< Yeremia 13 >

1 Bwana aliniambia hivi, “Nenda ukape nguo ya kitani na kuiweka karibu na kiuno chako, lakini usiiweke kwenye maji kwanza.”
This is what the Lord told me to do: Go and buy yourself a linen loincloth and put it on, but don't wash it.
2 Kwa hiyo nilinunua vazi kama vile Bwana alivyoagiza, na nikafunga karibu na kiuno changu.
So I went and bought a loincloth as the Lord had instructed me, and I put it on.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema,
Then the Lord gave me another message:
4 “Twaa vazi lako ulilolinunua lililo karibu na kiuno chako, uinuke, ukasafiri mpaka Frati. Ukaifiche huko katika mwamba wa jabali.
Take the loincloth that you bought and put on, and go immediately to the River Perath and hide it there in a hole among the rocks.
5 Basi nikaenda na kuificha katika Frati kama vile Bwana alivyoniamuru.
So I went and hid it at the River Perath, as the Lord had told me.
6 Baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, “Simama, urudi Frati. Ukaichukue nguo ambayo nilikuambia ufiche.”
A long time later the Lord told me, Go to Perath, and get the loincloth that I ordered you to hide there.
7 Kwa hiyo nikarudi Frati na kuchimba na kuchukua nguo mahali pale nilipoificha. Lakini tazama! Nguo hiyo ilikuwa imeharibika; haikuwa nzuri kabisa.
I went to Perath and dug up the loincloth, and removed it from where I'd hidden it. Obviously it was ruined—completely useless.
8 Ndipo neno la Bwana likanijia tena, kusema,
Then a message from the Lord came to me:
9 “Bwana asema hivi, Nitakiangamiza kiburi cha Yuda na Yerusalemu.
This is what the Lord says: I will ruin the arrogance of Judah and the great arrogance of Jerusalem in exactly the same way.
10 Watu hawa waovu wanaokataa kusikia neno langu, ambao huenda katika ugumu wa mioyo yao, ambao hufuata miungu mingine ili kuabudu na kuinama-watakuwa kama hii nguo isiyofaa kwa lolote.
These evil people refuse to listen to what I tell them. They follow their own stubborn and evil thinking and run off to worship other gods—they will be like this loincloth, completely useless.
11 Kwa maana kama vile vazi lililofungwa kwenye viuno vya mtu, ndivyo nimefainya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda zimefungwa kwangu- hili ndilo tamko la Bwana-wawe watu wangu, ili kunifanya jina, sifa, na heshima. Lakini hawakunisikiliza.
In the same way that a loincloth holds tightly to the body, so I made all the people of Israel and Judah hold tightly to me, declares the Lord. Then they could have been my people, representing me, giving me honor and praise. But they refused to listen.
12 Basi uwaambie neno hili, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi Kila chupa itajazwa divai.' Watakuambia, 'Je, hatujui kwamba kila chupa itajazwa divai?'
So tell them this is what the Lord, the God of Israel, says: Every wine jar shall be filled with wine. When they reply, “Don't we know that already? Of course every wine jar should be filled with wine!”
13 Basi uwaambie,' Bwana asema hivi: Tazama, nitawajaza kila mkaaji wa nchi hii ulevi, na wafalme wanaokaa kiti cha Daudi, na makuhani, na manabii, na wenyeji wote wa Yerusalemu.
then tell them that this is what the Lord says: I'm going to make everyone who lives in this land drunk—the kings sitting on David's throne, the priests, the prophets, and all the people of Jerusalem.
14 Ndipo nitawagonganisha kila mtu na mwenzake baba na watoto wao pamoja; hili ndilo tamko la Bwana-sitawahurumia au kuwa na huruma, wala sitawarehemu kutoka kwenye uharibifu.
I'm going to smash them against each other like wine jars, both parents and children, declares the Lord. I won't let any mercy or pity or compassion stop me from destroying them.
15 Sikilizeni na makini. Msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amesema.
Listen and pay attention. Don't be arrogant, for the Lord has spoken.
