< Yeremia 22 >
1 Bwana asema hivi, “Nenda kwenye nyumba ya mfalme wa Yuda, utangaze neno hili huko.
Assim diz o Senhor: Desce á casa do rei de Judah, e falla ali esta palavra.
2 Ukaseme, 'Ewe Mfalme wa Yuda, wewe aliyeketi kiti cha Daudi, usikilize neno la Bwana. Nisikilizeni, enyi watumishi wake, na ninyi, watu wake mnaokuja kwa malango haya.
E dize: Ouve a palavra do Senhor, ó rei de Judah, que te assentas no throno de David: tu, e os teus servos, e o teu povo, que entraes por estas portas.
3 Bwana asema hivi, “Fanya haki na uadilifu, na mtu yeyote ambaye ameibiwa-muokoeni kutoka mkononi mwa mshindani. Usimtendee mabaya mgeni yeyote katika nchi yako, au yatima au mjane. Usifanye vurugu au kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa.
Assim diz o Senhor: Fazei juizo e justiça, e livrae o roubado da mão do oppressor; e não opprimaes ao estrangeiro, nem ao orphão, nem á viuva; não façaes violencia, nem derrameis sangue innocente n'este logar.
4 Kwa kuwa mkifanya mambo hayo, basi wafalme wanaoketi kiti cha Daudi wataingia milango ya nyumba hii wakiendesha gari na farasi, yeye, watumishi wake, na watu wake!
Porque, se devéras fizerdes esta palavra, entrarão pelas portas d'esta casa os reis que se assentam no logar de David sobre o seu throno, em carros e montados em cavallos, elles, e os seus servos, e o seu povo.
5 Lakini ikiwa hamsikilizi maneno haya kutoka kwangu ambayo nimeyasema-hili ndilo tamko la Bwana-basi nyumba hii ya kifalme itaharibiwa.'”
Porém, se não derdes ouvidos a estas palavras, por mim mesmo tenho jurado, diz o Senhor, que esta casa se tornará em assolação.
6 Kwa maana Bwana asema hivi juu ya nyumba ya mfalme wa Yuda, “Wewe uko kama Gileadi, au kama kilele cha Lebanoni kwangu. Hata hivyo nitakugeuza kuwa jangwa, katika miji isiyo na wenyeji.
Porque assim diz o Senhor ácerca da casa do rei de Judah: Tu és para mim Gilead, e a altura do Libano: por certo que farei de ti um deserto e cidades deshabitadas.
7 Kwa kuwa nimewaagiza waharibifu kuja juu yenu! Watu wenye silaha zao watakata mierezi yako iliyo bora na kuiacha kuanguka kwenye moto.
Porque prepararei contra ti destruidores, cada um com as suas armas: e cortarão os teus cedros escolhidos, e lançal-os-hão no fogo.
8 Kisha mataifa mengi yatapita kwenye mji huu. Kila mtu atamwambia yule anayefuata, “Mbona Bwana amefanya hivi kwa jiji hili kuu?”
E muitas nações passarão por esta cidade, e dirá cada um ao seu companheiro: Porque obrou o Senhor assim com esta grande cidade?
9 Na mwingine atajibu, “Kwa sababu waliiacha agano la Bwana, Mungu wao, wakainama kwa miungu mingine, wakaiabudu.”
E dirão: Porque deixaram o concerto do Senhor seu Deus, e se inclinaram diante de deuses alheios, e os serviram.
10 Usilie kwa ajili ya aliyekufa. Usiomboleze kwa ajili yake. Lakini mlilie mtu yeyote anayeingia kifungoni, kwa maana hatarudi tena kuiona nchi aliyozaliwa.'
Não choreis o morto, nem o lastimeis: chorae abundantemente aquelle que sae, porque nunca mais tornará, nem verá a terra onde nasceu.
11 Maana Bwana asema hivi juu ya Yehoahazi, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyekuwa mfalme badala ya Yosia babaye, 'ametoka mahali hapa, wala hatarudi.
Porque assim diz o Senhor ácerca de Shallum, filho de Josias, rei de Judah, que reinava em logar de Josias seu pae, que saiu d'este logar: Nunca ali tornará mais.
12 Atakufa huko mahali ambapo walimchukua mateka, na hataiona tena nchi hii.'
Mas no logar para onde o levaram captivo ali morrerá, e nunca mais verá esta terra.
13 Ole mtu yeyote anayejenga nyumba yake kwa uovu na vyumba vyake vya juu katika udhalimu; ambao wengine hufanya kazi, lakini hawalipwi.
Ai d'aquelle que edifica a sua casa com injustiça, e os seus aposentos sem razão, que se serve do serviço do seu proximo sem paga, e não lhe dá o salario do seu trabalho.
14 Ole mtu yeyote atakayesema, 'Nitajenga nyumba ndefu na vyumba vya juu vipana, na hujenga madirisha mapana, na kuta zenye mwerezi, na huipaka rangi nyekundu.'
Que diz: Edificar-me-hei uma casa espaçosa, e aposentos largos: e lhe abre janellas, e está forrada de cedro, e pintada de vermelhão.
15 Je, hii ndiyo inakufanya uwe mfalme mzuri, kwamba unataka kuwa na mbao za mwerezi? Je baba yako hakula na kunywa, lakini lakini alifanya hukumu na haki? Kisha mambo yakawa mazuri kwa ajili yake.
