< Yakobo 1 >
1 Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, kwa makabila kumi na mbili yaliyotawanyika, salaam.
Jacobus, Guds och Herrans Jesu Christi tjenare: dem tolf slägtom, som äro här och der förskingrade, helso.
2 Hesabuni kuwa ni furaha zaidi, ndugu zangu, mnapopita katika matatizo mbali mbali,
Mine bröder, håller det för all glädje, när I fallen i mångahanda frestelse;
3 mkijua kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huwapa uvumilivu.
Och veter, att edor tros bepröfvelse gör tålamod.
4 Acheni uvumilivu uikamilishe kazi yake, kwamba muweze kukomaa kikamilifu, bila kupungukiwa katika lolote.
Men låter tålamodet hafva ett fullbordadt verk; på det I skolen vara fullkomna och hele, och intet fel hafva.
5 Lakini kama mtu kati yenu anahitaji hekima, aiombe kutoka kwa Mungu, ambaye hutoa kwa ukarimu na pasipo kukemea kwa wote wamwombao, na atawapa hekima.
Hvar nu någrom ibland eder fattas visdom, han bedje af Gudi, den der gifver enfaldeliga allom, och förviter icke; och han skall honom gifven varda.
6 Lakini omba kwa imani, bila shaka, kwa kuwa mwenye kutia shaka ni kama mawimbi katika bahari, huchukuliwa na upepo na kutupwa huku na huko.
Men han bedje i trone, intet tviflandes; ty den der tviflar, han är såsom hafsens våg, som af vädret drifs och föres.
7 Kwa hakika mtu huyu asifikirie kwamba atapokelewa ombi lake kutoka kwa Bwana;
Sådana menniska tänke icke, att hon får något af Herranom.
8 mtu huyu ana nia mbili, si imara katika njia zake zote.
En man, som tviflar, är ostadig i alla sina vägar.
9 Ndugu maskini anapaswa kujivuna katika kusimama kwake juu,
Men en broder, som ringa är, berömme sig af sin upphöjelse;
10 wakati huo huo ndugu tajiri katika unyenyekevu wake, kwa sababu atatoweka kama ua la kondeni katika shamba analopita.
Och den som rik är, af sin förnedring; ty såsom blomstret af gräset skall han förgås.
11 Jua huchomoza na joto la kuunguza kukausha mimea, na maua huanguka na uzuri wake hufa. Vivyo hivyo watu matajiri watachakaa katikati ya kazi zao.
Solen går upp med hetta, och gräset förvissnar, och blomstret faller af, och dess sköna fägring förgås; så skall ock den rike förvissna uti sina vägar.
12 Amebarikiwa mtu yule anayevumilia majaribu, kwa kuwa baada ya kushinda jaribu hilo, atapokea taji ya uzima, ambayo imeahidiwa kwa wale wampendao Mungu.
Salig är den man, som tåleliga lider frestelse; ty då han bepröfvad är, skall han ta lifsens krono, den Gud lofvat hafver dem som honom älska.
13 Mtu yeyote hapaswi kusema anapojaribiwa, “Jaribu hili linatoka kwa Mungu,” kwa sababu Mungu hajaribiwi na uovu, na Mungu mwenyewe hamjaribu yeyote.
Ingen säge, då han frestad varder, att han af Gudi frestad varder; ty Gud frestas icke af ondt, han frestar ock ingen;
14 Kila mtu hujaribiwa na tamaa zake mbaya zinazomshawishi na kumvuta mbali.
Utan hvar och en varder frestad, då han af sin egen begärelse dragen och lockad varder.
15 Ndipo baada ya tamaa ya dhambi kubeba mimba, dhambi huzaliwa, na baada ya dhambi kukomaa sawasawa, huishia katika mauti.
Derefter, sedan begärelsen hafver aflat, föder hon synden; men då synden är fullbordad, föder hon döden.
16 Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike.
Farer icke ville, mine käre bröder.
17 Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika hutoka juu, hushuka chini kutoka kwa Baba wa nuru. Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo.
All god gåfva, och all fullkomlig gåfva kommer ofvanefter, ifrå ljusens Fader; när hvilkom ingen förvandling är, eller ljus och mörkers omskiftelse.
18 Mungu alichagua kutupa sisi uzima kwa Neno la kweli, ili kwamba tuweze kuwa kama uzao wa kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
Han hafver oss födt efter sin vilja, genom sanningenes ord, på det vi skulle vara förstlingen af hans kreatur.
19 Mnajua hili, ndugu zangu wapendwa. Kila mmoja anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia, siyo mwepesi wa kuongea wala kukasirika,
Derföre, mine käre bröder, hvar och en menniska vare snar till att höra, och sen till att tala, och sen till vrede.
20 kwa kuwa hasira ya mwanadamu haiwezi kutenda haki ya Mungu.
Ty mansens vrede gör icke det rätt är för Gudi.
21 Kwa hiyo wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote ulio mahali popote, na kwa unyenyekevu lipokeeni neno lililopandwa ndani yenu, ambalo lina uwezo wa kuokoa roho zenu.
Lägger fördenskull bort alla orenlighet och alla ondsko, och anammer ordet med saktmodighet, som i eder plantadt är, det edra själar kan saliga göra.
22 Litiini neno, msilisikie tu, mkijidanganya nafsi zenu wenyewe.
Men varer ordets görare, och icke allenast hörare, bedragandes eder sjelfva.
23 Kwa kuwa kama yeyote alisikiaye neno bila kulitendea kazi ni sawa na mtu ajiangaliaye uso wake halisi katika kioo.
Ty der någor är allenast ordsens hörare, och icke görare, han är lik den man, som sitt lekamliga ansigte skådar i en spegel;
24 Hujitathimini uso wake, na huenda zake na baada ya muda mfupi husahau anavyofanana.
Ty då han sig beskådat hafver, går han derifrån, och förgäter straxt hurudana han var.
25 Bali mtu yule anayeiangalia kwa uangalifu sheria kamili, sheria ya uhuru, na kuendelea kuitii, si kwa sababu yeye ni msikilizaji anayesahau, huyu mtu atabarikiwa anapoitenda.
Men den der skådar uti frihetenes fullkomliga lag, och blifver deruti, och är icke en glömsker hörare, utan en görare, den samme varder salig uti sin gerning.
26 Ikiwa mtu yeyote atafikiri mwenyewe kuwa ni mtu wa dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, huudanganya moyo wake na dini yake ni bure.
Hvar nu någor ibland eder låter sig tycka, att han tjenar Gudi, och icke styrer sina tungo, utan bedrager sitt hjerta, hans Gudstjenst är fåfäng.
27 Dini iliyo safi na isiyoharibiwa mbele za Mungu wetu na Baba ni hii: kuwasaidia yatima na wajane katika mateso yao, na kujilinda wenyewe na ufisadi wa dunia.
Detta är för Gudi och Fadren en ren och obesmittad Gudstjenst, söka faderlös och moderlös barn, och enkor, uti deras bedröfvelse, och behålla sig obesmittad af verldene.