< Yakobo 1 >

1 Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, kwa makabila kumi na mbili yaliyotawanyika, salaam.
Jakob Boga in Gospoda Jezusa Kristusa hlapec, dvanajsterim rodom v raztrosu: zdravi!
2 Hesabuni kuwa ni furaha zaidi, ndugu zangu, mnapopita katika matatizo mbali mbali,
Za vso radost vam bodi, bratje moji, ako ste padli v mnogotere izkušnjave,
3 mkijua kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huwapa uvumilivu.
Spoznavajoč, da izkušnja vere vaše nareja stanovitnost;
4 Acheni uvumilivu uikamilishe kazi yake, kwamba muweze kukomaa kikamilifu, bila kupungukiwa katika lolote.
Stanovitnost pa imej delo popolno, da bodete popolni in dovršeni, v ničemur pogrešni.
5 Lakini kama mtu kati yenu anahitaji hekima, aiombe kutoka kwa Mungu, ambaye hutoa kwa ukarimu na pasipo kukemea kwa wote wamwombao, na atawapa hekima.
Če pa ima kdo izmed vas premalo modrosti, prosi je naj od Boga, kateri vsem daje obilo, in nikomur ne oponaša; in dala se mu bode.
6 Lakini omba kwa imani, bila shaka, kwa kuwa mwenye kutia shaka ni kama mawimbi katika bahari, huchukuliwa na upepo na kutupwa huku na huko.
Prosi pa naj v veri, brez dvomljenja; kdor namreč dvomi, podoben je valu morskemu, ki ga veter goni in premetava.
7 Kwa hakika mtu huyu asifikirie kwamba atapokelewa ombi lake kutoka kwa Bwana;
Naj namreč ne misli tisti človek, da bode kaj dobil od Gospoda;
8 mtu huyu ana nia mbili, si imara katika njia zake zote.
Mož omahljiv je nestanoviten na vseh potih svojih.
9 Ndugu maskini anapaswa kujivuna katika kusimama kwake juu,
Ponaša pa naj se brat nizki v visokosti svoji;
10 wakati huo huo ndugu tajiri katika unyenyekevu wake, kwa sababu atatoweka kama ua la kondeni katika shamba analopita.
Bogati pa v ponižnosti svoji, kajti minil bode kakor trave cvet.
11 Jua huchomoza na joto la kuunguza kukausha mimea, na maua huanguka na uzuri wake hufa. Vivyo hivyo watu matajiri watachakaa katikati ya kazi zao.
Kajti vzšlo je solnce z vročino in posušilo je travo, in cvet njen je odpadel, in lepota lica njenega je izginila. Tako bode tudi bogatin zvenil na potih svojih.
12 Amebarikiwa mtu yule anayevumilia majaribu, kwa kuwa baada ya kushinda jaribu hilo, atapokea taji ya uzima, ambayo imeahidiwa kwa wale wampendao Mungu.
Blagor možu, kateri prebije izkušnjavo; ker izkušen zadobode venec življenja, katerega je obljubil Gospod njim, ki ga ljubijo.
13 Mtu yeyote hapaswi kusema anapojaribiwa, “Jaribu hili linatoka kwa Mungu,” kwa sababu Mungu hajaribiwi na uovu, na Mungu mwenyewe hamjaribu yeyote.
Nihče naj, izkušan, ne reče: Od Boga sem izkušan; kajti Bog je neizkušljiv v hudo, in sam ne izkuša nikogar.
14 Kila mtu hujaribiwa na tamaa zake mbaya zinazomshawishi na kumvuta mbali.
Sleherni pa je izkušan, kogar lastna sla vleče in vabi;
15 Ndipo baada ya tamaa ya dhambi kubeba mimba, dhambi huzaliwa, na baada ya dhambi kukomaa sawasawa, huishia katika mauti.
Potem ko je sla izpočela, rodi pregreho, pregreha pa, ko je dovršena, rodí smrt.
16 Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike.
Ne tavajte, bratje moji ljubljeni;
17 Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika hutoka juu, hushuka chini kutoka kwa Baba wa nuru. Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo.
Vsak dober dar in vsako darilo popolno prihaja dol od očeta luči, pri katerem ni izpremembe ali osenčanja obrnitve.
18 Mungu alichagua kutupa sisi uzima kwa Neno la kweli, ili kwamba tuweze kuwa kama uzao wa kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
Po volji svoji nas je rodil po besedi resnice, da bodimo neka prvina stvarî njegovih.
19 Mnajua hili, ndugu zangu wapendwa. Kila mmoja anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia, siyo mwepesi wa kuongea wala kukasirika,
Zatorej, bratje moji ljubljeni, bodi vsak človek nagel v poslušanje, počasen v govorjenje, počasen v jezo;
20 kwa kuwa hasira ya mwanadamu haiwezi kutenda haki ya Mungu.
Kajti jeza človekova ne dela pravice Božje.
21 Kwa hiyo wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote ulio mahali popote, na kwa unyenyekevu lipokeeni neno lililopandwa ndani yenu, ambalo lina uwezo wa kuokoa roho zenu.
Zato odloživši sleherno nesnago in obilost hudobije sprejmite v krotkosti vsajeno besedo, ki more rešiti duše vaše.
22 Litiini neno, msilisikie tu, mkijidanganya nafsi zenu wenyewe.
Bodite pa delalci besede in ne samo poslušalci, ki se sami slepé.
23 Kwa kuwa kama yeyote alisikiaye neno bila kulitendea kazi ni sawa na mtu ajiangaliaye uso wake halisi katika kioo.
Ker če je kdo poslušalec besede, ne pa delalec, on je podoben možu, ki ogleduje v ogledalu rojstva svojega obličje;
24 Hujitathimini uso wake, na huenda zake na baada ya muda mfupi husahau anavyofanana.
Pogledal se je namreč in odšel, in hitro je pozabil, kakošen je bil.
25 Bali mtu yule anayeiangalia kwa uangalifu sheria kamili, sheria ya uhuru, na kuendelea kuitii, si kwa sababu yeye ni msikilizaji anayesahau, huyu mtu atabarikiwa anapoitenda.
Kdor pa je pogledal v popolno postavo svobode in v njej ostal on, ki ni postal pozabljiv poslušalec nego delalec dela, on bode srečen v dejanji svojem.
26 Ikiwa mtu yeyote atafikiri mwenyewe kuwa ni mtu wa dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, huudanganya moyo wake na dini yake ni bure.
Če meni kdo med vami, da je bogaboječ, pa ne brzda jezika svojega, nego vara svoje srce, njegova bogaboječnost je ničeva.
27 Dini iliyo safi na isiyoharibiwa mbele za Mungu wetu na Baba ni hii: kuwasaidia yatima na wajane katika mateso yao, na kujilinda wenyewe na ufisadi wa dunia.
Bogaboječnost čista in neoskrunjena pred Bogom in očetom je ta, skrbeti za sirote in vdove v njih stiski, neomadeževanega se braniti od sveta.

< Yakobo 1 >