< Yeremia 17 >
1 “Dhambi ya Yuda imeandikwa kwa kalamu ya chuma yenye ncha ya almasi. Imechongwa kwenye kibao cha mioyo yao na kwenye pembe za madhabahu zako.
[the] sin of Judah [is] inscribed with a stylus of iron with a point of flint [is] engraved on [the] tablet of heart their and to [the] horns of altars your.
2 Watoto wao wanakumbuka madhabahu zao na miti yao ya Ashera kwa miti ya majani kwenye milima mirefu.
When remember children their altars their and Asherah poles their at tree[s] luxuriant on hills high.
3 Mlima wangu katika nchi ya wazi na mali yako yote pamoja na hazina zako zote, nitakupa kama nyara kwa wengine. Hiyo ndiyo thamani ya maeneo yako ya juu na dhambi iliyo katika maeneo yako yote.
Mountain my in the field wealth your all treasures your to plunder I will give high places your for sin in all territories your.
4 Utapoteza urithi niliokupa. Nitakutumikisha kwa adui zako katika nchi ambayo hujui, kwa maana umewasha moto katika ghadhabu yangu, ambao utakawaka milele.”
And you will let fall and in you from inheritance your which I gave to you and I will make serve you enemies your in land which not you know for a fire you have kindled in anger my until perpetuity it will burn.
5 Bwana asema, “Mtu anayemtegemea mwanadamu amelaaniwa; amfanyaye mwanadamu kuwa nguvu yake na kugeuza moyo wake mbali na Bwana.
Thus - he says Yahweh [is] cursed the man who he trusts in humankind and he makes flesh strength his and from Yahweh it turns aside heart his.
6 Kwa maana atakuwa kama msitu mdogo katika Araba na hawezi kuona kitu kizuri kikija. Atakaa katika maeneo ya mawe jangwani, nchi isiyokuwa na wakazi.
And he will be like a bush in the desert plain and not he will see if it will come good and he will dwell parched places in the wilderness a land of saltiness and not anyone dwells.
7 Lakini mtu anayemtegemea Bwana amebarikiwa, kwa kuwa Bwana ndiye tumaini lake.
[is] blessed The man who he trusts in Yahweh and he is Yahweh trust his.
8 Kwa maana atakuwa kama mmea karibu na maji kando ya mto; mizizi yake itaenea. Hawezi kuona joto likija, kwa kuwa majani yake yatakuwa mabichi. Kisha mwaka wa ukame hawezi kuwa na wasiwasi, wala hataacha kuzalisha matunda.
And he will be like a tree - planted at water and [which] at a stream it sends out roots its and not (he will see *Q(K)*) if it will come heat and it will be leafage its luxuriant and in a year of drought not it will be anxious and not it will cease from producing fruit.
9 Moyo ni mdanganyifu zaidi kuliko kitu kingine chochote. Una mgonjwa; ni nani anayeweza kuelewa?
[is] deceitful The heart more than everything and [is] incurable it who? will he know it.
10 Mimi ni Bwana, ninayechunguza akili, ambaye hujaribu viuno. Ninampa kila mtu kulingana na njia zake, kulingana na matunda ya matendo yake.
I Yahweh [am] searching [the] heart [am] testing [the] kidneys to give to everyone (according to ways his *Q(K)*) according to [the] fruit of deeds his.
11 kama Kware akusanyaye mayai asiyotaga. Mtu anaweza kuwa tajiri kwa udhalimu, lakini wakati nusu ya siku zake ukipita, utajiri huo utamuacha, na mwishowe atakuwa mpumbavu.”
A partridge [which] it gathers a brood and not it has laid [one who] makes wealth and not with justice in [the] middle of (days his *Q(K)*) it will leave him and at end his he will be a fool.
12 “Mahali pa hekalu letu ni kiti cha enzi cha utukufu, kilichoinuliwa tangu mwanzo.
[is] a throne of Glory a high place from first [time] [the] place of sanctuary our.
13 Bwana ni tumaini la Israeli. Wote ambao wanakuacha watakuwa na aibu. Wale walio katika nchi ambao wanageuka kutoka kwako watauliwa. Kwa maana wamwacha Bwana, chemchemi ya maji yaliyo hai.
O hope of Israel O Yahweh all [those who] forsake you they will be ashamed (and disloyal [ones] my *Q(K)*) in the land they will be written down for they have forsaken [the] spring of water living Yahweh.
14 Niponye, Bwana, na mimi nitaponywa! Niokoe mimi, nami nitaokolewa. Kwa maana wewe ndio wimbo wangu wa sifa.
Heal me O Yahweh so I may be healed save me so let me be saved for [are] praise my you.
15 Tazama, wananiambia, 'Neno la Bwana liko wapi? Hebu lije!'
Here! they [are] saying to me where? [is] [the] word of Yahweh let it come please.
