< Yeremia 18 >

1 Neno la Bwana lilimjia Yeremia, kusema,
Cette parole fut [adressée] de par l'Eternel à Jérémie, disant:
2 “Simama, uende kwa nyumba ya mfinyanzi; kwa maana nitakusikilizisha neno langu huko.
Lève-toi, et descends dans la maison d'un potier, et là je te ferai entendre mes paroles.
3 Basi, nikaenda nyumbani kwa mfinyanzi, na tazama! Mfinyanzi alikuwa akifanya kazi kwenye gurudumu la mfinyanzi.
Je descendis donc dans la maison d'un potier, et voici, il faisait son ouvrage, assis sur sa selle.
4 Lakini chombo cha udongo ambacho alikuwa akikifinyanga kiliharibika mkononi mwake, kwa hiyo alibadili mawazo yake na akafanya kitu kingine ambacho kilionekana kuwa kizuri machoni pake.
Et le vase qu'il faisait de l'argile qui [était] en sa main, fut gâté, et il en fit encore un autre vase, comme il lui sembla bon de [le] faire.
5 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
Alors la parole de l'Eternel me fut [adressée], en disant:
6 “Je, siwezi kuwa kama huyu mfinyanzi kwenu, nyumba ya Israeli? Angalia! Kama udongo katika mkono wa mfinyanzi-ndivyo ulivyo mkononi mwangu, nyumba ya Israeli.
Maison d'Israël, ne vous pourrai-je pas faire comme a fait ce potier; dit l'Eternel? voici, comme l'argile est dans la main d'un potier, ainsi êtes-vous dans ma main, maison d'Israël.
7 Kwa wakati mmoja, ninaweza kutangaza jambo fulani juu ya taifa au ufalme, kwamba nitaufukuza, kuuvunja, au kuuharibu.
En un instant je parlerai contre une nation, et contre un Royaume, pour arracher, pour démolir, et pour détruire;
8 Lakini kama taifa ambalo nimefanya tamko hilo linageuka na kuacha maovu yake, basi nitaghairi nisitende maafa niliyokuwa nimepanga.
Mais si cette nation contre laquelle j'aurai parlé se détourne du mal qu'elle aura fait, je me repentirai aussi du mal que j'avais pensé de lui faire.
9 Wakati mwingine, ninaweza kutangaza jambo fulani kuhusu taifa au ufalme, kwamba nitaujenga au kuupanda.
Et si en un instant je parle d'une nation et d'un Royaume, pour l'édifier et pour le planter;
10 Lakini ikiwa watafanya mabaya machoni pangu kwa kutosikiliza sauti yangu, basi nitaghairi mema ambayo nilikuwa nimewaambia nitawafanyia.
Et que cette nation fasse ce qui me déplaît, en sorte qu'elle n'écoute point ma voix, je me repentirai aussi du bien que j'avais dit que je lui ferais.
11 Basi sasa, waambie watu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu, ukisema, 'Bwana asema hivi: Tazameni, nitawaangamiza. Mimi ni karibu kufinyanga mabaya dhidi yenu. Tubuni, kila mtu kutoka njia yake mbaya, hivyo njia zako na matendo yako yatakuletea mema.'
Or donc parle maintenant aux hommes de Juda, et aux habitants de Jérusalem, en disant: ainsi a dit l'Eternel: voici, je projette du mal contre vous, et je forme un dessein contre vous; abandonnez donc maintenant chacun sa mauvaise voie, et changez votre voie, et vos actions.
12 Lakini watasema, 'Hili halina maana. Tutafanya kulingana na mipango yetu wenyewe. Kila mmoja wetu atafanya mabaya kwa kuufuata uchupavu wa moyo wake.'
Et ils répondirent: il n'y a plus d'espérance; c'est pourquoi nous suivrons nos pensées, et chacun de nous fera selon la dureté de son cœur mauvais.
13 Kwa hiyo Bwana asema hivi, 'Uliza watu wa mataifa, ambao wamewahi kusikia habari kama hii? Bikira wa Israeli amefanya kitendo cha kutisha.
C'est pourquoi ainsi a dit l'Eternel: Demandez maintenant aux nations qui a entendu de telles choses? la vierge d'Israël a fait une chose très-énorme.
