< Yeremia 11 >
1 Hili ndilo neno lililojia Yeremia kutoka kwa Bwana, akasema,
La parole fut [adressée] à Jérémie par l'Éternel, en disant:
2 “Sikiliza maneno ya agano hili, uwaambie kila mtu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu.
Ecoutez les paroles de cette alliance, et prononcez[-les] aux hommes de Juda, et aux habitants de Jérusalem.
3 Uwaambie, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: na alaaniwe yeyote asiyesikiliza maneno ya agano hili.
Tu leur diras donc: ainsi a dit l'Eternel le Dieu d'Israël: maudit soit l'homme qui n'écoutera point les paroles de cette alliance;
4 Hili ndilo agano nililowaamuru baba zenu walishike siku nilipowatoa kutoka katika nchi ya Misri, kutoka tanuru ya chuma. Nikawaambia, “Sikilizeni sauti yangu na mfanye mambo yote kama nilivyowaamuru, kwa kuwa mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.”
Laquelle j'ai ordonnée à vos pères, le jour que je les ai retirés du pays d'Egypte, du fourneau de fer, en disant: Ecoutez ma voix, et faites toutes les choses que je vous ai commandées, et vous serez mon peuple, et je serai votre Dieu.
5 Nisikilizeni ili nipate kukitimiza kiapo nilichoapa kwa baba zenu, kiapo kwamba nitawapa nchi iliyojaa maziwa na asali kama ilivyo leo.'” Kisha mimi Yeremia nikajibu na kusema, “Ndio, Bwana!”
Afin que je ratifie le serment que j'ai fait à vos pères, de leur donner un pays découlant de lait et de miel, comme [il paraît] aujourd'hui. Et je répondis, et dis: Ainsi soit-il! ô Eternel!
6 Bwana akaniambia, “Hubiri habari hizi yote katika miji ya Yuda, na katika njia za Yerusalemu. Sema, “Sikilizeni maneno ya agano hili na mkayafanye.
Puis l'Eternel me dit: crie toutes ces paroles par les villes de Juda, et par les rues de Jérusalem, en disant: écoutez les paroles de cette alliance, et les faites;
7 Kwa maana nimewaagiza wazee wenu tangu siku ile niliyowaleta kutoka nchi ya Misri hadi wakati huu wa sasa, nimewaonya mara kwa mara na kusema, “Sikilizeni sauti yangu.'”
Car j'ai sommé expressément vos pères au jour que je les ai fait monter du pays d'Egypte jusqu’à aujourd'hui, me levant dès le matin, et les sommant, en disant: écoutez ma voix.
8 Lakini hawakusikiliza au wala kutega masikio yao. Kila mtu amekuwa akitembea katika ukaidi wa moyo wake mbaya. Kwa hiyo nilileta laana zote katika agano hili nililoamuru kuja juu yao. Lakini watu bado hawakuitii.”
Mais ils ne l'ont pas écoutée, et n'y ont point incliné leur oreille, mais ils ont marché chacun suivant la dureté de leur cœur mauvais; c'est pourquoi j'ai fait venir sur eux toutes les paroles de cette alliance, laquelle je leur avais commandé de garder, et qu'ils n'ont point gardée.
9 Kisha Bwana akaniambia, “Njama imeonekana kati ya watu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu.
Et l'Eternel me dit: il y a une conjuration parmi les hommes de Juda, et parmi les habitants de Jérusalem.
10 Wameugeukia uovu wa mababu zao wa mwanzo, ambao walikataa kusikiliza neno langu, ambao badala yake walifuata miungu mingine ili kuabudu. Waisraeli na nyumba ya Yuda walivunja agano langu nililoweka na baba zao.
Ils sont retournés aux iniquités de leurs ancêtres, qui ont refusé d'écouter mes paroles, et qui sont allés après d'autres dieux pour les servir; la maison d'Israël et la maison de Juda ont enfreint mon alliance, que j'avais traitée avec leurs pères.
11 Kwa hiyo Bwana asema hivi, 'Tazameni, nitawaletea majanga juu yao, majanga ambayo hawataweza kuyaepuka. Ndipo wataniita, lakini sitawasikiliza.
C'est pourquoi ainsi a dit l'Eternel: voici, je m'en vais faire venir sur eux un mal duquel ils ne pourront sortir; ils crieront vers moi, mais je ne les exaucerai point.
12 Miji ya Yuda na wenyeji wa Yerusalemu watakwenda na kuiita miungu ambayo walitoa sadaka, lakini hakika hawatawaokoa wakati wa majanga yao.
Et les villes de Juda et les habitants de Jérusalem s'en iront, et crieront vers les dieux auxquels ils font leurs parfums; mais ces dieux-là ne les délivreront nullement au temps de leur affliction.
