< Yeremia 22 >

1 Bwana asema hivi, “Nenda kwenye nyumba ya mfalme wa Yuda, utangaze neno hili huko.
Thus said the Lord, Goe downe to the house of the King of Iudah, and speake there this thing,
2 Ukaseme, 'Ewe Mfalme wa Yuda, wewe aliyeketi kiti cha Daudi, usikilize neno la Bwana. Nisikilizeni, enyi watumishi wake, na ninyi, watu wake mnaokuja kwa malango haya.
And say, Heare the worde of the Lord, O King of Iudah, that sittest vpon the throne of Dauid, thou and thy seruants, and thy people that enter in by these gates.
3 Bwana asema hivi, “Fanya haki na uadilifu, na mtu yeyote ambaye ameibiwa-muokoeni kutoka mkononi mwa mshindani. Usimtendee mabaya mgeni yeyote katika nchi yako, au yatima au mjane. Usifanye vurugu au kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa.
Thus saith the Lord, Execute ye iudgement and righteousnes, and deliuer the oppressed from the hande of the oppressor, and vexe not the stranger, the fatherlesse, nor the widowe: doe no violence, nor sheade innocent blood in this place.
4 Kwa kuwa mkifanya mambo hayo, basi wafalme wanaoketi kiti cha Daudi wataingia milango ya nyumba hii wakiendesha gari na farasi, yeye, watumishi wake, na watu wake!
For if ye do this thing, then shall the kings sitting vpon the throne of Dauid enter in by the gates of this House, and ride vpon charets, and vpon horses, both he and his seruants and his people.
5 Lakini ikiwa hamsikilizi maneno haya kutoka kwangu ambayo nimeyasema-hili ndilo tamko la Bwana-basi nyumba hii ya kifalme itaharibiwa.'”
But if ye will not heare these wordes, I sweare by my selfe, saith the Lord, that this House shalbe waste.
6 Kwa maana Bwana asema hivi juu ya nyumba ya mfalme wa Yuda, “Wewe uko kama Gileadi, au kama kilele cha Lebanoni kwangu. Hata hivyo nitakugeuza kuwa jangwa, katika miji isiyo na wenyeji.
For thus hath the Lord spoken vpon the Kings house of Iudah, Thou art Gilead vnto me, and the head of Lebanon, yet surely I wil make thee a wildernes and as cities not inhabited,
7 Kwa kuwa nimewaagiza waharibifu kuja juu yenu! Watu wenye silaha zao watakata mierezi yako iliyo bora na kuiacha kuanguka kwenye moto.
And I will prepare destroyers against thee, euery one with his weapons, and they shall cut downe thy chiefe cedar trees, and cast them in the fire.
8 Kisha mataifa mengi yatapita kwenye mji huu. Kila mtu atamwambia yule anayefuata, “Mbona Bwana amefanya hivi kwa jiji hili kuu?”
And many nations shall passe by this citie, and they shall say euery man to his neighbour, Wherefore hath the Lord done thus vnto this great citie?
9 Na mwingine atajibu, “Kwa sababu waliiacha agano la Bwana, Mungu wao, wakainama kwa miungu mingine, wakaiabudu.”
Then shall they answere, Because they haue forsaken the couenant of the Lord their God, and worshipped other gods, and serued them.
10 Usilie kwa ajili ya aliyekufa. Usiomboleze kwa ajili yake. Lakini mlilie mtu yeyote anayeingia kifungoni, kwa maana hatarudi tena kuiona nchi aliyozaliwa.'
Weepe not for the dead, and be not moued for them, but weepe for him that goeth out: for he shall returne no more, nor see his natiue countrey.
11 Maana Bwana asema hivi juu ya Yehoahazi, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyekuwa mfalme badala ya Yosia babaye, 'ametoka mahali hapa, wala hatarudi.
For thus saith ye Lord, As touching Shallum the sonne of Iosiah King of Iudah, which reigned for Iosiah his father, which went out of this place, he shall not returne thither,
12 Atakufa huko mahali ambapo walimchukua mateka, na hataiona tena nchi hii.'
But he shall die in the place, whither they haue ledde him captiue, and shall see this lande no more.
13 Ole mtu yeyote anayejenga nyumba yake kwa uovu na vyumba vyake vya juu katika udhalimu; ambao wengine hufanya kazi, lakini hawalipwi.
Wo vnto him that buildeth his house by vnrighteousnesse, and his chambers without equitie: he vseth his neighbour without wages, and giueth him not for his worke.
14 Ole mtu yeyote atakayesema, 'Nitajenga nyumba ndefu na vyumba vya juu vipana, na hujenga madirisha mapana, na kuta zenye mwerezi, na huipaka rangi nyekundu.'
He saith, I will build me a wide house and large chambers: so he will make him selfe large windowes, and feeling with cedar, and paint them with vermilion.
15 Je, hii ndiyo inakufanya uwe mfalme mzuri, kwamba unataka kuwa na mbao za mwerezi? Je baba yako hakula na kunywa, lakini lakini alifanya hukumu na haki? Kisha mambo yakawa mazuri kwa ajili yake.
