< Yeremia 22 >

1 Bwana asema hivi, “Nenda kwenye nyumba ya mfalme wa Yuda, utangaze neno hili huko.
Thus said Jehovah: Go down to the house of the king of Judah, and there speak these words.
2 Ukaseme, 'Ewe Mfalme wa Yuda, wewe aliyeketi kiti cha Daudi, usikilize neno la Bwana. Nisikilizeni, enyi watumishi wake, na ninyi, watu wake mnaokuja kwa malango haya.
Hear the word of Jehovah, thou king of Judah, That sittest upon the throne of David, Thou, and thy servants, and thy people, Who go in and out through these gates!
3 Bwana asema hivi, “Fanya haki na uadilifu, na mtu yeyote ambaye ameibiwa-muokoeni kutoka mkononi mwa mshindani. Usimtendee mabaya mgeni yeyote katika nchi yako, au yatima au mjane. Usifanye vurugu au kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa.
Thus saith Jehovah: Do justice and righteousness; Deliver the spoiled out of the hand of the oppressor; To the stranger, the fatherless, and the widow Do no wrong, do no violence, And shed no innocent blood in this place!
4 Kwa kuwa mkifanya mambo hayo, basi wafalme wanaoketi kiti cha Daudi wataingia milango ya nyumba hii wakiendesha gari na farasi, yeye, watumishi wake, na watu wake!
For if ye shall do this, Then shall there enter in through the gates of this house Kings, who shall sit upon the throne of David, Riding in chariots and upon horses, Each one with his servants and his people.
5 Lakini ikiwa hamsikilizi maneno haya kutoka kwangu ambayo nimeyasema-hili ndilo tamko la Bwana-basi nyumba hii ya kifalme itaharibiwa.'”
But if ye will not hearken to these words, By myself do I swear, saith Jehovah, That this house shall become a desolation.
6 Kwa maana Bwana asema hivi juu ya nyumba ya mfalme wa Yuda, “Wewe uko kama Gileadi, au kama kilele cha Lebanoni kwangu. Hata hivyo nitakugeuza kuwa jangwa, katika miji isiyo na wenyeji.
For thus saith Jehovah to the house of the king of Judah: Gilead art thou to me, yea, the summit of Lebanon; Yet will I make thee a desert, As cities not inhabited.
7 Kwa kuwa nimewaagiza waharibifu kuja juu yenu! Watu wenye silaha zao watakata mierezi yako iliyo bora na kuiacha kuanguka kwenye moto.
I will appoint against thee destroyers, Every one with his weapons; And they shall cut down thy choice cedars, And cast them into the fire.
8 Kisha mataifa mengi yatapita kwenye mji huu. Kila mtu atamwambia yule anayefuata, “Mbona Bwana amefanya hivi kwa jiji hili kuu?”
And many nations shall pass by this city, And they shall say one to another, “Wherefore hath Jehovah done thus to this great city?”
9 Na mwingine atajibu, “Kwa sababu waliiacha agano la Bwana, Mungu wao, wakainama kwa miungu mingine, wakaiabudu.”
Then shall they answer: “Because they forsook the covenant of Jehovah their God, And worshipped strange gods, And served them.”
10 Usilie kwa ajili ya aliyekufa. Usiomboleze kwa ajili yake. Lakini mlilie mtu yeyote anayeingia kifungoni, kwa maana hatarudi tena kuiona nchi aliyozaliwa.'
Weep not for him that is dead, Make no lamentation for him! Weep, weep ye for him who is gone away; For he shall return no more, Nor see his native land!
11 Maana Bwana asema hivi juu ya Yehoahazi, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyekuwa mfalme badala ya Yosia babaye, 'ametoka mahali hapa, wala hatarudi.
For thus saith Jehovah Concerning Shallum, the son of Josiah, king of Judah, Who reigned instead of Josiah his father, Who went forth from this place: He shall return to it no more;
12 Atakufa huko mahali ambapo walimchukua mateka, na hataiona tena nchi hii.'
But in the place whither they have led him captive shall he die, And shall see this land no more.
13 Ole mtu yeyote anayejenga nyumba yake kwa uovu na vyumba vyake vya juu katika udhalimu; ambao wengine hufanya kazi, lakini hawalipwi.
Woe to him that buildeth his house with injustice, And his upper apartments with wrong; That exacteth a man's service without wages, And giveth him no recompense!
14 Ole mtu yeyote atakayesema, 'Nitajenga nyumba ndefu na vyumba vya juu vipana, na hujenga madirisha mapana, na kuta zenye mwerezi, na huipaka rangi nyekundu.'
That saith, “I will build me a large house, And spacious apartments,” And that cutteth out windows, And ceileth it with cedar, And painteth it with vermilion!
15 Je, hii ndiyo inakufanya uwe mfalme mzuri, kwamba unataka kuwa na mbao za mwerezi? Je baba yako hakula na kunywa, lakini lakini alifanya hukumu na haki? Kisha mambo yakawa mazuri kwa ajili yake.
