapotelea mbali kutoka kwenye nchi niliyowapa wao na baba zao.”
and to send: depart in/on/with them [obj] [the] sword [obj] [the] famine and [obj] [the] pestilence till to finish they from upon [the] land: soil which to give: give to/for them and to/for father their

< Yeremia 24 >