< Yeremia 11 >

1 Hili ndilo neno lililojia Yeremia kutoka kwa Bwana, akasema,
[the] word which to be to(wards) Jeremiah from with LORD to/for to say
2 “Sikiliza maneno ya agano hili, uwaambie kila mtu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu.
to hear: hear [obj] word [the] covenant [the] this and to speak: speak them to(wards) man: anyone Judah and upon to dwell Jerusalem
3 Uwaambie, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: na alaaniwe yeyote asiyesikiliza maneno ya agano hili.
and to say to(wards) them thus to say LORD God Israel to curse [the] man which not to hear: hear [obj] word [the] covenant [the] this
4 Hili ndilo agano nililowaamuru baba zenu walishike siku nilipowatoa kutoka katika nchi ya Misri, kutoka tanuru ya chuma. Nikawaambia, “Sikilizeni sauti yangu na mfanye mambo yote kama nilivyowaamuru, kwa kuwa mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.”
which to command [obj] father your in/on/with day to come out: send I [obj] them from land: country/planet Egypt from furnace [the] iron to/for to say to hear: hear in/on/with voice my and to make: do [obj] them like/as all which to command [obj] you and to be to/for me to/for people and I to be to/for you to/for God
5 Nisikilizeni ili nipate kukitimiza kiapo nilichoapa kwa baba zenu, kiapo kwamba nitawapa nchi iliyojaa maziwa na asali kama ilivyo leo.'” Kisha mimi Yeremia nikajibu na kusema, “Ndio, Bwana!”
because to arise: establish [obj] [the] oath which to swear to/for father your to/for to give: give to/for them land: country/planet to flow: flowing milk and honey like/as day: today [the] this and to answer and to say amen LORD
6 Bwana akaniambia, “Hubiri habari hizi yote katika miji ya Yuda, na katika njia za Yerusalemu. Sema, “Sikilizeni maneno ya agano hili na mkayafanye.
and to say LORD to(wards) me to call: call out [obj] all [the] word [the] these in/on/with city Judah and in/on/with outside Jerusalem to/for to say to hear: hear [obj] word [the] covenant [the] this and to make: do [obj] them
7 Kwa maana nimewaagiza wazee wenu tangu siku ile niliyowaleta kutoka nchi ya Misri hadi wakati huu wa sasa, nimewaonya mara kwa mara na kusema, “Sikilizeni sauti yangu.'”
for to testify to testify in/on/with father your in/on/with day to ascend: establish I [obj] them from land: country/planet Egypt and till [the] day: today [the] this to rise and to testify to/for to say to hear: obey in/on/with voice my
8 Lakini hawakusikiliza au wala kutega masikio yao. Kila mtu amekuwa akitembea katika ukaidi wa moyo wake mbaya. Kwa hiyo nilileta laana zote katika agano hili nililoamuru kuja juu yao. Lakini watu bado hawakuitii.”
and not to hear: obey and not to stretch [obj] ear their and to go: walk man: anyone in/on/with stubbornness heart their [the] bad: evil and to come (in): bring upon them [obj] all word [the] covenant [the] this which to command to/for to make: do and not to make: do
9 Kisha Bwana akaniambia, “Njama imeonekana kati ya watu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu.
and to say LORD to(wards) me to find conspiracy in/on/with man: anyone Judah and in/on/with to dwell Jerusalem
10 Wameugeukia uovu wa mababu zao wa mwanzo, ambao walikataa kusikiliza neno langu, ambao badala yake walifuata miungu mingine ili kuabudu. Waisraeli na nyumba ya Yuda walivunja agano langu nililoweka na baba zao.
to return: turn back upon iniquity: crime father their [the] first which to refuse to/for to hear: hear [obj] word my and they(masc.) to go: follow after God another to/for to serve: minister them to break house: household Israel and house: household Judah [obj] covenant my which to cut: make(covenant) with father their
11 Kwa hiyo Bwana asema hivi, 'Tazameni, nitawaletea majanga juu yao, majanga ambayo hawataweza kuyaepuka. Ndipo wataniita, lakini sitawasikiliza.
to/for so thus to say LORD look! I to come (in): bring to(wards) them distress: harm which not be able to/for to come out: come from her and to cry out to(wards) me and not to hear: hear to(wards) them
12 Miji ya Yuda na wenyeji wa Yerusalemu watakwenda na kuiita miungu ambayo walitoa sadaka, lakini hakika hawatawaokoa wakati wa majanga yao.
