< Yakobo 3 >
1 Ndugu zangu, siyo wengi wenu mnapaswa kuwa walimu, mkijua kwamba tutapokea hukumu kubwa zaidi.
hE mama bhrAtaraH, zikSakairasmAbhi rgurutaradaNPO lapsyata iti jnjAtvA yUyam anEkE zikSakA mA bhavata|
2 Kwa kuwa wote tunakosea katika njia nyingi. Kama yeyote huwa hajikwai katika maneno yake, huyo ni mtu mkamilifu, aweza kudhibiti mwili wake wote pia.
yataH sarvvE vayaM bahuviSayESu skhalAmaH, yaH kazcid vAkyE na skhalati sa siddhapuruSaH kRtsnaM vazIkarttuM samarthazcAsti|
3 Sasa kama tunaweka lijamu za farasi katika vinywa vyao wanatutii, na tunaweza kuigeuza miili yao yote.
pazyata vayam azvAn vazIkarttuM tESAM vaktrESu khalInAn nidhAya tESAM kRtsnaM zarIram anuvarttayAmaH|
4 Tambua pia kwamba meli, ingawa ni kubwa na husukumwa na upepo mkali, zinaongozwa kwa usukani mdogo sana kwenda popote anakotaka nahodha.
pazyata yE pOtA atIva bRhadAkArAH pracaNPavAtaizca cAlitAstE'pi karNadhArasya manO'bhimatAd atikSudrENa karNEna vAnjchitaM sthAnaM pratyanuvarttantE|
5 Vivyo hivyo, ulimi ni kiungo kidogo cha mwili, lakini hujisifia makuu sana. Angalia msitu mkubwa unavyoweza kuwashwa kwa cheche ndogo ya moto!
tadvad rasanApi kSudratarAggaM santI darpavAkyAni bhASatE| pazya kIdRgmahAraNyaM dahyatE 'lpEna vahninA|
6 Ulimi pia ni moto, ni ulimwengu wa uovu, umewekwa miongoni mwa viungo vya mwili wetu, ambao hunajisi mwili wote na huiweka juu ya moto njia ya maisha, na wenyewe kuchomwa moto wa kuzimu. (Geenna )
rasanApi bhavEd vahniradharmmarUpapiSTapE| asmadaggESu rasanA tAdRzaM santiSThati sA kRtsnaM dEhaM kalagkayati sRSTirathasya cakraM prajvalayati narakAnalEna jvalati ca| (Geenna )
7 Kila aina ya mnyama wa polini, ndege, kitambaacho na kiumbe cha baharini kinadhibitiwa na wanadamu.
pazupakSyurOgajalacarANAM sarvvESAM svabhAvO damayituM zakyatE mAnuSikasvabhAvEna damayAnjcakrE ca|
8 lakini hakuna mwanadamu hata mmoja ambaye anaweza kudhibiti ulimi; ni uovu usiotulia, umejaa sumu ya kufisha.
kintu mAnavAnAM kEnApi jihvA damayituM na zakyatE sA na nivAryyam aniSTaM halAhalaviSENa pUrNA ca|
9 Kwa ulimi twamtukuza Bwana na Baba yetu, na kwa huo twawalaani watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
tayA vayaM pitaram IzvaraM dhanyaM vadAmaH, tayA cEzvarasya sAdRzyE sRSTAn mAnavAn zapAmaH|
10 Katika kinywa hichohicho husema maneno ya baraka na laana. Ndugu zangu mambo haya hayapaswi kuwa.
EkasmAd vadanAd dhanyavAdazApau nirgacchataH| hE mama bhrAtaraH, EtAdRzaM na karttavyaM|
11 Je, kisima kimoja huweza kutoa maji matamu na machungu?
prasravaNaH kim EkasmAt chidrAt miSTaM tiktanjca tOyaM nirgamayati?
12 Ndugu zangu, Je, mti wa mtini unaweza kuzaa matunda ya mzeituni, au mzabibu unazaa matunda ya mtini? Wala chemchemi ya maji chumvi haitoi maji yasio na chumvi.
hE mama bhrAtaraH, uPumbarataruH kiM jitaphalAni drAkSAlatA vA kim uPumbaraphalAni phalituM zaknOti? tadvad EkaH prasravaNO lavaNamiSTE tOyE nirgamayituM na zaknOti|
13 Ni nani miongoni mwenu aliye na hekima na ufahamu? Hebu mtu huyo na aoneshe maisha mema katika kazi zake kwa unyenyekevu utokanao na hekima.
yuSmAkaM madhyE jnjAnI subOdhazca ka AstE? tasya karmmANi jnjAnamUlakamRdutAyuktAnIti sadAcArAt sa pramANayatu|
14 Lakini kama mnao wivu mkali na nia ya ubinafsi mioyoni mwenu, msijivune na kusema uongo mkiupinga ukweli.
kintu yuSmadantaHkaraNamadhyE yadi tiktErSyA vivAdEcchA ca vidyatE tarhi satyamatasya viruddhaM na zlAghadhvaM nacAnRtaM kathayata|
15 Hii siyo hekima ile ishukayo kutoka juu, lakini badala yake ni ya kidunia, si ya kiroho, na ni ya kipepo.
tAdRzaM jnjAnam UrddhvAd AgataM nahi kintu pArthivaM zarIri bhautikanjca|
16 Kwa kuwa palipo na wivu na ubinafsi upo, kuna vurugu na kila matendo maovu
yatO hEtOrIrSyA vivAdEcchA ca yatra vEdyEtE tatraiva kalahaH sarvvaM duSkRtanjca vidyatE|
17 Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, kisha kupenda amani, upole na ukarimu, yenye kujaa rehema na matunda mema, bila kupendelea watu fulani, na kweli.
kintUrddhvAd AgataM yat jnjAnaM tat prathamaM zuci tataH paraM zAntaM kSAntam AzusandhEyaM dayAdisatphalaiH paripUrNam asandigdhaM niSkapaTanjca bhavati|
18 Na tunda la haki hupandwa katika amani kwa wale ambao wanatenda mambo ya amani.
zAntyAcAribhiH zAntyA dharmmaphalaM rOpyatE|