< Yeremia 24 >

1 Bwana alinionyeshea kitu. Tazama, vikapu viwili vya tini viliwekwa mbele ya hekalu la Bwana. (Maono haya yalitokea baada ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, kumchukua mateka Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, maofisa wa Yuda, mafundi na wafua vyuma kutoka Yerusalemu na kuwapeleka Babeli.)
The Lord revealed to me, and behold, two baskets full of figs were set before the temple of the Lord, after Nebuchadnezzar, the king of Babylon, carried away Jeconiah, the son of Jehoiakim, king of Judah, and his leaders, and the craftsmen and engravers of Jerusalem, and led them into Babylon.
2 Kikapu kimoja cha tini kilikuwa nzuri sana, kama tini za kwanza zilizoiva, lakini kikapu kingine cha tini zilizokuwa mbaya sana zisizoweza kuliwa.
One basket had exceedingly good figs, like the figs usually found early in the season, and the other basket had exceedingly bad figs, which could not be eaten because they were so bad.
3 Bwana akaniambia, “Unaona nini Yeremia?” Nikasema, “Tini. Tini ambazo ni nzuri sana na tini ambazo ni mbaya sana haziwezi kuliwa.”
And the Lord said to me: “What do you see, Jeremiah?” And I said: “Figs: the good figs are very good, and the bad figs are very bad and cannot be eaten because they are so bad.”
4 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
And the word of the Lord came to me, saying:
5 “Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: nitawaangalia mateka wa Yuda kwa manufaa yao, kama vile tini hizi nzuri, nilipowatoa mateka kutoka hapa mpaka nchi ya Wakaldayo.
“Thus says the Lord, the God of Israel: Just like these good figs, so will I regard as good the captives of Judah, whom I have sent from this place into the land of the Chaldeans.
6 Nitaweka macho yangu kwao wapate mema na kuwarejeshea nchi hii. Nitawajenga, wala sitawaangamiza.
And I will set my eyes upon them, so as to be pleased. And I will lead them back into this land. And I will build them up, and I will not tear them down. And I will plant them, and I will not uproot them.
7 Nitawapanda, wala sitawang'oa. Ndipo nitawapa moyo wa kunijua; kwa kuwa mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu na mimi nitakuwa Mungu wao, hivyo watanirudia kwa moyo wao yote.
And I will give them a heart, so that they may know me, that I am the Lord. And they will be my people, and I will be their God. For they shall return to me with their whole heart.
8 Lakini kama vile tini mbaya ambazo ni hazifai kuliwa - asema Bwana - nitatenda hivi kwa Sedekia, mfalme wa Yuda, pamoja na viongozi wake, na pamoja na wengine wa Yerusalemu ambao wanabaki katika nchi hii au kwenda kukaa katika nchi ya Misri.
And just like the very bad figs, which cannot be eaten because they are so bad, thus says the Lord: so will I regard Zedekiah, the king of Judah, and his leaders, and the rest of Jerusalem, those who have remained in this city, and those who are living in the land of Egypt.
9 Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha, wapate maafa, mbele ya falme zote duniani, aibu na somo kwa mithali, matusi, na laana mahali pote nitakapowafukuza.
And I will give them over, with upheaval and affliction, to all the kingdoms of the earth: to be a disgrace, and a parable, and a proverb, and a curse in all the places to which I have cast them out.
10 Nitatuma upanga, njaa, na tauni dhidi yao watapotelea mbali kutoka kwenye nchi niliyowapa wao na baba zao.”
And I will send among them the sword, and famine, and pestilence: until they have been worn away from the land, which I gave to them and to their fathers.”

< Yeremia 24 >