16 Mtukuze Bwana, Mungu wako, kabla ya hajaleta giza, na kabla ya kuifanya miguu yako kuwa na mashaka juu ya milima wakati wa jioni. Kwa maana unatarajia mwanga, lakini ataugeuza kuwa mahali pa giza, na kuwa giza nene.
Honor the Lord your God before he brings the darkness, before you trip and fall in the twilight on the mountains. You long for light to come, but he send only gloom and complete darkness.
17 Kwa hiyo ikiwa husikilizi, nitaomboleza peke yangu kwa sababu ya kiburi chako. Hakika macho yangu yatalia na kutoa machozi, kwa sababu kundi la Bwana limechukuliwa mateka.
But if you refuse to listen, I will weep secretly inside because of your pride. My tears pouring down because the Lord's flock has been captured.
18 “Mwambieni mfalme na mama wa malkia, 'Jinyenyekezeni, na kukaa chini, kwa maana taji juu ya kichwa chako, kiburi chako na utukufu wako, umeanguka.'
Tell the king and the queen mother: Get down from your thrones, because your splendid crowns have fallen from your heads.
19 Miji ya Negebu itafungwa, bila mtu wa kufungua. Yuda watachukuliwa mateka, wote uhamishoni.
The towns in the Negev are surrounded; no one can get through to them. The whole of Judah has been taken away into exile, everyone has been exiled.
20 Inua macho yako na angalia wale wanaokuja kutoka kaskazini. Je, ni kundi gani alilokupa, kundi ambalo lilikuwa zuri sana kwako?
Look up and you'll see the invaders coming from the north. Where is the flock that was given to you to look after? Where are the sheep you were so proud of?
21 Je, unasema nini wakati Mungu anawaweka wale ambao uliwafundisha kuwa marafiki? Je, huu si mwanzo wa maumivu ya utungu ambayo yatakuchukua kama mwanamke aliye katika kuzaa?
What are you going to say when he puts your enemies in charge of you, people you once counted as your friends? Won't you suffer pains like a woman in labor?
22 Kisha unaweza kusema moyoni mwako, 'Kwa nini mambo haya yanatokea kwangu?' Itakuwa kwa uovu wa maovu yako ambapo marinda yako yamefunuliwa na umeumizwa.
If you say to yourself, Why has this happened to me? it's because you have been so wicked. That's why your skirts were stripped off and you were raped.
23 Je, watu wa Kushi hubadilisha rangi yao ya ngozi, au chui hubadilisha madoa yake? Ikiwa ndivyo, basi wewe mwenyewe, ingawa unazoea uovu, utaweza kufanya mema.
Can Ethiopians change the color of their skin? Can a leopard change its spots? In the same way you can't change and do good because you're so used to doing evil.
24 Kwa hiyo nitawaangamiza kama makapi ambayo yanaangamia katika upepo wa jangwa.
I'm going to scatter you like chaff blown away by the desert wind.
25 Hii ndiyo niliyokupa, sehemu ambayo nimekuagiza kwako-hili ndilo tamko la Bwana - kwa sababu umenisahau na kuamini katika udanganyifu.
This is what's going to happen to you; this is what I have decided to do to you, declares the Lord, because you have forgotten me and believed in lies.
26 Kwa hiyo mimi mwenyewe nitaondoa nguo zako, na sehemu zako za siri zitaonekana.
I will pull your skirts up over your face, so you will be seen naked and ashamed.
27 Uzinzi na ubembe wako, aibu ya tabia yako ya uasherati kwenye milima na katika mashamba! Nitayafanya yaonekane, mambo haya ya machukizo! Ole wako, Yerusalemu! Hutaki kuwa safi. Je! Hili litaendelea kwa muda gani?”
I watched your acts of adultery and lust, how you prostituted yourselves shamelessly, worshiping idols on the hills and in the fields. Yes, I saw the disgusting things you did. Disaster is coming to you, Jerusalem! How long are you going to remain unclean?

< Yeremia 13 >