< Yeremia 24 >

1 Bwana alinionyeshea kitu. Tazama, vikapu viwili vya tini viliwekwa mbele ya hekalu la Bwana. (Maono haya yalitokea baada ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, kumchukua mateka Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, maofisa wa Yuda, mafundi na wafua vyuma kutoka Yerusalemu na kuwapeleka Babeli.)
Yahweh shewed me, and lo! two baskets of figs, which had been set before the temple of Yahweh, —after that Nebuchadrezzar king of Babylon had carried away captive, Jeconiah son of Jehoiakim king of Judah and the princes of Judah and the carpenters and the smiths out of Jerusalem, and had brought them into Babylon: —
2 Kikapu kimoja cha tini kilikuwa nzuri sana, kama tini za kwanza zilizoiva, lakini kikapu kingine cha tini zilizokuwa mbaya sana zisizoweza kuliwa.
the one basket, was of very good figs, like the first-ripe figs; and, the other basket, was of very bad figs, which could not be eaten for badness.
3 Bwana akaniambia, “Unaona nini Yeremia?” Nikasema, “Tini. Tini ambazo ni nzuri sana na tini ambazo ni mbaya sana haziwezi kuliwa.”
Then said Yahweh unto me, —What canst thou see, Jeremiah? And I said, Figs: the good figs, very good; and the bad, very bad, which cannot be eaten, for badness.
4 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
Then came the word of Yahweh unto me, saying:
5 “Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: nitawaangalia mateka wa Yuda kwa manufaa yao, kama vile tini hizi nzuri, nilipowatoa mateka kutoka hapa mpaka nchi ya Wakaldayo.
Thus, saith Yahweh God of Israel, Like these good figs, so, will I regard them of Judah who are carried into captivity, whom I have sent out of this place into the land of the Chaldeans, for good.
6 Nitaweka macho yangu kwao wapate mema na kuwarejeshea nchi hii. Nitawajenga, wala sitawaangamiza.
Therefore will I set mine eye upon them for good, and will bring them back upon this land, —and will build them up, and not pull them down, and will plant them and not root them up;
7 Nitawapanda, wala sitawang'oa. Ndipo nitawapa moyo wa kunijua; kwa kuwa mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu na mimi nitakuwa Mungu wao, hivyo watanirudia kwa moyo wao yote.
and will give them a heart to know, me, that, I, am Yahweh, So shall they become my people, And, I, will become their God; for they will return unto me with all their heart.
8 Lakini kama vile tini mbaya ambazo ni hazifai kuliwa - asema Bwana - nitatenda hivi kwa Sedekia, mfalme wa Yuda, pamoja na viongozi wake, na pamoja na wengine wa Yerusalemu ambao wanabaki katika nchi hii au kwenda kukaa katika nchi ya Misri.
And like the bad figs, which cannot be eaten for badness, Surely thus, saith Yahweh—so, will I deliver up Zedekiah king of Judah, and his princes and the remnant of Jerusalem that remain in this land, and them who are dwelling in the land of Egypt;
9 Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha, wapate maafa, mbele ya falme zote duniani, aibu na somo kwa mithali, matusi, na laana mahali pote nitakapowafukuza.
yea I will deliver them up, as a terror of calamity, to all the kingdoms of the earth, —as a reproach and as a byword, as a mockery and as a contempt, in every place whither I will drive them;
10 Nitatuma upanga, njaa, na tauni dhidi yao watapotelea mbali kutoka kwenye nchi niliyowapa wao na baba zao.”
and I will send among them, sword famine and pestilence, —until they are consumed from off the soil which I gave to them and to their fathers.

< Yeremia 24 >