< Yakobo 2 >

1 Ndugu zangu msiifuate imani ya Bwana Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, kwa kupendelea watu fulani.
Mes frères, que votre foi en Jésus-Christ, notre glorieux Seigneur, soit exempte de toute acception de personnes.
2 Kama mtu fulani akiingia kwenye mikutano yenu amevaa pete za dhahabu na mavazi mazuri, pia akaingia masikini mwenye mavazi machafu,
Supposez qu'il entre dans votre assemblée un homme portant un anneau d'or et des habits magnifiques, et qu'il y entre aussi un pauvre misérablement vêtu.
3 na mkaonyesha kumjali zaidi yule mwenye mavazi mazuri na kusema, “Tafadhari wewe keti hapa mahali pazuri” lakini mkamwambia yule masikini, “Wewe simama pale,” au “Kaa chini ya miguu yangu.”
Si, tournant vos regards vers celui qui porte les habits magnifiques, vous lui dites: Toi, assieds-toi ici, à cette bonne place; et que vous disiez au pauvre: Toi, tiens-toi là debout, ou assieds-toi au-dessous de mon marchepied, —
4 Je, hamuhukumiani ninyi wenyewe, na kuwa waamuzi wenye mawazo mabaya?
n'établissez-vous pas en vous-mêmes des distinctions, et vos jugements ne sont-ils pas inspirés par de mauvaises pensées?
5 Sikilizeni, ndugu zangu wapendwa, je, Mungu hakuwachagua masikini wa dunia kuwa matajiri katika imani na kurithi ufalme aliowaahidia wampendao?
Écoutez, mes frères bien-aimés: Dieu n'a-t-il pas choisi les pauvres selon le monde pour les rendre riches en la foi et héritiers du royaume qu'il a promis à ceux qui l'aiment?
6 Lakini mmewadharau masikini! Je, sio matajiri wanaowatesa ninyi, na sio wao wanaowaburuta mahakamani?
Et vous, vous avez méprisé le pauvre, alors que ce sont les riches qui vous oppriment et qui vous traînent devant les tribunaux;
7 Je, si matajiri wanaolitukana jina lile zuri ambalo kwalo mnaitiwa?
et ce sont eux aussi qui blasphèment le beau nom qui a été invoqué sur vous!
8 Hata hivyo, kama mwaitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa katika maandiko, “Utampenda jirani yako kama wewe mwenyewe,” mwafanya vyema.
Sans doute, si vous accomplissez la loi royale, selon l'Écriture: «Tu aimeras ton prochain comme toi-même»— vous agissez bien.
9 Lakini kama mkipendelea baadhi ya watu, mnatenda dhambi, mwahukumiwa na sheria kuwa ni wavunja sheria.
Mais si vous faites acception de personnes, vous commettez un péché, et la loi vous condamne comme transgresseurs.
10 Kwa kuwa yeyote atiiye sheria yote, na bado akajikwaa katika nukta moja tu, amekuwa na hatia ya kuvunja sheria yote!
Car celui qui observe la loi tout entière, mais qui en viole un seul commandement, est coupable comme s'il les avait tous violés.
11 Kwa kuwa Mungu aliyesema, “Usizini,” ndiye pia aliyesema, “Usiue.” Kama hauzini, lakini una uwa, umekwishavunja sheria ya Mungu.
En effet, celui qui a dit: «Tu ne commettras point d'adultère» a dit aussi: «Tu ne tueras point.» Si donc tu ne commets pas d'adultère, mais que tu commettes un meurtre, tu es transgresseur de la loi.
12 Kwa hiyo zungumzeni na kutii kama wale ambao mko karibu kuhukumiwa na sheria ya uhuru.
Parlez et agissez comme devant être jugés par une loi de liberté.
13 Kwa kuwa hukumu huja pasipo huruma kwa wale wasio na huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.
Le jugement est sans miséricorde pour celui qui n'a pas fait miséricorde; mais la miséricorde triomphe du jugement.
14 Kuna uzuri gani, ndugu zangu, kama mtu anasema ninayo imani, lakini hana matendo? Je, imani hiyo yaweza kumwokoa?
Mes frères, que sert-il à un homme de dire qu'il a la foi, s'il n'a pas les oeuvres? Cette foi peut-elle le sauver?
15 Kama ndugu wa kiume au wa kike ni muhitaji wa mavazi au chakula cha kila siku,
Si un frère ou une soeur sont dans le dénuement, s'ils manquent de la nourriture de chaque jour,
16 na mmoja wenu akawaambia, “Nendeni kwa amani, mkaote moto na mle vizuri,” lakini hamuwapi mahitaji muhimu ya mwili, hiyo yafaaa nini?
et que l'un de nous leur dise: Allez en paix, chauffez-vous, rassasiez-vous. — et cela, sans leur donner ce qui est nécessaire pour la vie du corps, — à quoi cela sert-il?
17 Hali kadhalika, imani pekee, kama haina matendo, imekufa.
Il en est de même de la foi: si elle ne produit pas d'oeuvres, elle est morte en elle-même.
18 Bado mtu fulani anaweza kusema, “Una imani, na mimi ninayo matendo.” Nionyeshe imani yako pasipo matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.
Ou bien encore, quelqu'un dira; Tu as la foi, et moi, j'ai les oeuvres. Montre-moi ta foi sans les oeuvres, et moi, je te montrerai ma foi par mes oeuvres.
19 Waamini kuwa kuna Mungu mmoja; uko sahihi. Lakini mapepo nayo yanaamini hivyo na kutetemeka.
Tu crois qu'il y a un seul Dieu, tu fais bien; les démons le croient aussi, et ils tremblent!
20 Je, unataka kujua, ewe mtu mpumbavu, namna ambavyo imani hiyo pasipo matendo isivyofaa?
Mais veux-tu te convaincre, ô homme vain, que la foi sans les oeuvres est inutile?
21 Je, si baba yetu Abrahamu alihesabiwa haki kwa matendo alipomtoa mwanawe Isaka juu ya madhabahu?
Abraham, notre père, ne fut-il pas justifié par les oeuvres, lorsqu'il lui offrit sur l'autel son fils Isaac?
22 Mnaona kuwa imani yake ilifanya kazi na matendo yake, na kwa matendo yake, imani yake ilifikia kusudio lake.
Tu vois que la foi agissait avec ses oeuvres, et que par ses oeuvres sa foi fut rendue parfaite.
23 Maandiko yalitimizwa yasemayo, “Abrahamu alimwamini Mungu, na akahesabiwa kuwa ni mwenye haki.” Hivyo Abrahamu aliitwa rafiki wa Mungu.
Ainsi s'accomplit ce que dit l'Écriture: «Abraham crut à Dieu, et cela lui fut imputé à justice»; et il fut appelé ami de Dieu.
24 Mwaona kuwa kwa matendo mtu huhesabiwa haki, na si kwa imani tu.
Vous voyez que l'homme est justifié par les oeuvres, et non par la foi seulement.
25 Hali kadhalika, je, hakuwa Rahabu yule kahaba alihesabiwa haki kwa matendo, alipowakaribisha wajumbe na kuwapeleka kwa barabara nyingine?
De même aussi, Rahab, la femme de mauvaise vie, ne fut-elle pas justifiée par les oeuvres, pour avoir reçu les messagers et les avoir fait partir par un autre chemin?
26 Kwa kuwa kama vile mwili usipokuwa na roho umekufa, vivyo hivyo imani pasipo matendo imekufa.
En effet, comme le corps sans âme est mort, ainsi la foi sans les oeuvres est morte.

< Yakobo 2 >