< Yeremia 18 >
1 Neno la Bwana lilimjia Yeremia, kusema,
The word that came unto Jeremiah from Yahweh, saying:
2 “Simama, uende kwa nyumba ya mfinyanzi; kwa maana nitakusikilizisha neno langu huko.
Arise and go down to the house of the potter, —and, there, will I cause thee to hear my words.
3 Basi, nikaenda nyumbani kwa mfinyanzi, na tazama! Mfinyanzi alikuwa akifanya kazi kwenye gurudumu la mfinyanzi.
So I went down, to the house of the potter, —and there he was! making a piece of work on the wheels,
4 Lakini chombo cha udongo ambacho alikuwa akikifinyanga kiliharibika mkononi mwake, kwa hiyo alibadili mawazo yake na akafanya kitu kingine ambacho kilionekana kuwa kizuri machoni pake.
Then was marred, the vessel that he was making, while yet it was clay in the hand of the potter, —so he turned and made of it another vessel, as seemed right in the eyes of the potter to make it.
5 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
Then came the word of Yahweh unto me, saying:
6 “Je, siwezi kuwa kama huyu mfinyanzi kwenu, nyumba ya Israeli? Angalia! Kama udongo katika mkono wa mfinyanzi-ndivyo ulivyo mkononi mwangu, nyumba ya Israeli.
Like this potter, can I not deal with you O house of Israel? Demandeth Yahweh: Lo! as clay in the hand of the potter, So, are, ye, in my hand O house of Israel.
7 Kwa wakati mmoja, ninaweza kutangaza jambo fulani juu ya taifa au ufalme, kwamba nitaufukuza, kuuvunja, au kuuharibu.
The moment I speak, concerning a nation or concerning a kingdom, —to pull up and to break down, and to destroy;
8 Lakini kama taifa ambalo nimefanya tamko hilo linageuka na kuacha maovu yake, basi nitaghairi nisitende maafa niliyokuwa nimepanga.
and that nation return from its wickedness against whom I have spoken, then will I repent concerning the calamity which I had devised to bring upon it.
9 Wakati mwingine, ninaweza kutangaza jambo fulani kuhusu taifa au ufalme, kwamba nitaujenga au kuupanda.
And, the moment I speak, concerning a nation or concerning a kingdom, —to build and to plant;
10 Lakini ikiwa watafanya mabaya machoni pangu kwa kutosikiliza sauti yangu, basi nitaghairi mema ambayo nilikuwa nimewaambia nitawafanyia.
and it commit wickedness in mine eyes, in not hearkening unto my voice, then will I repent concerning the good wherewith I had said I would do it good.
11 Basi sasa, waambie watu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu, ukisema, 'Bwana asema hivi: Tazameni, nitawaangamiza. Mimi ni karibu kufinyanga mabaya dhidi yenu. Tubuni, kila mtu kutoka njia yake mbaya, hivyo njia zako na matendo yako yatakuletea mema.'
Now, therefore, I pray thee, speak unto the men of Judah and concerning the inhabitants of Jerusalem saying, Thus, saith Yahweh, —Lo! I am fashioning against you calamity, and devising against you, a device, —Return I pray you every man from his wicked way, And amend your ways and your doings.
12 Lakini watasema, 'Hili halina maana. Tutafanya kulingana na mipango yetu wenyewe. Kila mmoja wetu atafanya mabaya kwa kuufuata uchupavu wa moyo wake.'
And, since they will say, Hopeless! For after our own devices, will we walk, And, every one, the stubbornness of his own wicked heart, will we do!
13 Kwa hiyo Bwana asema hivi, 'Uliza watu wa mataifa, ambao wamewahi kusikia habari kama hii? Bikira wa Israeli amefanya kitendo cha kutisha.
Therefore, Thus saith Yahweh, Ask I pray you among the nations, —Who hath heard such things as these? A very horrible thing, hath, the virgin, Israel done!
14 Je, theluji ya Lebanoni imetoka milima yenye miamba juu ya pande zake? Je, mito ya mlima inayotoka mbali iliharibiwa, mito hiyo ya baridi?
Shall the snow of Lebanon, fail from the rock of the field? Or shall waters from afar, deep, overflowing, be dried up?
15 Hata hivyo watu wangu wamesahau. Wamefanya sadaka kwa sanamu zisizo na maana na wamefanya mashaka katika njia zao; wameacha njia za kale za kutembea katika njia ndogo.
Yet my people have forgotten me, Unto vanity, have they been burning incense; And it hath caused them to stumble In their ways The roads of age-past times, To walk in by-paths—A way not cast up.
16 Nchi yao itakuwa ya hofu, kitu cha kuzomewa milele. Kila mtu atakayepita karibu naye atashuhudia na kutingisha kichwa chake.
To make their land a desolation The hissings of age-abiding times, —Every one that passeth by her, shall be astonished and wag his head.
17 Nitawaangamiza mbele ya adui zao kama upepo wa mashariki. Nitawageuzia kisogo, wala sio uso wangu, siku ya msiba wao.'”
Like an east wind, will I scatter them before the enemy, —The back and not the face, will I let them see in the day of their distress.
18 Basi watu wakasema, “Njoni, tufanye njama dhidi ya Yeremia, maana sheria haitapotea kabisa kwa makuhani, wala ushauri kutoka kwa wenye hekima, au maneno ya manabii. Njoo, mshambulie kwa maneno yetu na tusisikilize tena chochote anachosema.”
Then said they, —Come ye and let us devise against Jeremiah devices, For the law shall not perish from the priest, Nor, counsel, from the wise, Nor, the word from the prophet: Come and let as smite him with the tongue, And let us not give ear to any of his words!
19 Sikiliza, Ee Bwana! Na kusikiliza sauti ya adui yangu.
Give thou ear O Yahweh unto me, —And hearken unto the voice of mine accusers.
20 Je, maafa kutoka kwao itakuwa malipo yangu kwa kuwa mema kwao? Kwa maana wamenichimbia shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele yako ili niseme mema kwa ajili yao na kugeuza ghadhabu yako isiwapate.
Shall, evil, be recompensed for good? For they have digged a pit for my life, —Remember how I stood before thee To speak in their behalf what was good! To turn back thine indignation from them.
21 Basi uwape watoto wao njaa, na uwatie mikononi mwa wale wanaotumia upanga. Basi, waache wanawake wao wafiwe na kuwa wajane, na watu wao watauawa, na vijana wao wauawe kwa upanga wa vita.
Therefore, give thou up their sons to the famine And deliver them into the hands of the sword, And let their, wives, become, childless and widows, And let, their men, be slain by death, Their young men be smitten by the sword in battle.
22 Kelele ya kusikitisha isikiwe kutoka katika nyumba zao, kama utakapoleta washambuliaji ghafla juu yao. Kwa kuwa wamechimba shimo kunikamata na wameficha mitego katika miguu yangu.
Let there be heard a cry out of their houses, When thou shalt bring in upon them a troop, suddenly, —Because they digged a pit to capture me, And snares, did they hide for my feet.
23 Lakini wewe, Bwana, unajua mipango yao yote dhidi yangu ya kuniua. Usisamehe uovu na dhambi zao. Usiondoe dhambi zao mbali nawe. Badala yake, waache waangamizwe mbele yako. Tenda juu yao wakati wa ghadhabu yako.
But, thou, O Yahweh, knowest all their counsels against me to put me to death, Put thou no propitiatory-covering over their iniquity, And their sin from before thee, do not thou blot out, —But let them be overthrown before thee, In the time of thine anger, deal thou effectively with them.