14 Je, theluji ya Lebanoni imetoka milima yenye miamba juu ya pande zake? Je, mito ya mlima inayotoka mbali iliharibiwa, mito hiyo ya baridi?
N'abandonnera-t-on pas la neige du Liban pour la roche du champ? et ne laissera-t-on pas les eaux qui ne sont point naturelles, et qui sont froides, [encore] qu'elles coulent?
15 Hata hivyo watu wangu wamesahau. Wamefanya sadaka kwa sanamu zisizo na maana na wamefanya mashaka katika njia zao; wameacha njia za kale za kutembea katika njia ndogo.
Mais mon peuple m'a oublié, et il a fait des parfums à ce qui n'est que vanité, et qui les a fait broncher dans leurs voies, pour [les faire retirer] des sentiers anciens, afin de marcher dans les sentiers d'un chemin qui n'est point battu;
16 Nchi yao itakuwa ya hofu, kitu cha kuzomewa milele. Kila mtu atakayepita karibu naye atashuhudia na kutingisha kichwa chake.
Pour faire venir sur leur pays une désolation et un opprobre perpétuel; [tellement que] quiconque passera par là en sera étonné, et branlera la tête.
17 Nitawaangamiza mbele ya adui zao kama upepo wa mashariki. Nitawageuzia kisogo, wala sio uso wangu, siku ya msiba wao.'”
Je les disperserai devant l'ennemi, comme par le vent d'Orient; je leur tournerai le dos, au jour de leur calamité.
18 Basi watu wakasema, “Njoni, tufanye njama dhidi ya Yeremia, maana sheria haitapotea kabisa kwa makuhani, wala ushauri kutoka kwa wenye hekima, au maneno ya manabii. Njoo, mshambulie kwa maneno yetu na tusisikilize tena chochote anachosema.”
Et ils ont dit: venez, et faisons quelques machinations contre Jérémie; car la Loi ne se perdra pas chez le Sacrificateur, ni le conseil chez le Sage, ni la parole chez le Prophète; venez, et frappons-le de la langue, et ne soyons point attentifs à aucun de ses discours.
19 Sikiliza, Ee Bwana! Na kusikiliza sauti ya adui yangu.
Eternel, entends-moi, et écoute la voix de ceux qui plaident contre moi.
20 Je, maafa kutoka kwao itakuwa malipo yangu kwa kuwa mema kwao? Kwa maana wamenichimbia shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele yako ili niseme mema kwa ajili yao na kugeuza ghadhabu yako isiwapate.
Le mal sera-t-il rendu pour le bien? car ils ont creusé une fosse pour mon âme. Souviens-toi que je me suis présenté devant toi afin de parler pour leur bien, [et] afin de détourner d'eux ta grande colère.
21 Basi uwape watoto wao njaa, na uwatie mikononi mwa wale wanaotumia upanga. Basi, waache wanawake wao wafiwe na kuwa wajane, na watu wao watauawa, na vijana wao wauawe kwa upanga wa vita.
C'est pourquoi livre leurs enfants à la famine, et fais couler leur sang à coups d'épée; que leurs femmes soient privées d'enfants, et veuves, et que leurs maris soient mis à mort; et leurs jeunes gens tués avec l'épée dans la bataille.
22 Kelele ya kusikitisha isikiwe kutoka katika nyumba zao, kama utakapoleta washambuliaji ghafla juu yao. Kwa kuwa wamechimba shimo kunikamata na wameficha mitego katika miguu yangu.
Que le cri soit ouï de leurs maisons, quand tu auras fait venir subitement des troupes contre eux; parce qu'ils ont creusé une fosse pour me prendre, et qu'ils ont tendu des filets à mes pieds.
23 Lakini wewe, Bwana, unajua mipango yao yote dhidi yangu ya kuniua. Usisamehe uovu na dhambi zao. Usiondoe dhambi zao mbali nawe. Badala yake, waache waangamizwe mbele yako. Tenda juu yao wakati wa ghadhabu yako.
Or tu sais, ô Eternel! que tout leur conseil est contre moi pour me mettre à mort; ne sois point apaisé à l'égard de leur iniquité, et n'efface point leur péché de devant ta face, mais qu'on les fasse tomber en ta présence; agis contre eux au temps de ta colère.

< Yeremia 18 >