Porventura reinarás, porque te encerras em cedro? acaso teu pae não comeu e bebeu, e não usou de juizo e justiça? e então lhe succedeu bem.
16 Alihukumu maneno ya masikini na mhitaji. Ilikuwa vizuri. Je, huku siko kunijua mimi? - hili ni tamko la Bwana.
Julgou a causa do afflicto e necessitado; então lhe succedeu bem; porventura não é isto conhecer-me? diz o Senhor.
17 Lakini hakuna kitu machoni na moyoni mwako isipokuwa wasiwasi kwa faida yako isiyo ya haki na kwa kumwaga damu isiyo na hatia, kwa ukandamizaji kuwatendea jeuri wengine.
Porém os teus olhos e o teu coração não attentam senão para a tua avareza, e para o sangue innocente, para derramal-o, e para a oppressão, e para a violencia, para os levar a effeito.
18 Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda. Hawatamwomboleza wakisema 'ole, ndugu yangu! au 'Ole, dada yangu!' Hawataomboleza kwa kusema 'Ole, bwana! ' au 'ole, utukufu!'
Portanto assim diz o Senhor ácerca de Joaquim, filho de Josias, rei de Judah: Não lamentarão por elle, dizendo: Ai, irmão meu, ou, Ai, irmã minha! nem lamentarão por elle, dizendo: Ai, Senhor, ou, Ai, sua magestade!
19 Atazikwa maziko ya punda, ataburuzwa mbali na kutupwa nje ya milango ya Yerusalemu.
Em sepultura de jumento será sepultado, arrastando-o e lançando-o para bem longe, fóra das portas de Jerusalem.
20 Panda milima ya Lebanoni piga kelele. Paza sauti yako Bashani. Piga kelele kutoka kwenye milima ya Abarimu, kwa maana marafiki zako wote wataharibiwa.
Sobe ao Libano, e clama, e levanta a tua voz em Basan, e clama pelas passagens, que já estão quebrantados os teus namorados.
21 Nilinena nawe wakati ulioko salama, lakini ukasema, 'Sitasikia.' Hii ilikuwa desturi yako tangu ujana wako, kwani hukusikiliza sauti yangu.
Fallei comtigo na tua posteridade, porém tu disseste: Não ouvirei. Este é o teu caminho, desde a tua mocidade, que nunca déste ouvidos á minha voz.
22 Upepo utawalisha wachungaji wako wote, na marafiki zako watakwenda kufungwa. Hakika wewe utakuwa na aibu na kufadhaika kwa matendo yako yote mabaya.
O vento apascentará a todos os teus pastores, e os teus namorados irão para o captiveiro: certamente então te confundirás, e te envergonharás, por causa de toda a tua maldade.
23 Wewe mfalme, wewe ambaye huishi katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni, wewe aliyefanya kiota kati ya mierezi, utakuwa na hali ya kuhurumiwa utakapopata utungu kama wakati wa kuzaa.”
Ó tu, que habitas no Libano e fazes o teu ninho nos cedros, quão lastimada serás quando te vierem as dôres e os ais como da que está de parto!
24 “Kama mimi niishivyo-hili ndilo tamko la Bwana-hata kama wewe, Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, ulikuwa alama ya mkono wangu wa kulia, ningekuangusha.
Vivo eu, diz o Senhor, que ainda que Conias, filho de Joaquim, rei de Judah, fosse o annel do sello na minha mão direita, que d'ali te arrancaria.
25 Kwa kuwa nimewatia mikono ya wale wanaotaka uhai wenu na kwenye mkono wa wale ambao mnawaogopa, hata mkononi mwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli na Wakaldayo.
E te entregarei na mão dos que buscam a tua vida, e na mão d'aquelles diante de quem tu temes, a saber, na mão de Nabucodonozor, rei de Babylonia, e na mão dos chaldeos.
26 Nitawatupa wewe na mama yako aliyekuzaa katika nchi nyingine, nchi ambayo hujazaliwa, na huko utakufa.
E lançar-te-hei, a ti e á tua mãe que te pariu, a uma terra estranha, em que não nasceste, e ali morrereis.
27 Na kuhusu eneo hili ambalo watataka kurudi, hawatarudi hapa.
E á terra, para a qual elles levantam a sua alma, para tornarem a ella, a ella não tornarão.
28 Je! Hiki ni chombo kilichodharauliwa na kilichopasuka? Je, Konia ni chombo kilichodharauliwa? Kwa nini wamemtupa yeye na wazao wake, kumpeleka katika nchi wasiyoijua?
É pois porventura este homem Conias um vil idolo quebrantado? ou um vaso de que ninguem se agrada? por que razão foram arremessados fóra, elle e a sua geração, e arrojados para uma terra que não conhecem?
29 Ee Ardhi, Ardhi, Ardhi! Sikieni neno la Bwana!
Ó terra, terra, terra! ouve a palavra do Senhor.
30 Bwana asema hivi, 'Andika juu ya mtu huyu Konia Yeye hatakuwa na mtoto. Hatafanikiwa wakati wa siku zake, wala hakuna hata mmoja kati ya uzao wake atakayefanikiwa au kuketi tena kwenye kiti cha Daudi na kutawala juu ya Yuda.'”
Assim diz o Senhor: Escrevei que este homem está roubado de filhos, homem que não prosperará nos seus dias; porque não prosperará algum da sua geração, que se assentar no throno de David, e que reinar mais em Judah.