< Yakobo 1 >
1 Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, kwa makabila kumi na mbili yaliyotawanyika, salaam.
Jacques, serviteur de Dieu et du Seigneur Jésus-Christ, aux douze tribus qui sont dispersées, salut!
2 Hesabuni kuwa ni furaha zaidi, ndugu zangu, mnapopita katika matatizo mbali mbali,
Mes frères, considérez comme le sujet d'une parfaite joie les épreuves diverses qui vous surviennent,
3 mkijua kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huwapa uvumilivu.
sachant que l'épreuve, à laquelle est soumise votre foi, produit la patience.
4 Acheni uvumilivu uikamilishe kazi yake, kwamba muweze kukomaa kikamilifu, bila kupungukiwa katika lolote.
Mais il faut que la patience ait accompli parfaitement son oeuvre, pour que vous soyez vous-mêmes parfaits et accomplis, et qu'il ne vous manque rien.
5 Lakini kama mtu kati yenu anahitaji hekima, aiombe kutoka kwa Mungu, ambaye hutoa kwa ukarimu na pasipo kukemea kwa wote wamwombao, na atawapa hekima.
Si l'un de vous manque de sagesse, qu'il la demande à Dieu, qui donne à tous libéralement, sans rien reprocher; et elle lui sera donnée.
6 Lakini omba kwa imani, bila shaka, kwa kuwa mwenye kutia shaka ni kama mawimbi katika bahari, huchukuliwa na upepo na kutupwa huku na huko.
Mais qu'il demande avec foi, sans douter; car celui qui doute est semblable au flot de la mer, qui est agité et poussé ça et là par le vent.
7 Kwa hakika mtu huyu asifikirie kwamba atapokelewa ombi lake kutoka kwa Bwana;
Que cet homme-là ne s'attende point à recevoir quelque chose de la part du Seigneur:
8 mtu huyu ana nia mbili, si imara katika njia zake zote.
c'est un homme au coeur partagé, inconstant dans toute sa conduite.
9 Ndugu maskini anapaswa kujivuna katika kusimama kwake juu,
Que le frère qui est de condition humble se glorifie de son élévation,
10 wakati huo huo ndugu tajiri katika unyenyekevu wake, kwa sababu atatoweka kama ua la kondeni katika shamba analopita.
et que le riche se glorifie de son humiliation, car il passera comme la fleur de l'herbe.
11 Jua huchomoza na joto la kuunguza kukausha mimea, na maua huanguka na uzuri wake hufa. Vivyo hivyo watu matajiri watachakaa katikati ya kazi zao.
Le soleil s'est levé avec sa brûlante chaleur; l'herbe a séché, sa fleur est tombée, et l'éclat de sa beauté a péri: ainsi se flétrira le riche, au milieu même de ses entreprises.
12 Amebarikiwa mtu yule anayevumilia majaribu, kwa kuwa baada ya kushinda jaribu hilo, atapokea taji ya uzima, ambayo imeahidiwa kwa wale wampendao Mungu.
Heureux l'homme qui endure la tentation; car, après qu'il aura été mis à l'épreuve, il recevra la couronne de vie que Dieu a promise à ceux qui l'aiment.
13 Mtu yeyote hapaswi kusema anapojaribiwa, “Jaribu hili linatoka kwa Mungu,” kwa sababu Mungu hajaribiwi na uovu, na Mungu mwenyewe hamjaribu yeyote.
Que personne, lorsqu'il est tenté, ne dise: C'est Dieu qui me tente; car Dieu ne peut être tenté par aucun mal, et lui-même ne tente personne.
14 Kila mtu hujaribiwa na tamaa zake mbaya zinazomshawishi na kumvuta mbali.
Mais chacun est tenté, quand il est attiré et amorcé par sa propre convoitise.
15 Ndipo baada ya tamaa ya dhambi kubeba mimba, dhambi huzaliwa, na baada ya dhambi kukomaa sawasawa, huishia katika mauti.
Puis la convoitise, ayant conçu, donne naissance au péché; et le péché, lorsqu'il est consommé, enfante la mort.
16 Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike.
Mes frères bien-aimés, ne vous y trompez pas:
17 Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika hutoka juu, hushuka chini kutoka kwa Baba wa nuru. Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo.
toute grâce excellente et tout don parfait viennent d'en haut et descendent du Père des lumières, en qui il n'y a aucune variation ni aucune ombre de changement.
18 Mungu alichagua kutupa sisi uzima kwa Neno la kweli, ili kwamba tuweze kuwa kama uzao wa kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
C'est lui qui, de sa libre volonté, nous a engendrés par la parole de vérité, afin que nous soyons comme les prémices de ses créatures.
19 Mnajua hili, ndugu zangu wapendwa. Kila mmoja anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia, siyo mwepesi wa kuongea wala kukasirika,
Vous le savez, mes frères bien-aimés, il faut que tout homme soit prompt à écouter, lent à parler, lent à se mettre en colère;
20 kwa kuwa hasira ya mwanadamu haiwezi kutenda haki ya Mungu.
car la colère de l'homme n'accomplit pas la justice de Dieu.
21 Kwa hiyo wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote ulio mahali popote, na kwa unyenyekevu lipokeeni neno lililopandwa ndani yenu, ambalo lina uwezo wa kuokoa roho zenu.
Rejetez donc toute souillure et tout reste de méchanceté, et recevez avec douceur la parole qui a été plantée en vous, et qui peut sauver vos âmes.
22 Litiini neno, msilisikie tu, mkijidanganya nafsi zenu wenyewe.
Mettez en pratique la parole, et ne vous contentez pas de l'écouter, en vous abusant vous-mêmes par de faux raisonnements.
23 Kwa kuwa kama yeyote alisikiaye neno bila kulitendea kazi ni sawa na mtu ajiangaliaye uso wake halisi katika kioo.
En effet, si quelqu'un écoute la parole et ne la met pas en pratique, il est semblable à un homme qui regarde dans un miroir son visage naturel,
24 Hujitathimini uso wake, na huenda zake na baada ya muda mfupi husahau anavyofanana.
et qui, après s'être regardé, s'en va et oublie aussitôt comment il est.
25 Bali mtu yule anayeiangalia kwa uangalifu sheria kamili, sheria ya uhuru, na kuendelea kuitii, si kwa sababu yeye ni msikilizaji anayesahau, huyu mtu atabarikiwa anapoitenda.
Mais celui qui aura plongé ses regards dans la loi parfaite, la loi de la liberté, et qui l'aura contemplée avec persévérance, n'étant pas un auditeur oublieux, mais un fidèle observateur de ses préceptes, celui-là trouvera son bonheur dans son obéissance.
26 Ikiwa mtu yeyote atafikiri mwenyewe kuwa ni mtu wa dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, huudanganya moyo wake na dini yake ni bure.
Si un homme, qui se croit religieux, ne tient pas sa langue en bride et se trompe ainsi lui-même, la religion d'un tel homme est vaine.
27 Dini iliyo safi na isiyoharibiwa mbele za Mungu wetu na Baba ni hii: kuwasaidia yatima na wajane katika mateso yao, na kujilinda wenyewe na ufisadi wa dunia.
La religion pure et sans tache devant Dieu, notre Père, consiste à visiter les orphelins et les veuves dans leurs afflictions, et à se préserver des souillures du monde.