< Yeremia 23 >
1 “Ole wao wachungaji ambao huangamiza na kuwatawanya kondoo wa malisho yangu-hii ndiyo ahadi ya Bwana.”
“Woe to shepherds destroying, And scattering the flock of My pasture,” A declaration of YHWH.
2 Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi juu ya wachungaji ambao wanawachunga watu wake, “Ninyi mnawatawanya kundi langu na kuwafukuza. Hamuwajali hata kidogo. Tambueni hili! Mimi nitawalipiza uovu wa matendo yenu-hili ni tamko la Bwana.
Therefore, thus said YHWH, God of Israel, Against the shepherds who feed My people: “You have scattered My flock, and drive them away, And have not inspected them, Behold, I am charging on you the evil of your doings,” A declaration of YHWH.
3 Mimi mwenyewe nitakusanya mabaki ya kondoo wangu kutoka nchi zote nilizowafukuza, nami nitawarejesha kwenye eneo la malisho, ambako watazaa na kuongezeka.
“And I gather the remnant of My flock Out of all the lands to where I drove them, And have brought them back to their fold, And they have been fruitful, and multiplied.
4 Ndipo nitawainua wachungaji juu yao ambao watawachunga hivyo hawataogopa tena au kupotezwa. Hakuna hata mmoja atakayepotea-hili ni tamko la Bwana.
And I have raised shepherds for them, And they have fed them, And they no longer fear, nor are frightened, Nor are they lacking,” A declaration of YHWH.
5 Angalia, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-nitakapomuinulia Daudi tawi la haki. Atatawala kama mfalme; atatenda kwa busara na kusababisha hukumu na haki katika nchi.
“Behold, days are coming,” A declaration of YHWH, “And I have raised a righteous shoot to David, And a king has reigned and acted wisely, And done judgment and righteousness in the earth.
6 Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli wataishi kwa usalama. Na jina lake atakayeitwa Bwana ni haki yetu.
Judah is saved in His days, and Israel dwells confidently, And this [is] His Name that YHWH proclaims Him: Our Righteousness.
7 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-hawatasema tena, 'Kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya Misri.'
Therefore, behold, days are coming,” A declaration of YHWH, “And they no longer say, YHWH lives who brought up The sons of Israel out of the land of Egypt,
8 Badala yake watasema, 'Kama Bwana aishivyo, ambaye aliwaleta na ambaye aliwaongoza wana wa nyumba ya Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote walizofukuzwa.' Nao watakaa katika nchi yao wenyewe.”
But—YHWH lives, who brought up, And who brought in, the seed of the house of Israel, From the land of the north, And from all the lands to where I drove them, And they have dwelt on their own ground!”
9 Kuhusu manabii, moyo wangu umevunjika ndani yangu, na mifupa yangu yote imetetemeka. Nimekuwa kama mlevi, kama mtu ambaye ameshindwa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
In reference to the prophets: My heart has been broken in my midst, All my bones have fluttered, I have been as a man—a drunkard, And as a man—wine has passed over him, Because of YHWH, and of His holy words.
10 Kwa maana nchi imejaa wazinzi. Kwa sababu ya hayo nchi imeuka. Milima katika jangwa imekauka. Njia hizi za manabii ni mbaya; nguvu zao hazitumiwi kwa namna sahihi.
For the land has been full of adulterers, For the land has mourned because of these, The pleasant places of the wilderness have dried up, And their course is evil, and their might—not right.
11 Kwa maana manabii na makuhani wote wamekufuru. Nimeona uovu wao ndani ya nyumba yangu! - hili ndilo tamko la Bwana;
“For both prophet and priest have been profane, Indeed, I found their wickedness in My house,” A declaration of YHWH.
12 kwa hiyo njia yao itakuwa kama mahali pa kupumzika katika giza. Watasukumwa chini. Wao wataanguka ndani yake. Kwa maana nitawatuma mabaya juu yao katika mwaka wa adhabu yao; hili ndilo tamko la Bwana.
“Therefore their way is as slippery places to them, They are driven into thick darkness, And they have fallen in it, For I bring in calamity against them, The year of their inspection,” A declaration of YHWH.
13 kwa maana nimeona uchungu kati ya manabii huko Samaria. Walitabiri kwa Baali na wakawaongoza watu wangu Israeli kwenye njia sahihi.
“And I have seen folly in prophets of Samaria, They have prophesied by Ba‘al, And cause My people—Israel—to err.