Shalt thou reign because thou rivallest others in cedar? Did not thy father eat and drink? Yet he had regard to justice and equity; Therefore it was well, with him.
16 Alihukumu maneno ya masikini na mhitaji. Ilikuwa vizuri. Je, huku siko kunijua mimi? - hili ni tamko la Bwana.
He maintained the cause of the poor and needy; Then was it well with him; Was not this to know me, saith Jehovah?
17 Lakini hakuna kitu machoni na moyoni mwako isipokuwa wasiwasi kwa faida yako isiyo ya haki na kwa kumwaga damu isiyo na hatia, kwa ukandamizaji kuwatendea jeuri wengine.
But thine eyes and thy heart are only upon thine own gain, And the shedding of innocent blood, And deeds of violence and oppression.
18 Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda. Hawatamwomboleza wakisema 'ole, ndugu yangu! au 'Ole, dada yangu!' Hawataomboleza kwa kusema 'Ole, bwana! ' au 'ole, utukufu!'
Therefore thus saith Jehovah, Concerning Jehoiakim, the son of Josiah, king of Judah: They shall not lament for him, saying, “Alas, my brother!” or, “Alas, sister!” They shall not lament for him, saying, “Alas, lord!” or, “Alas, his glory!”
19 Atazikwa maziko ya punda, ataburuzwa mbali na kutupwa nje ya milango ya Yerusalemu.
With the burial of an ass shall he be buried, Dragged along and cast forth beyond the gates of Jerusalem.
20 Panda milima ya Lebanoni piga kelele. Paza sauti yako Bashani. Piga kelele kutoka kwenye milima ya Abarimu, kwa maana marafiki zako wote wataharibiwa.
Go thou up to Lebanon and cry, [[O Jerusalem!]] And upon Bashan lift up thy voice; Cry aloud from Abarim! For all thy lovers are fallen.
21 Nilinena nawe wakati ulioko salama, lakini ukasema, 'Sitasikia.' Hii ilikuwa desturi yako tangu ujana wako, kwani hukusikiliza sauti yangu.
I spake to thee in thy prosperity, But thou saidst, “I will not hear.” This hath been thy manner from thy youth; Thou hast not obeyed my voice.
22 Upepo utawalisha wachungaji wako wote, na marafiki zako watakwenda kufungwa. Hakika wewe utakuwa na aibu na kufadhaika kwa matendo yako yote mabaya.
The wind shall consume all thy shepherds, And thy lovers shall go into captivity; Then shalt thou be ashamed And confounded for all thy wickedness.
23 Wewe mfalme, wewe ambaye huishi katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni, wewe aliyefanya kiota kati ya mierezi, utakuwa na hali ya kuhurumiwa utakapopata utungu kama wakati wa kuzaa.”
O thou that dwellest in Lebanon, That makest thy nest in cedars, How wretched shalt thou be, when anguish cometh upon thee, Pain, as of a woman in travail!
24 “Kama mimi niishivyo-hili ndilo tamko la Bwana-hata kama wewe, Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, ulikuwa alama ya mkono wangu wa kulia, ningekuangusha.
As I live, saith Jehovah, Thou Coniah, son of Jehoiakim, king of Judah, Though thou wert the signet upon my right hand, Even thence would I pluck thee!
25 Kwa kuwa nimewatia mikono ya wale wanaotaka uhai wenu na kwenye mkono wa wale ambao mnawaogopa, hata mkononi mwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli na Wakaldayo.
And I will give thee into the hand of them that seek thy life, And into the hand of them that thou fearest, Even into the hand of Nebuchadnezzar, king of Babylon, And into the hand of the Chaldaeans.
26 Nitawatupa wewe na mama yako aliyekuzaa katika nchi nyingine, nchi ambayo hujazaliwa, na huko utakufa.
And I will cast thee forth, And thy mother that bore thee, Into a foreign land, Where ye were not born; And there shall ye die.
27 Na kuhusu eneo hili ambalo watataka kurudi, hawatarudi hapa.
To the land to which they desire to return, Thither shall they not return.
28 Je! Hiki ni chombo kilichodharauliwa na kilichopasuka? Je, Konia ni chombo kilichodharauliwa? Kwa nini wamemtupa yeye na wazao wake, kumpeleka katika nchi wasiyoijua?
“Is then this man Coniah a contemptible broken vessel? Is he a vessel which no man careth for? Wherefore are he and his offspring cast forth, And thrown into a land which they know not?”
29 Ee Ardhi, Ardhi, Ardhi! Sikieni neno la Bwana!
O land, land, land, hear the word of Jehovah!
30 Bwana asema hivi, 'Andika juu ya mtu huyu Konia Yeye hatakuwa na mtoto. Hatafanikiwa wakati wa siku zake, wala hakuna hata mmoja kati ya uzao wake atakayefanikiwa au kuketi tena kwenye kiti cha Daudi na kutawala juu ya Yuda.'”
Thus saith Jehovah: Write ye this man childless, A man that shall not be prosperous through his life; For none of his offspring shall prosper, So as to sit on the throne of David, And reign hereafter in Judah.

< Yeremia 22 >