< Yakobo 3 >

1 Ndugu zangu, siyo wengi wenu mnapaswa kuwa walimu, mkijua kwamba tutapokea hukumu kubwa zaidi.
Kardeşlerim, biz öğretmenlerin daha titiz bir yargılamadan geçeceğini biliyorsunuz; bu nedenle çoğunuz öğretmen olmayın.
2 Kwa kuwa wote tunakosea katika njia nyingi. Kama yeyote huwa hajikwai katika maneno yake, huyo ni mtu mkamilifu, aweza kudhibiti mwili wake wote pia.
Çünkü hepimiz çok hata yaparız. Sözleriyle hata yapmayan kimse, bütün bedenini de dizginleyebilen yetkin bir kişidir.
3 Sasa kama tunaweka lijamu za farasi katika vinywa vyao wanatutii, na tunaweza kuigeuza miili yao yote.
Bize boyun eğmeleri için atların ağzına gem vururuz, böylece bütün bedenlerini yönlendiririz.
4 Tambua pia kwamba meli, ingawa ni kubwa na husukumwa na upepo mkali, zinaongozwa kwa usukani mdogo sana kwenda popote anakotaka nahodha.
Düşünün, gemiler de o kadar büyük olduğu, güçlü rüzgarlar tarafından sürüklendiği halde, dümencinin gönlü nereye isterse küçücük bir dümenle o yöne çevrilirler.
5 Vivyo hivyo, ulimi ni kiungo kidogo cha mwili, lakini hujisifia makuu sana. Angalia msitu mkubwa unavyoweza kuwashwa kwa cheche ndogo ya moto!
Bunun gibi, dil de bedenin küçük bir üyesidir, ama büyük işlerle övünür. Düşünün, küçücük bir kıvılcım koca bir ormanı tutuşturabilir.
6 Ulimi pia ni moto, ni ulimwengu wa uovu, umewekwa miongoni mwa viungo vya mwili wetu, ambao hunajisi mwili wote na huiweka juu ya moto njia ya maisha, na wenyewe kuchomwa moto wa kuzimu. (Geenna g1067)
Dil de bir ateş, bedenimizin üyeleri arasında bir kötülük dünyasıdır. Bütün varlığımızı kirletir. Cehennemden alevlenmiş olarak yaşamımızın gidişini alevlendirir. (Geenna g1067)
7 Kila aina ya mnyama wa polini, ndege, kitambaacho na kiumbe cha baharini kinadhibitiwa na wanadamu.
İnsan soyu, her tür yabanıl hayvanı, kuşu, sürüngeni ve deniz yaratığını evcilleştirmiş ve evcilleştirmektedir.
8 lakini hakuna mwanadamu hata mmoja ambaye anaweza kudhibiti ulimi; ni uovu usiotulia, umejaa sumu ya kufisha.
Ama dili hiçbir insan evcilleştiremez. Dil öldürücü zehirle dolu, dinmeyen bir kötülüktür.
9 Kwa ulimi twamtukuza Bwana na Baba yetu, na kwa huo twawalaani watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
Dilimizle Rab'bi, Baba'yı överiz. Yine dilimizle Tanrı'ya benzer yaratılmış insana söveriz.
10 Katika kinywa hichohicho husema maneno ya baraka na laana. Ndugu zangu mambo haya hayapaswi kuwa.
Övgü ve sövgü aynı ağızdan çıkar. Kardeşlerim, bu böyle olmamalı.
11 Je, kisima kimoja huweza kutoa maji matamu na machungu?
Bir pınar aynı gözden tatlı ve acı su akıtır mı?
12 Ndugu zangu, Je, mti wa mtini unaweza kuzaa matunda ya mzeituni, au mzabibu unazaa matunda ya mtini? Wala chemchemi ya maji chumvi haitoi maji yasio na chumvi.
Kardeşlerim, incir ağacı zeytin ya da asma incir verebilir mi? Bunun gibi, tuzlu su kaynağı tatlı su veremez.
13 Ni nani miongoni mwenu aliye na hekima na ufahamu? Hebu mtu huyo na aoneshe maisha mema katika kazi zake kwa unyenyekevu utokanao na hekima.
Aranızda bilge ve anlayışlı olan kim? Olumlu yaşayışıyla, bilgelikten doğan alçakgönüllülükle iyi eylemlerini göstersin.
14 Lakini kama mnao wivu mkali na nia ya ubinafsi mioyoni mwenu, msijivune na kusema uongo mkiupinga ukweli.
Ama yüreğinizde kin, kıskançlık, bencillik varsa övünmeyin, gerçeği yadsımayın.
15 Hii siyo hekima ile ishukayo kutoka juu, lakini badala yake ni ya kidunia, si ya kiroho, na ni ya kipepo.
Böylesi “bilgelik” gökten inen değil, dünyadan, insan doğasından, cinlerden gelen bilgeliktir.
16 Kwa kuwa palipo na wivu na ubinafsi upo, kuna vurugu na kila matendo maovu
Çünkü nerede kıskançlık, bencillik varsa, orada karışıklık ve her tür kötülük vardır.
17 Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, kisha kupenda amani, upole na ukarimu, yenye kujaa rehema na matunda mema, bila kupendelea watu fulani, na kweli.
Ama gökten inen bilgelik her şeyden önce paktır, sonra barışçıldır, yumuşaktır, uysaldır. Merhamet ve iyi meyvelerle doludur. Kayırıcılığı, ikiyüzlülüğü yoktur.
18 Na tunda la haki hupandwa katika amani kwa wale ambao wanatenda mambo ya amani.
Barış içinde eken barış yapıcıları doğruluk ürününü biçerler.

< Yakobo 3 >