16 Mimi sikuwahi kuacha kuwa mchungaji nyuma yako. Sikuitamani siku ya maafa. Unajua yaliyotoka mdomoni mwangu. Yalifanyika mbele ya uwepo wako.
And I not I have hastened - from a shepherd after you and a day incurable not I have desired you you know [the] utterance of lips my before face your it was.
17 Usiwe sababu ya hofu kwangu. Wewe ni kimbilio langu siku ya msiba.
May not you become to me an object of terror [are] refuge my you in a day of calamity.
18 Waaibike watu wanaoniudhi, lakini nisiaibike mimi. Wataogopa, lakini usiache nifadhaike. Tuma siku ya maafa dhidi yao na kuwaangamiza maradufu.”
Let them be put to shame pursuers my and may not I be put to shame I let them be dismayed they and may not I be dismayed I bring on them a day of calamity and double destruction destroy them.
19 Bwana akaniambia hivi: “Nenda ukasimame katika lango la watu ambako wafalme wa Yuda wanaingia na kutoka, basi katika malango mengine yote ya Yerusalemu.
Thus he said Yahweh to me go and you will stand in [the] gate of [the] sons of (the people *Q(K)*) which they go in it [the] kings of Judah and which they go out in it and in all [the] gates of Jerusalem.
20 Uwaambie, 'Sikieni neno la Bwana, wafalme wa Yuda, na ninyi watu wote wa Yuda, na kila mtu wa Yerusalemu atakayeingia kwa njia ya malango haya.
And you will say to them hear [the] word of Yahweh O kings of Judah and all Judah and all [the] inhabitants of Jerusalem who go in the gates these.
21 Bwana asema hivi: “Jihadharini kwa ajili ya maisha yenu na msichukue mzigo siku ya sabato ili muilete katika malango ya Yerusalemu.
Thus he says Yahweh take heed to lives your and may not you carry a burden on [the] day of the sabbath and you will bring [it] in [the] gates of Jerusalem.
22 Wala msilete mzigo nje ya nyumba zenu siku ya sabato. Msifanye kazi yoyote, lakini muitenge siku ya Sabato, kama nilivyowaagiza wazee wako kufanya.'”
And not you must bring out a burden from houses your on [the] day of the sabbath and any work not you must do and you will set apart as holy [the] day of the sabbath just as I commanded ancestors your.
23 Hawakusikiliza wala kutaega masikio yao, lakini walifanya shingo zao kuwa ngumu ili wasinisikilize wala kukubali maonyo.
And not they listened and not they inclined ear their and they stiffened neck their to not (to listen *Q(K)*) and to not to accept correction.
24 Itatokea kwamba ikiwa mtanisikiliza kweli-hili ndilo tamko la Bwana-na msilete mzigo kwenye malango ya jiji hili siku ya sabato lakini badala yake mkatenga siku ya sabato kwa Bwana na msifanye kazi yoyote juu yake -
And it will be certainly [if] you will listen! to me [the] utterance of Yahweh to not - to bring a burden in [the] gates of the city this on [the] day of the sabbath and to set apart as holy [the] day of the sabbath to not to do (on it *Q(K)*) any work.
25 basi wafalme, wakuu, na wale wanaokaa kiti cha Daudi wataingia malango ya mji huu kwa magari na farasi, wao na viongozi wao, watu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu. Na mji huu utakaa milele.
And they will come in [the] gates of the city this kings - and princes [who] sit on [the] throne of David [who] ride - in chariot[s] and on horses they and officials their everyone of Judah and [the] inhabitants of Jerusalem and it will remain the city this for ever.
26 Watakuja kutoka miji ya Yuda na kutoka pande zote za Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na visiwa vya chini, kutoka milimani na kutoka kaskazini, wakileta sadaka za kuteketezwa, dhabihu, sadaka za nafaka na ubani, sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana.
And they will come from [the] cities of Judah and from round about Jerusalem and from [the] land of Benjamin and from the Shephelah and from the hill country and from the Negev [those who] bring burnt offering and sacrifice and grain offering and frankincense and [those who] bring a thank-offering [the] house of Yahweh.
27 Lakini ikiwa hamtasikiliza-kutakasa siku ya Sabato, kutochukua mizigo nzito, wala msiingie milango ya Yerusalemu siku ya sabato, nitawasha moto katika malango yake, nao utaangamiza majumba kuteketeza ngome za Yerusalemu, na hauwezi kuzimika.
And if not you will listen to me to set apart as holy [the] day of the sabbath and to not - to carry a burden and to go in [the] gates of Jerusalem on [the] day of the sabbath and I will kindle a fire in gates its and it will consume [the] fortresses of Jerusalem and not it will be extinguished.