Shalt thou reigne, because thou closest thy selfe in cedar? did not thy father eate and drinke and prosper, when he executed iudgement and iustice?
16 Alihukumu maneno ya masikini na mhitaji. Ilikuwa vizuri. Je, huku siko kunijua mimi? - hili ni tamko la Bwana.
When he iudged the cause of the afflicted and the poore, he prospered: was not this because he knewe me, saith the Lord?
17 Lakini hakuna kitu machoni na moyoni mwako isipokuwa wasiwasi kwa faida yako isiyo ya haki na kwa kumwaga damu isiyo na hatia, kwa ukandamizaji kuwatendea jeuri wengine.
But thine eyes and thine heart are but only for thy couetousnesse, and for to sheade innocent blood, and for oppression, and for destruction, euen to doe this.
18 Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda. Hawatamwomboleza wakisema 'ole, ndugu yangu! au 'Ole, dada yangu!' Hawataomboleza kwa kusema 'Ole, bwana! ' au 'ole, utukufu!'
Therefore thus saith the Lord against Iehoiakim, the sonne of Iosiah king of Iudah, They shall not lament him, saying, Ah, my brother, or ah, sister: neither shall they mourne for him, saying, Ah, lord, or ah, his glorie.
19 Atazikwa maziko ya punda, ataburuzwa mbali na kutupwa nje ya milango ya Yerusalemu.
He shalbe buryed, as an asse is buryed, euen drawen and cast foorth without the gates of Ierusalem.
20 Panda milima ya Lebanoni piga kelele. Paza sauti yako Bashani. Piga kelele kutoka kwenye milima ya Abarimu, kwa maana marafiki zako wote wataharibiwa.
Goe vp to Lebanon, and cry: showte in Bashan and crye by the passages: for all thy louers are destroyed.
21 Nilinena nawe wakati ulioko salama, lakini ukasema, 'Sitasikia.' Hii ilikuwa desturi yako tangu ujana wako, kwani hukusikiliza sauti yangu.
I spake vnto thee when thou wast in prosperitie: but thou saidest, I will not heare: this hath bene thy maner from thy youth, that thou wouldest not obey my voyce.
22 Upepo utawalisha wachungaji wako wote, na marafiki zako watakwenda kufungwa. Hakika wewe utakuwa na aibu na kufadhaika kwa matendo yako yote mabaya.
The wind shall feede all thy pastors, and thy louers shall goe into captiuitie: and then shalt thou be ashamed and confounded of al thy wickednesse.
23 Wewe mfalme, wewe ambaye huishi katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni, wewe aliyefanya kiota kati ya mierezi, utakuwa na hali ya kuhurumiwa utakapopata utungu kama wakati wa kuzaa.”
Thou that dwellest in Lebanon, and makest thy nest in the cedars, howe beautiful shalt thou be when sorowes come vpon thee, as the sorowe of a woman in trauaile?
24 “Kama mimi niishivyo-hili ndilo tamko la Bwana-hata kama wewe, Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, ulikuwa alama ya mkono wangu wa kulia, ningekuangusha.
As I liue, saith the Lord, though Coniah the sonne of Iehoiakim King of Iudah, were the signet of my right hand, yet would I plucke thee thence.
25 Kwa kuwa nimewatia mikono ya wale wanaotaka uhai wenu na kwenye mkono wa wale ambao mnawaogopa, hata mkononi mwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli na Wakaldayo.
And I will giue thee into the hande of them that seeke thy life, and into the hande of them, whose face thou fearest, euen into the hand of Nebuchad-nezzar king of Babel, and into the hande of the Caldeans.
26 Nitawatupa wewe na mama yako aliyekuzaa katika nchi nyingine, nchi ambayo hujazaliwa, na huko utakufa.
And I will cause them to cary thee away, and thy mother that bare thee, into another countrey, where ye were not borne, and there shall ye die.
27 Na kuhusu eneo hili ambalo watataka kurudi, hawatarudi hapa.
But to the lande, whereunto they desire to returne, they shall not returne thither.
28 Je! Hiki ni chombo kilichodharauliwa na kilichopasuka? Je, Konia ni chombo kilichodharauliwa? Kwa nini wamemtupa yeye na wazao wake, kumpeleka katika nchi wasiyoijua?
Is not this man Coniah as a despised and broken idole? or as a vessell, wherein is no pleasure? wherefore are they caryed away, hee and his seede, and cast out into a lande that they knowe not?
29 Ee Ardhi, Ardhi, Ardhi! Sikieni neno la Bwana!
O earth, earth, earth, heare the worde of the Lord.
30 Bwana asema hivi, 'Andika juu ya mtu huyu Konia Yeye hatakuwa na mtoto. Hatafanikiwa wakati wa siku zake, wala hakuna hata mmoja kati ya uzao wake atakayefanikiwa au kuketi tena kwenye kiti cha Daudi na kutawala juu ya Yuda.'”
Thus saith the Lord, Write this man destitute of children, a man that shall not prosper in his dayes: for there shall be no man of his seede that shall prosper and sit vpon the throne of Dauid, or beare rule any more in Iudah.

< Yeremia 22 >