13 Kwa kuwa idadi ya miungu yako ewe Yuda imeongezeka sawa na idadi ya miji yako. Na umefanya idadi ya madhabahu ya aibu huko Yerusalemu, madhabahu ya kufukiza uvumba kwa Baali, sawa na idadi ya njia zake.
Car, ô Juda! tu as eu autant de dieux que de villes; et toi, Jérusalem, tu as dressé autant d'autels aux choses honteuses, que tu as de rues, des autels, [dis-je], pour faire des parfums à Bahal.
14 Kwa hiyo wewe mwenyewe, Yeremia, usiwaombee watu hawa. Lazima usiomboleze au kuomba kwa niaba yao. Kwa maana siwezi kusikiliza wakati wananiita katika majanga yao.
Toi donc ne fais point de requête pour ce peuple, et ne jette point de cri, ni ne fais point de prière pour eux; car je ne les exaucerai point au temps qu'ils crieront vers moi dans leur calamité.
15 Mpendwa wangu anafanya nini nyumbani kwangu, ikiwa amekuwa na nia mbaya? Nyama za sadaka yako hazitakusaidia. Unafurahi kwa sababu ya matendo yako mabaya.
Qu'est-ce que mon bien-aimé a à faire dans ma maison, que tant de gens se servent d'elle pour y faire leurs complots? la chair sainte est transportée loin de toi, et encore quand tu fais mal, tu t'égayes.
16 Katika siku za nyuma Bwana alikuita mti wa mzeituni wenye majani, mzuri wenye matunda mazuri. Lakini atawasha moto juu yake ambayo itaonekana kama sauti ya dhoruba; matawi yake yatavunjika.
L'Eternel avait appelé ton nom, Olivier vert [et] beau, à cause du beau fruit; [mais] au son d'un grand bruit il y a allumé le feu, et ses branches ont été rompues.
17 Kwa maana Bwana wa majeshi, aliyekua amekusudia maafa juu yako, kwa sababu ya matendo mabaya ambayo nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda wamefanya-wamenikasirisha kwa kumtolea Baali sadaka.'”
Car l'Eternel des armées, qui t'a plantée, a prononcé du mal contre toi, à cause de la malice de la maison d'Israël, et de la maison de Juda, qu'ils ont commise contre eux-mêmes, jusqu’à m'irriter en faisant des parfums à Bahal.
18 Bwana alinijulisha mambo haya, kwa hiyo nakayajua. Wewe, Bwana, umenifanya nione matendo yao.
Et l'Eternel me l'a donné à connaître, et je l'ai connu; et tu m'as fait voir leurs actions.
19 Nilikuwa kama kondoo mpole unayeongozwa na mchinjaji. Sikujua kwamba walikuwa wameunda mipango dhidi yangu, “Hebu tuangamize mti na matunda yake! Hebu tumkatilie mbali na nchi ya walio hai ili jina lake lisikumbukwe tena.
Mais moi, comme un agneau, [ou comme] un bœuf qui est mené pour être égorgé, je n'ai point su qu'ils eussent fait contre moi quelque machination, [en disant]: détruisons l'arbre avec son fruit, et l'exterminons de la terre des vivants, et qu'on ne se souvienne plus de son nom.
20 Lakini Bwana wa majeshi ndiye mwamuzi mwenye haki ambaye huchunguza moyo na akili. Mimi nitashuhudia kisasi chako dhidi yao, kwa kuwa nimekuletea kesi yangu kwako.
Mais toi, Eternel des armées, qui juges justement, et qui sondes les reins et le cœur, fais que je voie la vengeance que tu feras d'eux; car je t'ai découvert ma cause.
21 Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya watu wa Anathothi, wanaotafuta uhai wako, “wanasema, 'Usifanye unabii kwa jina la Bwana, usije utakufa kwa mkono wetu.'
C'est pourquoi ainsi a dit l'Eternel, touchant les gens de Hanathoth, qui cherchent ta vie, et qui disent: ne prophétise plus au Nom de l'Eternel, et tu ne mourras point par nos mains.
22 Kwa hiyo Bwana wa majeshi asema hivi, 'Tazameni, nitawaadhibu. Vijana wao wenye nguvu watakufa kwa upanga. Wana wao na binti zao watakufa kwa njaa.
C'est pourquoi [donc] ainsi a dit l'Eternel des armées: voici, je vais les punir; les jeunes gens mourront par l'épée, leurs fils et leurs filles mourront par la famine;
23 Hakuna hata mmoja atakayeachwa, kwa maana nitaleta maafa dhidi ya watu wa Anathothi, mwaka wa adhabu yao.'”
Et il ne restera rien d'eux, car je ferai venir le mal sur les gens de Hanathoth, en l'année de leur visitation.