< Yeremia 19 >

1 Bwana akasema hivi, “Nenda ukanunue chupa ya udongo wakati ukiwa na wazee wa watu na makuhani.
Thus saith the Lord: Go, and take a potter’s earthen bottle, and take of the ancients of the people, and of the ancients of the priests:
2 Kisha uende mpaka bonde la Ben Hinomu wakati wa kuingia kwenye mlango uliovunjika wa mfinyanzi, na huko utangaza maneno nitakayokuambia.
And go forth into the valley of the son of Ennom, which is by the entry of the earthen gate: and there thou shalt proclaim the words that I shall tell thee.
3 Ukisema, 'Sikilizeni neno la Bwana, wafalme wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu! Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, “Tazameni, na nitaletea msiba juu ya mahali hapa, na masikio ya kila mtu anayesikia yatawaka.
And thou shalt say: Hear the word of the Lord, O ye kings of Juda, and ye inhabitants of Jerusalem: Thus saith the Lord of hosts, the God of Israel: Behold I will bring an affliction upon this place: so that whoever shall hear it, his ears shall tingle:
4 Nitafanya hivyo kwa sababu wameniacha na kudharau mahali hapa. Katika mahali hapa wanatoa sadaka kwa miungu mingine ambayo hawakuijua. Wao, baba zao, na wafalme wa Yuda pia wamejaza mahali damu isiyo na hatia.
Because they have forsaken me, and have profaned this place: and have sacrificed therein to strange gods, whom neither they nor their fathers knew, nor the kings of Juda: and they have filled this place with the blood of innocents.
5 Walimjengea Baali mahali pa juu na kuwachoma watoto wao kwa moto kama sadaka za kuteketezwa kwake-kitu ambacho sijawaamuru au kutaja, wala hakuingia ndani ya akili yangu.
And they have built the high places of Baalim, to burn their children with fire for a holocaust to Baalim: which I did not command, nor speak of, neither did it once come into my mind.
6 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-ambapo mahali hapa hapataitwa tena Tofethi, bonde la Ben Hinomu, kwa kuwa litakuwa bonde la machinjo.
Therefore behold the days come, saith the Lord, that this place shall no more be called Topheth, nor the valley of the son of Ennom, but the valley of slaughter.
7 Katika mahali hapa nitatamgua mipango ya Yuda na Yerusalemu. Nitawafanya wapate kuuawa kwa upanga mbele ya adui zao na kwa mkono wa wale wanaotafuta maisha yao. Ndipo nitawapa miili yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa dunia.
And I will defeat the counsel of Juda and of Jerusalem in this place: and I will destroy them with the sword in the sight of their enemies, and by the hands of them that seek their lives: and I will give their carcasses to be meat for the fowls of the air, and for the beasts of the earth.
8 Ndipo nitaifanya mji huu kuwa uharibifu na kitu cha kuzomewa, kila mtu anayepita atashangaa na kuzomea kwa sababu mateso yake yote.
And I will make this city an astonishent, and a hissing: every one that shall pass by it, shall be astonished, and shall hiss because of all the plagues thereof.
9 Nitawafanya wale nyama ya wana wao na binti zao; kila mtu atakula mwili wa jirani yake katika dhiki na katika uchungu ambao umeletwa kwao na maadui zao na wale wanaotaka maisha yao.'”
And I will feed them with the flesh of their sons, and with the flesh of their daughters: and they shall eat every one the flesh of his friend in the siege, and in the distress wherewith their enemies, and they that seek their lives shall straiten them.
10 Kisha utavunja chupa ya udongo mbele ya watu ambao walikwenda pamoja nawe.
And thou shalt break the bottle in the sight of the men that shall go with thee.
11 Uwaambie,'Bwana wa majeshi asema hivi: nitafanya jambo hili kwa watu hawa na mji huu- hii ndiyo ahadi ya Bwana, kama vile Yeremia alivyovunja chupa ya udongo ili isiweze kutengenezwa tena. Watu watazika wafu huko Tofethi hata hapatabaki mahali pa kuzika.
And thou shalt say to them: Thus saith the Lord of hosts: even so will I break this people, and this city, as the potter’s vessel is broken, which cannot be made whole again: and they shall be buried in Topheth, because there is no other place to bury in.
12 Hivyo ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na wenyeji wake nitakapofanya jiji hili kama Tofethi, hili ndio tamko la Bwana;
Thus will I do to this place, saith the Lord, and to the inhabitants thereof: and I will make this city as Topheth.
13 kwa hiyo nyumba za Yerusalemu na wafalme wa Yuda watakuwa kama Tofethi, nyumba zote zilizo juu ya watu waovu wanaoabudu nyota zote za mbinguni na kumwaga sadaka za kinywaji kwa miungu mingine.'”
And the houses of Jerusalem, and the houses of Juda shall be unclean as the place of Topheth: all the houses upon whose roots they have sacrificed to all the host of heaven, and have poured out drink offerings to strange gods.
14 Ndipo Yeremia akatoka Tofethi, ambako Bwana amemtuma ahubiri. Akasimama katika ua wa nyumba ya Bwana, akawaambia watu wote,
Then Jeremias came from Topheth, whither the Lord had sent him to prophecy, and he stood in the court of the house of the Lord, and said to all people:
15 “Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazameni, nitawaletea mji huu na miji yake yote maafa yote niliyonena dhidi yake, kwa kuwa walifanya shingo zao kuwa ngumu na kukataa kusikiliza maneno yangu.'”
Thus saith the Lord of hosts, the God of Israel: Behold I will bring in upon this city, and upon all the cities thereof all the evils that I have spoken against it: because they have hardened their necks, and they might not hear my words.

< Yeremia 19 >