< Yeremia 19 >
1 Bwana akasema hivi, “Nenda ukanunue chupa ya udongo wakati ukiwa na wazee wa watu na makuhani.
Thus saith Jehovah: Go and buy an earthen bottle of the potter, And take with thee the elders of the people, And the elders of the priests,
2 Kisha uende mpaka bonde la Ben Hinomu wakati wa kuingia kwenye mlango uliovunjika wa mfinyanzi, na huko utangaza maneno nitakayokuambia.
And go forth to the valley of the son of Hinnom, At the entrance of the pottery-gate, And proclaim there the words Which I shall speak to thee.
3 Ukisema, 'Sikilizeni neno la Bwana, wafalme wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu! Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, “Tazameni, na nitaletea msiba juu ya mahali hapa, na masikio ya kila mtu anayesikia yatawaka.
Say, Hear the word of Jehovah, Ye kings of Judah and inhabitants of Jerusalem! Thus saith Jehovah of hosts, the God of Israel: Behold, I am about to bring such an evil upon this place, That whoever heareth of it, his ears shall tingle.
4 Nitafanya hivyo kwa sababu wameniacha na kudharau mahali hapa. Katika mahali hapa wanatoa sadaka kwa miungu mingine ambayo hawakuijua. Wao, baba zao, na wafalme wa Yuda pia wamejaza mahali damu isiyo na hatia.
For they have forsaken me, And have alienated this place, And have burned incense in it to strange gods, Which neither they, nor their fathers, nor the kings of Judah have known, And have filled this place with the blood of innocent children,
5 Walimjengea Baali mahali pa juu na kuwachoma watoto wao kwa moto kama sadaka za kuteketezwa kwake-kitu ambacho sijawaamuru au kutaja, wala hakuingia ndani ya akili yangu.
And have built high places to Baal, To burn their sons in the fire for burnt-offerings to Baal; Which I ordained not, and commanded not, And which never came into my mind.
6 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-ambapo mahali hapa hapataitwa tena Tofethi, bonde la Ben Hinomu, kwa kuwa litakuwa bonde la machinjo.
Therefore, behold, the days are coming, saith Jehovah, When this place shall no more be called Tophet, Nor the valley of the son of Hinnom, But the valley of Slaughter.
7 Katika mahali hapa nitatamgua mipango ya Yuda na Yerusalemu. Nitawafanya wapate kuuawa kwa upanga mbele ya adui zao na kwa mkono wa wale wanaotafuta maisha yao. Ndipo nitawapa miili yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa dunia.
For I will in this place bring to naught the plans of Judah and Jerusalem, And I will cause them to fall by the sword before their enemies, And by the hands of them that seek their lives; And their dead bodies will I give for food To the birds of heaven and the beasts of the earth.
8 Ndipo nitaifanya mji huu kuwa uharibifu na kitu cha kuzomewa, kila mtu anayepita atashangaa na kuzomea kwa sababu mateso yake yote.
And I will make this city a wonder and a hissing; Every one that passeth by it shall wonder and hiss, On account of all its plagues.
9 Nitawafanya wale nyama ya wana wao na binti zao; kila mtu atakula mwili wa jirani yake katika dhiki na katika uchungu ambao umeletwa kwao na maadui zao na wale wanaotaka maisha yao.'”
For I will cause them to eat the flesh of their sons and of their daughters, Yea, the flesh of each other shall they eat, In the straitness and the distress With which their enemies, and they that seek their lives, shall press them.
10 Kisha utavunja chupa ya udongo mbele ya watu ambao walikwenda pamoja nawe.
Then break thou the bottle Before the eyes of the men that go with thee.
11 Uwaambie,'Bwana wa majeshi asema hivi: nitafanya jambo hili kwa watu hawa na mji huu- hii ndiyo ahadi ya Bwana, kama vile Yeremia alivyovunja chupa ya udongo ili isiweze kutengenezwa tena. Watu watazika wafu huko Tofethi hata hapatabaki mahali pa kuzika.
And say to them: Thus saith Jehovah of hosts: So will I break this people and this city, As one breaks a potter's vessel which cannot be made whole again; And they shall be buried in Tophet, till there is no room to bury.
12 Hivyo ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na wenyeji wake nitakapofanya jiji hili kama Tofethi, hili ndio tamko la Bwana;
Thus will I do to this place and to its inhabitants, saith Jehovah, And I will make this city itself like Tophet;
13 kwa hiyo nyumba za Yerusalemu na wafalme wa Yuda watakuwa kama Tofethi, nyumba zote zilizo juu ya watu waovu wanaoabudu nyota zote za mbinguni na kumwaga sadaka za kinywaji kwa miungu mingine.'”
And the houses of Jerusalem and the houses of the kings of Judah shall be unclean, like the place of Tophet, All the houses upon whose roofs they have burned incense to all the host of heaven, And poured out drink-offerings to strange gods.
14 Ndipo Yeremia akatoka Tofethi, ambako Bwana amemtuma ahubiri. Akasimama katika ua wa nyumba ya Bwana, akawaambia watu wote,
Then came Jeremiah from Tophet, Whither Jehovah had sent him to prophesy, And stood in the court of the house of Jehovah, And said to all the people:
15 “Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazameni, nitawaletea mji huu na miji yake yote maafa yote niliyonena dhidi yake, kwa kuwa walifanya shingo zao kuwa ngumu na kukataa kusikiliza maneno yangu.'”
Thus saith Jehovah of hosts, the God of Israel: Behold, I am about to bring upon this city, and upon all the cities belonging to it, All the evil which I have pronounced against it; For they have made their necks stiff, And refused to hearken to my words.