< Yeremia 19 >

1 Bwana akasema hivi, “Nenda ukanunue chupa ya udongo wakati ukiwa na wazee wa watu na makuhani.
Thus said the Lord, Go and buy a bottle from a maker of earthenware, and [take] some of the elders of the people, and of the elders of the priests;
2 Kisha uende mpaka bonde la Ben Hinomu wakati wa kuingia kwenye mlango uliovunjika wa mfinyanzi, na huko utangaza maneno nitakayokuambia.
And go forth unto the valley of the son of Hinnom, which is by the entry of the gate Charsith, and proclaim there the words that I will speak unto thee.
3 Ukisema, 'Sikilizeni neno la Bwana, wafalme wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu! Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, “Tazameni, na nitaletea msiba juu ya mahali hapa, na masikio ya kila mtu anayesikia yatawaka.
And say, Hear ye the word of the Lord, O kings of Judah, and inhabitants of Jerusalem, Thus hath said the Lord of hosts, the God of Israel, Behold, I will bring evil over this place, so that the ears of every one that heareth it shall tingle.
4 Nitafanya hivyo kwa sababu wameniacha na kudharau mahali hapa. Katika mahali hapa wanatoa sadaka kwa miungu mingine ambayo hawakuijua. Wao, baba zao, na wafalme wa Yuda pia wamejaza mahali damu isiyo na hatia.
For the reason that they have forsaken me, and have defiled this place, and have burnt incense in it unto other gods, which they had not known, either they or their fathers, or the kings of Judah, and have filled this place with the blood of innocents;
5 Walimjengea Baali mahali pa juu na kuwachoma watoto wao kwa moto kama sadaka za kuteketezwa kwake-kitu ambacho sijawaamuru au kutaja, wala hakuingia ndani ya akili yangu.
And they have built the high-places of Ba'al, to burn their sons with fire as burnt-offerings unto Ba'al, which I had not commanded, nor spoken, and which had not come into my mind:
6 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-ambapo mahali hapa hapataitwa tena Tofethi, bonde la Ben Hinomu, kwa kuwa litakuwa bonde la machinjo.
Therefore, behold, days are coming, saith the Lord, that this place shall no more be called The Thopheth, nor The valley of the son of Hinnom, but, The valley of slaughter.
7 Katika mahali hapa nitatamgua mipango ya Yuda na Yerusalemu. Nitawafanya wapate kuuawa kwa upanga mbele ya adui zao na kwa mkono wa wale wanaotafuta maisha yao. Ndipo nitawapa miili yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa dunia.
And I will make void the counsel of Judah and Jerusalem in this place; and I will cause them to fall by the sword before their enemies, and by the hand of those that seek their life: and I will give their carcasses as food unto the fowls of the heaven, and unto the beasts of the earth.
8 Ndipo nitaifanya mji huu kuwa uharibifu na kitu cha kuzomewa, kila mtu anayepita atashangaa na kuzomea kwa sababu mateso yake yote.
And I will render this city desolate, and an [object of] derision: every one that passeth thereby shall be astonished and hiss because of all its plagues.
9 Nitawafanya wale nyama ya wana wao na binti zao; kila mtu atakula mwili wa jirani yake katika dhiki na katika uchungu ambao umeletwa kwao na maadui zao na wale wanaotaka maisha yao.'”
And I will cause them to eat the flesh of their sons and the flesh of their daughters, and they shall eat every one the flesh of his associate, in the siege and straitness, wherewith their enemies, and those that seek their life, shall distress them.
10 Kisha utavunja chupa ya udongo mbele ya watu ambao walikwenda pamoja nawe.
Then shalt thou break the bottle before the eyes of the men that are going with thee.
11 Uwaambie,'Bwana wa majeshi asema hivi: nitafanya jambo hili kwa watu hawa na mji huu- hii ndiyo ahadi ya Bwana, kama vile Yeremia alivyovunja chupa ya udongo ili isiweze kutengenezwa tena. Watu watazika wafu huko Tofethi hata hapatabaki mahali pa kuzika.
And thou shalt say unto them, Thus hath said the Lord of hosts, In this manner will I break this people and this city, as one breaketh a potter's vessel, that cannot be restored again; and in Thopheth shall they bury, for want of room to bury.
12 Hivyo ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na wenyeji wake nitakapofanya jiji hili kama Tofethi, hili ndio tamko la Bwana;
Thus will I do unto this place, saith the Lord, and to its inhabitants, and to make this city as Thopheth:
13 kwa hiyo nyumba za Yerusalemu na wafalme wa Yuda watakuwa kama Tofethi, nyumba zote zilizo juu ya watu waovu wanaoabudu nyota zote za mbinguni na kumwaga sadaka za kinywaji kwa miungu mingine.'”
And the houses of Jerusalem, and the houses of the kings of Judah, which are unclean, shall become as the place of the Thopheth, with all the houses upon the roofs of which they have burnt incense to all the host of heaven, and have poured out drink-offerings to other gods.
14 Ndipo Yeremia akatoka Tofethi, ambako Bwana amemtuma ahubiri. Akasimama katika ua wa nyumba ya Bwana, akawaambia watu wote,
Then came Jeremiah from the Thopheth, whither the Lord had sent him to prophesy; and he placed himself in the court of the house of the Lord; and said to all the people,
15 “Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazameni, nitawaletea mji huu na miji yake yote maafa yote niliyonena dhidi yake, kwa kuwa walifanya shingo zao kuwa ngumu na kukataa kusikiliza maneno yangu.'”
Thus hath said the Lord of hosts, the God of Israel, Behold, I will bring upon this city and upon all its towns all the evil that I have spoken against it; because they have hardened their neck, so as not to hear my words.

< Yeremia 19 >