and to go: went city Judah and to dwell Jerusalem and to cry out to(wards) [the] God which they(masc.) to offer: offer to/for them and to save not to save to/for them in/on/with time distress: harm their
13 Kwa kuwa idadi ya miungu yako ewe Yuda imeongezeka sawa na idadi ya miji yako. Na umefanya idadi ya madhabahu ya aibu huko Yerusalemu, madhabahu ya kufukiza uvumba kwa Baali, sawa na idadi ya njia zake.
for number city your to be God your Judah and number outside Jerusalem to set: make altar to/for shame altar to/for to offer: offer to/for Baal
14 Kwa hiyo wewe mwenyewe, Yeremia, usiwaombee watu hawa. Lazima usiomboleze au kuomba kwa niaba yao. Kwa maana siwezi kusikiliza wakati wananiita katika majanga yao.
and you(m. s.) not to pray about/through/for [the] people [the] this and not to lift: loud about/through/for them cry and prayer for nothing I to hear: hear in/on/with time to call: call to they to(wards) me about/through/for distress: harm their
15 Mpendwa wangu anafanya nini nyumbani kwangu, ikiwa amekuwa na nia mbaya? Nyama za sadaka yako hazitakusaidia. Unafurahi kwa sababu ya matendo yako mabaya.
what? to/for beloved my in/on/with house: temple my to make: do she [the] plot [to] [the] many and flesh holiness to pass from upon you for distress: harm your then to exult
16 Katika siku za nyuma Bwana alikuita mti wa mzeituni wenye majani, mzuri wenye matunda mazuri. Lakini atawasha moto juu yake ambayo itaonekana kama sauti ya dhoruba; matawi yake yatavunjika.
olive luxuriant beautiful fruit appearance to call: call by LORD name your to/for voice: sound tumult great: large to kindle fire upon her and to shatter branch his
17 Kwa maana Bwana wa majeshi, aliyekua amekusudia maafa juu yako, kwa sababu ya matendo mabaya ambayo nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda wamefanya-wamenikasirisha kwa kumtolea Baali sadaka.'”
and LORD Hosts [the] to plant [obj] you to speak: promise upon you distress: harm in/on/with because of distress: evil house: household Israel and house: household Judah which to make: do to/for them to/for to provoke me to/for to offer: offer to/for Baal
18 Bwana alinijulisha mambo haya, kwa hiyo nakayajua. Wewe, Bwana, umenifanya nione matendo yao.
and LORD to know me and to know [emph?] then to see: see me deed their
19 Nilikuwa kama kondoo mpole unayeongozwa na mchinjaji. Sikujua kwamba walikuwa wameunda mipango dhidi yangu, “Hebu tuangamize mti na matunda yake! Hebu tumkatilie mbali na nchi ya walio hai ili jina lake lisikumbukwe tena.
and I like/as lamb tame to conduct to/for to slaughter and not to know for upon me to devise: devise plot to ruin tree in/on/with food his and to cut: eliminate him from land: country/planet alive and name his not to remember still
20 Lakini Bwana wa majeshi ndiye mwamuzi mwenye haki ambaye huchunguza moyo na akili. Mimi nitashuhudia kisasi chako dhidi yao, kwa kuwa nimekuletea kesi yangu kwako.
and LORD Hosts to judge righteousness to test kidney and heart to see: see vengeance your from them for to(wards) you to reveal: reveal [obj] strife my
21 Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya watu wa Anathothi, wanaotafuta uhai wako, “wanasema, 'Usifanye unabii kwa jina la Bwana, usije utakufa kwa mkono wetu.'
to/for so thus to say LORD upon human Anathoth [the] to seek [obj] soul: life your to/for to say not to prophesy in/on/with name LORD and not to die in/on/with hand our
22 Kwa hiyo Bwana wa majeshi asema hivi, 'Tazameni, nitawaadhibu. Vijana wao wenye nguvu watakufa kwa upanga. Wana wao na binti zao watakufa kwa njaa.
to/for so thus to say LORD Hosts look! I to reckon: punish upon them [the] youth to die in/on/with sword son: child their and daughter their to die in/on/with famine
23 Hakuna hata mmoja atakayeachwa, kwa maana nitaleta maafa dhidi ya watu wa Anathothi, mwaka wa adhabu yao.'”
and remnant not to be to/for them for to come (in): bring distress: harm to(wards) human Anathoth year punishment their

< Yeremia 11 >