14 Na miongoni mwa manabii huko Yerusalemu nimeona mambo ya kutisha: wanafanya uzinzi na huenda kwa udanganyifu. Wanaimarisha mikono ya waovu; hakuna mtu anarejea na kuacha uovu wake. Wote wamekuwa kama Sodoma kwangu na wenyeji wake kama Gomora!”
And I have seen a horrible thing in prophets of Jerusalem, Committing adultery, and walking falsely, Indeed, they strengthened the hands of evildoers, So that they have not turned back, Each from his wickedness, All of them have been as Sodom to me, And its inhabitants as Gomorrah.”
15 Kwa hiyo, Bwana wa majeshi asema hivi juu ya manabii, “Tazameni, nitawafanya wale magugu na kunywa maji yenye sumu, kwa maana kufuru imetoka kwa manabii wa Yerusalemu na kuingia katika nchi yote.”
Therefore, thus said YHWH of Hosts, concerning the prophets: “Behold, I am causing them to eat wormwood, And have caused them to drink water of gall, For from prophets of Jerusalem Profanity has gone forth to all the land.”
16 Bwana wa majeshi asema hivi, “Usisikilize maneno ya manabii wanaokuhubiri. Wamekudanganya! Wanatangaza maono kutoka kwenye mawazo yao wenyewe, si kwa kinywa cha Bwana.
Thus said YHWH of Hosts: “You do not listen to the words Of the prophets who are prophesying to you, They are making you vain things, They speak a vision of their own heart, Not from the mouth of YHWH.
17 Wanasema daima kwa wale wanaonidharau mimi, 'Bwana asema kutakuwa na amani kwako.' Na kila mtu anayetembea katika ukaidi wa moyo wake anasema, 'mabaya hayatakuja kwenu.'
Diligently saying to those despising, The word of YHWH: Peace is for you, And [to] everyone walking in the stubbornness of his heart, they have said: Evil does not come to you.”
18 Lakini nani amesimama katika mkutano wa baraza la Bwana? Ni nani anayeona na kusikia neno lake? Ni nani anayezingatia maneno yake na kusikiliza?
For who has stood in the counsel of YHWH, And sees and hears His word? Who has regarded My word, and listens?
19 Tazama, kuna dhoruba inayotoka kwa Bwana! Hasira yake inatoka, na dhoruba inazunguka. Inazunguka vichwa vya waovu.
Behold, a whirlwind of YHWH—Fury has gone out, even a piercing whirlwind, It stays on the head of the wicked.
20 Hasira za Bwana hazitarejea mpaka zitakapotimiza nia ya moyo wake. Katika siku za mwisho, utaelewa.
The anger of YHWH does not turn back Until His doing, and until His establishing, The thoughts of His heart, In the latter end of the days You attend to it with understanding.
21 Sikuwatuma manabii hawa. Wao tu walionekana. Sikuwahubiri jambo lolote kwao, lakini bado wanatabiri.
“I have not sent the prophets, and they have run, I have not spoken to them, and they have prophesied.
22 Kwa kuwa kama walisimama katika mkutano wangu wa baraza, wangeweza kuwasababisha watu wangu kusikia neno langu; wangewafanya wapate kuacha maneno yao mabaya na mazoea mabaya.
But if they stood in My counsel, Then they cause My people to hear My words, And they turn them back from their evil way, And from the evil of their doings.
23 Mimi ni Mungu aliye karibu-hili ni tamko la Bwana-mimi sio Mungu aliye mbali?
[Am] I a God near,” A declaration of YHWH, “And not a God far off?
24 Je, kuna mtu yeyote anayejificha mahali penye siri ili nisiweze kumwona? -Hili ndilo tamko la Bwana-Je mbingu na nchi hazikujawa nami? -hili Ndilo tamko la Bwana.
Is anyone hidden in secret places, And I do not see him?” A declaration of YHWH, “Do I not fill the heavens and the earth?” A declaration of YHWH.
25 Nimesikia yale waliyosema manabii, wale waliokuwa wanatabiri uongo kwa jina langu. Wakisema, 'Nilikuwa na ndoto!
“I have heard that which the prophets said, Who prophesy falsehood in My Name, saying, I have dreamed, I have dreamed.
26 Nilikuwa na ndoto!' Je, hii itaendelea mpaka lini, manabii wanaotabiri uongo kutoka kwa akili zao, na wanasema nini kutokana na udanganyifu mioyoni mwao?
Until when is it in the heart of the prophets? The prophets of falsehood, Indeed, prophets of the deceit of their heart,
27 Wana mpango wa kuwafanya watu wangu kusahau jina langu kwa ndoto ambazo wanazoripoti, kila mmoja kwa jirani yake, kama vile babu zao walivyosahau jina langu kwa ajili ya jina la Baali.
