< Yakobo 1 >

1 Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, kwa makabila kumi na mbili yaliyotawanyika, salaam.
This letter comes from James, servant of God and of the Lord Jesus Christ. It is sent to the twelve tribes scattered abroad. Best wishes to you!
2 Hesabuni kuwa ni furaha zaidi, ndugu zangu, mnapopita katika matatizo mbali mbali,
My friends, choose to stay happy even when all kinds of troubles come your way,
3 mkijua kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huwapa uvumilivu.
because you know that endurance comes from dealing with challenges to your trust in God.
4 Acheni uvumilivu uikamilishe kazi yake, kwamba muweze kukomaa kikamilifu, bila kupungukiwa katika lolote.
Let your endurance become as strong as possible, so that you will be completely mature, without any shortcomings.
5 Lakini kama mtu kati yenu anahitaji hekima, aiombe kutoka kwa Mungu, ambaye hutoa kwa ukarimu na pasipo kukemea kwa wote wamwombao, na atawapa hekima.
If any of you need wisdom, ask God, who gives generously to everyone without holding back.
6 Lakini omba kwa imani, bila shaka, kwa kuwa mwenye kutia shaka ni kama mawimbi katika bahari, huchukuliwa na upepo na kutupwa huku na huko.
But when you ask, remember to trust in God—don't have any doubts. Someone who doubts is like the crashing waves of the sea, tossed about and driven by the wind.
7 Kwa hakika mtu huyu asifikirie kwamba atapokelewa ombi lake kutoka kwa Bwana;
Nobody like that should think they'll get anything from the Lord—
8 mtu huyu ana nia mbili, si imara katika njia zake zote.
their minds think every which way, and they're unstable in whatever they do.
9 Ndugu maskini anapaswa kujivuna katika kusimama kwake juu,
Believers who are born poor should take pride in the high position they've been given,
10 wakati huo huo ndugu tajiri katika unyenyekevu wake, kwa sababu atatoweka kama ua la kondeni katika shamba analopita.
while the rich should “boast” in the humble position they now have, since they will fade away like flowers in the field.
11 Jua huchomoza na joto la kuunguza kukausha mimea, na maua huanguka na uzuri wake hufa. Vivyo hivyo watu matajiri watachakaa katikati ya kazi zao.
For the sun rises along with the blistering wind and scorches the grass. The flowers fall and their beauty is marred. Everything the rich achieve will fade in just the same way.
12 Amebarikiwa mtu yule anayevumilia majaribu, kwa kuwa baada ya kushinda jaribu hilo, atapokea taji ya uzima, ambayo imeahidiwa kwa wale wampendao Mungu.
Happy is anyone who patiently endures temptation, for when they've proved that they are trustworthy, they will receive the crown of life which God promises to those who love him.
13 Mtu yeyote hapaswi kusema anapojaribiwa, “Jaribu hili linatoka kwa Mungu,” kwa sababu Mungu hajaribiwi na uovu, na Mungu mwenyewe hamjaribu yeyote.
Nobody should say when they're tempted, “I'm being tempted by God.” For God is not tempted by evil, nor does he tempt anyone.
14 Kila mtu hujaribiwa na tamaa zake mbaya zinazomshawishi na kumvuta mbali.
Temptations come from our own evil desires that lead us astray and entrap us.
15 Ndipo baada ya tamaa ya dhambi kubeba mimba, dhambi huzaliwa, na baada ya dhambi kukomaa sawasawa, huishia katika mauti.
Such desires lead to sin, and sin, when it's fully developed, causes death.
16 Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike.
My dear friends, don't be deceived.
17 Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika hutoka juu, hushuka chini kutoka kwa Baba wa nuru. Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo.
All that's good, every perfect gift, is from above, and comes down from the Father who made heaven's lights. Unlike them he doesn't change—he doesn't vary or cause shadows.
18 Mungu alichagua kutupa sisi uzima kwa Neno la kweli, ili kwamba tuweze kuwa kama uzao wa kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
He chose to give us new life through the word of truth, so that out of all his creation we would be very special to him.
19 Mnajua hili, ndugu zangu wapendwa. Kila mmoja anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia, siyo mwepesi wa kuongea wala kukasirika,
Remember this, my dear friends: everyone should be quick to listen but slow to speak, and slow to get angry,
20 kwa kuwa hasira ya mwanadamu haiwezi kutenda haki ya Mungu.
because human anger doesn't reflect the good character of God.
21 Kwa hiyo wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote ulio mahali popote, na kwa unyenyekevu lipokeeni neno lililopandwa ndani yenu, ambalo lina uwezo wa kuokoa roho zenu.
So get rid of all that's filthy and evil. Humbly accept the word that's been implanted within you—for this is what can save you.
22 Litiini neno, msilisikie tu, mkijidanganya nafsi zenu wenyewe.
But do what the word says—don't just listen to it and delude yourselves.
23 Kwa kuwa kama yeyote alisikiaye neno bila kulitendea kazi ni sawa na mtu ajiangaliaye uso wake halisi katika kioo.
If you just listen to the word, and don't act on it, it's like staring at your own face in a mirror.
24 Hujitathimini uso wake, na huenda zake na baada ya muda mfupi husahau anavyofanana.
You see yourself, but then you leave, and immediately forget what you looked like.
25 Bali mtu yule anayeiangalia kwa uangalifu sheria kamili, sheria ya uhuru, na kuendelea kuitii, si kwa sababu yeye ni msikilizaji anayesahau, huyu mtu atabarikiwa anapoitenda.
But if you look to the perfect law of freedom and follow it, not as someone who just listens and then forgets, but as someone who acts on it—then you will be blessed in what you do.
26 Ikiwa mtu yeyote atafikiri mwenyewe kuwa ni mtu wa dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, huudanganya moyo wake na dini yake ni bure.
If you think you're religious, but don't control what you say, you deceive yourself—your religion is pointless.
27 Dini iliyo safi na isiyoharibiwa mbele za Mungu wetu na Baba ni hii: kuwasaidia yatima na wajane katika mateso yao, na kujilinda wenyewe na ufisadi wa dunia.
In the eyes of our God and Father, religion that's pure and genuine is to visit orphans and widows in their suffering, and to keep yourself from being contaminated by the world.

< Yakobo 1 >