< Yeremia 19 >
1 Bwana akasema hivi, “Nenda ukanunue chupa ya udongo wakati ukiwa na wazee wa watu na makuhani.
Thus said YHWH: “Go, and you have acquired a potter’s earthen vessel, and from [the] elderly of the people, and from [the] elderly of the priests,
2 Kisha uende mpaka bonde la Ben Hinomu wakati wa kuingia kwenye mlango uliovunjika wa mfinyanzi, na huko utangaza maneno nitakayokuambia.
and you have gone forth to the Valley of the Son of Hinnom, that [is] at the opening of the gate of the pottery, and have proclaimed there the words that I speak to you,
3 Ukisema, 'Sikilizeni neno la Bwana, wafalme wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu! Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, “Tazameni, na nitaletea msiba juu ya mahali hapa, na masikio ya kila mtu anayesikia yatawaka.
and have said, Hear a word of YHWH, you kings of Judah, and inhabitants of Jerusalem!” Thus said YHWH of Hosts, God of Israel: “Behold, I am bringing in evil on this place, at which the ears of everyone who is hearing it tingles,
4 Nitafanya hivyo kwa sababu wameniacha na kudharau mahali hapa. Katika mahali hapa wanatoa sadaka kwa miungu mingine ambayo hawakuijua. Wao, baba zao, na wafalme wa Yuda pia wamejaza mahali damu isiyo na hatia.
because that they have forsaken Me, and make known this place, and make incense in it to other gods, that they did not know, they and their fathers, and the kings of Judah, and they have filled this place [with] innocent blood,
5 Walimjengea Baali mahali pa juu na kuwachoma watoto wao kwa moto kama sadaka za kuteketezwa kwake-kitu ambacho sijawaamuru au kutaja, wala hakuingia ndani ya akili yangu.
and have built the high places of Ba‘al to burn their sons with fire, burnt-offerings to Ba‘al, that I did not command, nor spoke of, nor did it come up on My heart.
6 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-ambapo mahali hapa hapataitwa tena Tofethi, bonde la Ben Hinomu, kwa kuwa litakuwa bonde la machinjo.
Therefore, behold, days are coming,” a declaration of YHWH, “and this place is no longer called The Tophet and Valley of the Son of Hinnom, but Valley of the Slaughter.
7 Katika mahali hapa nitatamgua mipango ya Yuda na Yerusalemu. Nitawafanya wapate kuuawa kwa upanga mbele ya adui zao na kwa mkono wa wale wanaotafuta maisha yao. Ndipo nitawapa miili yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa dunia.
And I have made void the counsel of Judah and Jerusalem in this place, and have caused them to fall by the sword before their enemies, and by the hand of those seeking their life, and I have given their carcass for food to the bird of the heavens, and to the beast of the earth,
8 Ndipo nitaifanya mji huu kuwa uharibifu na kitu cha kuzomewa, kila mtu anayepita atashangaa na kuzomea kwa sababu mateso yake yote.
and I have made this city for a desolation, and for a hissing, everyone passing by it is astonished, and hisses for all its plagues.
9 Nitawafanya wale nyama ya wana wao na binti zao; kila mtu atakula mwili wa jirani yake katika dhiki na katika uchungu ambao umeletwa kwao na maadui zao na wale wanaotaka maisha yao.'”
And I have caused them to eat the flesh of their sons, and the flesh of their daughters, and they each eat the flesh of his friend, in the siege and in the constriction with which their enemies constrict them, and those seeking their life.”
10 Kisha utavunja chupa ya udongo mbele ya watu ambao walikwenda pamoja nawe.
“And you have broken the bottle before the eyes of the men who are going with you,
11 Uwaambie,'Bwana wa majeshi asema hivi: nitafanya jambo hili kwa watu hawa na mji huu- hii ndiyo ahadi ya Bwana, kama vile Yeremia alivyovunja chupa ya udongo ili isiweze kutengenezwa tena. Watu watazika wafu huko Tofethi hata hapatabaki mahali pa kuzika.
and have said to them, Thus said YHWH of Hosts: Thus I break this people and this city, as one breaks the potter’s vessel, that is not able to be repaired again, and in Tophet they bury—without place to bury;
12 Hivyo ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na wenyeji wake nitakapofanya jiji hili kama Tofethi, hili ndio tamko la Bwana;
so I do to this place—a declaration of YHWH—and to its inhabitants, so as to make this city as Tophet;
13 kwa hiyo nyumba za Yerusalemu na wafalme wa Yuda watakuwa kama Tofethi, nyumba zote zilizo juu ya watu waovu wanaoabudu nyota zote za mbinguni na kumwaga sadaka za kinywaji kwa miungu mingine.'”
and the houses of Jerusalem, and the houses of the kings of Judah, have been as the place of Tophet—defiled, even all the houses on whose roofs they have made incense to all the host of the heavens, so as to pour out oblations to other gods.”
14 Ndipo Yeremia akatoka Tofethi, ambako Bwana amemtuma ahubiri. Akasimama katika ua wa nyumba ya Bwana, akawaambia watu wote,
And Jeremiah comes in from Tophet, to where YHWH had sent him to prophesy, and he stands in the court of the house of YHWH, and he says to all the people:
15 “Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazameni, nitawaletea mji huu na miji yake yote maafa yote niliyonena dhidi yake, kwa kuwa walifanya shingo zao kuwa ngumu na kukataa kusikiliza maneno yangu.'”
“Thus said YHWH of Hosts, God of Israel: Behold, I am bringing to this city, and on all its cities, all the calamity that I have spoken against it, for they have hardened their neck to not hear My words!”