< Yeremia 13 >

1 Bwana aliniambia hivi, “Nenda ukape nguo ya kitani na kuiweka karibu na kiuno chako, lakini usiiweke kwenye maji kwanza.”
Thus says the Lord to me: “Go, and obtain for yourself a linen waistcloth. And you shall place it over your loins, and you shall not put it into water.”
2 Kwa hiyo nilinunua vazi kama vile Bwana alivyoagiza, na nikafunga karibu na kiuno changu.
And so I obtained a waistcloth, according to the word of the Lord, and I placed it around my loins.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema,
And the word of the Lord came to me a second time, saying:
4 “Twaa vazi lako ulilolinunua lililo karibu na kiuno chako, uinuke, ukasafiri mpaka Frati. Ukaifiche huko katika mwamba wa jabali.
“Take the waistcloth, which you obtained, which is around your loins, and, rising up, go to the Euphrates, and hide it there in an opening of the rock.”
5 Basi nikaenda na kuificha katika Frati kama vile Bwana alivyoniamuru.
And so I went, and I hid it by the Euphrates, just as the Lord had instructed me.
6 Baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, “Simama, urudi Frati. Ukaichukue nguo ambayo nilikuambia ufiche.”
And it happened that, after many days, the Lord said to me: “Rise up, go to the Euphrates, and take from there the waistcloth, which I instructed you to hide there.”
7 Kwa hiyo nikarudi Frati na kuchimba na kuchukua nguo mahali pale nilipoificha. Lakini tazama! Nguo hiyo ilikuwa imeharibika; haikuwa nzuri kabisa.
And so I went to the Euphrates, and I dug up and took the waistcloth from the place where I had hidden it. And behold, the waistcloth had rotted, so that it was not fit for any use.
8 Ndipo neno la Bwana likanijia tena, kusema,
And the word of the Lord came to me, saying:
9 “Bwana asema hivi, Nitakiangamiza kiburi cha Yuda na Yerusalemu.
“Thus says the Lord: In the same way, I will cause the arrogance of Judah and the arrogance of Jerusalem to rot.
10 Watu hawa waovu wanaokataa kusikia neno langu, ambao huenda katika ugumu wa mioyo yao, ambao hufuata miungu mingine ili kuabudu na kuinama-watakuwa kama hii nguo isiyofaa kwa lolote.
This most wicked people, they are not willing to listen to my words, for they walk in the depravity of their own heart, and they have gone after strange gods, so as to serve them and to adore them. And so, they will become like this waistcloth, which is not fit for any use.
11 Kwa maana kama vile vazi lililofungwa kwenye viuno vya mtu, ndivyo nimefainya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda zimefungwa kwangu- hili ndilo tamko la Bwana-wawe watu wangu, ili kunifanya jina, sifa, na heshima. Lakini hawakunisikiliza.
For just as the waistcloth clings to the loins of a man, so have I brought close to me the entire house of Israel and the entire house of Judah, says the Lord, so that they would be to me: a people, and a name, and a praise, and a glory. But they did not listen.
12 Basi uwaambie neno hili, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi Kila chupa itajazwa divai.' Watakuambia, 'Je, hatujui kwamba kila chupa itajazwa divai?'
Therefore, you shall speak to them this word: Thus says the Lord, the God of Israel: ‘Every bottle will be filled with wine.’ And they will say to you: ‘Are we ignorant that every bottle will be filled with wine?’
13 Basi uwaambie,' Bwana asema hivi: Tazama, nitawajaza kila mkaaji wa nchi hii ulevi, na wafalme wanaokaa kiti cha Daudi, na makuhani, na manabii, na wenyeji wote wa Yerusalemu.
And you shall say to them: Thus says the Lord: Behold, I will fill all the inhabitants of this land, and the kings from the stock of David who sit upon his throne, and the priests, and the prophets, and all the inhabitants of Jerusalem, unto inebriation.
14 Ndipo nitawagonganisha kila mtu na mwenzake baba na watoto wao pamoja; hili ndilo tamko la Bwana-sitawahurumia au kuwa na huruma, wala sitawarehemu kutoka kwenye uharibifu.
And I will scatter them, a man from his brother, and fathers and sons similarly, says the Lord. I will not spare them, and I will not pardon them, and I will not take pity, so as not to destroy them.”