Who are devising to cause My people To forget My Name by their dreams, That they each recount to his neighbor, As their fathers forgot My Name for Ba‘al.
28 Nabii aliye na ndoto, aseme ndoto hiyo. Lakini yule ambaye nimemwambia kitu fulani, basi aseme neno langu kwa kweli. Je, majani yanahusiana na nafaka? - hili ni tamko la Bwana-
The prophet with whom [is] a dream, Let him recount the dream, And he with whom [is] My word, Let him truly speak My word. What does the straw [have to do] with the grain?” A declaration of YHWH.
29 Na neno langu si kama moto? -Hili ni tamko la Bwana-na kama mwamba wenye kupiga nyundo?
“Is it not thus? My word [is] as fire,” A declaration of YHWH. “And as a hammer—it breaks a rock in pieces.
30 Tazameni, ninapingana na nabii-hii ndiyo ahadi ya Bwana-yeyote anayeiba maneno kutoka kwa mtu mwingine na anasema yanatoka kwangu.
Therefore, behold, I [am] against the prophets,” A declaration of YHWH, “Each stealing My words from his neighbor.
31 Tazama, ninapingana na manabii-hili ndilo tamko la Bwana-ambao hutumia lugha zao kutabiri maneno.
Behold, I [am] against the prophets,” A declaration of YHWH, “Who are making their tongue smooth, And they affirm—an affirmation.
32 Tazameni, ninapingana na manabii wanaoota ndoto-hii ndiyo ahadi ya Bwana-na kisha kuwahubiri na kwa njia hii kuwadanganya watu wangu kwa udanganyifu wao na kujivunia. Mimi ni juu yao, kwa kuwa sikuwatuma wala kuwapa amri. Kwa hivyo hawatawasaidia watu hawa - hili ndilo tamko la Bwana.
Behold, I [am] against the prophets of false dreams,” A declaration of YHWH, “And they recount them, and cause My people to err, By their falsehoods, and by their instability, And I have not sent them, Nor have I commanded them, And they are not profitable to this people at all,” A declaration of YHWH.
33 Watu hawa au nabii au kuhani wakakuuliza, 'Je, ni nini tamko la Bwana?' basi lazima uwaambie, 'Ni tamko gani? Kwa maana nimekuacha wewe-hili ndilo tamko la Bwana.
“And when this people, or the prophet, Or a priest, asks you, saying, What [is] the burden of YHWH? Then you have said to them: You [are] the burden, and I have left you,” A declaration of YHWH.
34 Kwa habari ya manabii, makuhani, na watu wanaosema, 'Hili ndilo tamko la Bwana,' nitamuadhibu mtu huyo na nyumba yake.
“And the prophet, and the priest, and the people, That says, The burden of YHWH, I have seen after that man, and after his house.
35 Endelea kusema, kila mtu kwa jirani yake na kila mtu kwa ndugu yake, 'Bwana alijibu nini?' na 'Bwana alitangaza nini?'
Thus you each say to his neighbor, And each to his brother: What has YHWH answered? And what has YHWH spoken?
36 Lakini usizungumze tena juu ya tamko la Bwana, kwa kuwa kila tamko kutoka kwa kila mtu limekuwa ujumbe wake mwenyewe, na umepotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana wa majeshi, Mungu wetu.
And you do not mention the burden of YHWH anymore, For the burden to each is His word, And you have overturned the words of the living God, YHWH of Hosts, our God.
37 Utamuuliza nabii hivi, 'Bwana alikujibu nini? Je, Bwana alisema nini? Kisha unasema tamko kutoka kwa Bwana;
Thus you say to the prophet, What has YHWH answered you? And what has YHWH spoken?
38 lakini Bwana asema hivi, Sema hivi, “Hili ni tamko la Bwana” ingawa nimekuagiza na kusema, “Usiseme: Hili ni tamko kutoka kwa Bwana.”
And if you say, The burden of YHWH, Therefore, thus said YHWH: Because of your saying this word, The burden of YHWH, And I send to you, saying, You do not say, The burden of YHWH.
39 Kwa hiyo, angalia, nitawachukua na kukutupa mbali na mimi, pamoja na jiji ambalo nilikupa wewe na baba zako.
Therefore, behold, I have utterly taken you away, And I have sent you out, And the city that I gave to you, And to your fathers, from before My face,
40 Ndipo nitaweka aibu ya milele na fedheha juu yenu ambayo haitasahauliwa.'”
And I have put continuous reproach on you, And continuous shame that is not forgotten!”