15 Sikilizeni na makini. Msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amesema.
Hear and pay close attention. Do not choose to lift yourself up, for the Lord has spoken.
16 Mtukuze Bwana, Mungu wako, kabla ya hajaleta giza, na kabla ya kuifanya miguu yako kuwa na mashaka juu ya milima wakati wa jioni. Kwa maana unatarajia mwanga, lakini ataugeuza kuwa mahali pa giza, na kuwa giza nene.
Give glory to the Lord your God, before darkness falls, and before your feet stumble on the darkened mountains. You will expect light, but he will turn it into the shadow of death and into utter darkness.
17 Kwa hiyo ikiwa husikilizi, nitaomboleza peke yangu kwa sababu ya kiburi chako. Hakika macho yangu yatalia na kutoa machozi, kwa sababu kundi la Bwana limechukuliwa mateka.
But if you will not listen to this, then my soul will weep in secret before the face of your pride. It will weep bitterly, and my eyes will flow with tears, because the flock of the Lord has been taken captive.
18 “Mwambieni mfalme na mama wa malkia, 'Jinyenyekezeni, na kukaa chini, kwa maana taji juu ya kichwa chako, kiburi chako na utukufu wako, umeanguka.'
“Say to the king and to the female ruler: Humble yourselves, sit down. For the crown of your glory has gone down from your head.
19 Miji ya Negebu itafungwa, bila mtu wa kufungua. Yuda watachukuliwa mateka, wote uhamishoni.
The cities of the south have been closed, and there is no one who may open them. All of Judah has been taken away into complete captivity.
20 Inua macho yako na angalia wale wanaokuja kutoka kaskazini. Je, ni kundi gani alilokupa, kundi ambalo lilikuwa zuri sana kwako?
Lift up your eyes and see, you who are arriving from the north. Where is the flock that was given to you, your famous cattle?
21 Je, unasema nini wakati Mungu anawaweka wale ambao uliwafundisha kuwa marafiki? Je, huu si mwanzo wa maumivu ya utungu ambayo yatakuchukua kama mwanamke aliye katika kuzaa?
What will you say when he visits upon you? For you have taught them against you, and you have instructed them with your own head. Will not pains take hold of you, as with a woman in labor?
22 Kisha unaweza kusema moyoni mwako, 'Kwa nini mambo haya yanatokea kwangu?' Itakuwa kwa uovu wa maovu yako ambapo marinda yako yamefunuliwa na umeumizwa.
But if you say in your heart, ‘Why have these things happened to me?’ it is because of the greatness of your iniquity that your shame has been uncovered and the soles of your feet have been defiled.
23 Je, watu wa Kushi hubadilisha rangi yao ya ngozi, au chui hubadilisha madoa yake? Ikiwa ndivyo, basi wewe mwenyewe, ingawa unazoea uovu, utaweza kufanya mema.
If the Ethiopian is able to change his skin, or the leopard is able to change his spots, then you also may be able to do well, though you have learned evil.
24 Kwa hiyo nitawaangamiza kama makapi ambayo yanaangamia katika upepo wa jangwa.
And I will scatter them like chaff, which is carried away by the wind in the desert.
25 Hii ndiyo niliyokupa, sehemu ambayo nimekuagiza kwako-hili ndilo tamko la Bwana - kwa sababu umenisahau na kuamini katika udanganyifu.
This is your lot, and this is the portion of your measure from me, says the Lord, because you have forgotten me, and you have had confidence in what is false.
26 Kwa hiyo mimi mwenyewe nitaondoa nguo zako, na sehemu zako za siri zitaonekana.
Therefore, I have even bared your thighs before your face, and your shame has been seen.
27 Uzinzi na ubembe wako, aibu ya tabia yako ya uasherati kwenye milima na katika mashamba! Nitayafanya yaonekane, mambo haya ya machukizo! Ole wako, Yerusalemu! Hutaki kuwa safi. Je! Hili litaendelea kwa muda gani?”
For I have seen your adulteries, and your neighing for the wickedness of your fornication, and your abominations upon the hills in the field. Woe to you, Jerusalem! How much longer before you will be made clean after me?”

< Yeremia 13 >