< Isaya 7 >

1 Siku zile wakati Ahazi mtoto wa Yothani mtoto wa Uzia, mfalme wa Yuda, Rezeni mfalme wa Amramu, na Peka mtoto wa Remaelia, mfalme wa Israeli, walienda Yerusalemu kupigana vita nao, lakini hawakuweza kushinda vita.
In the time of Ahaz, the son of Jotham, the son of Uzziah, king of Judah, Rezin, king of Syria, and Pekah, the son of Remaliah, king of Israel, came up against Jerusalem to besiege it; but he could not prevail against it.
2 Ilitaarifiwa kwa nyumba ya Daudi kwamba Amramu amejiunga na Efraimu. Moyo wake na moyo watu wake ukatetemeka, kama vile miti ya misitu inavyopepea kwa upepo.
And when it was told the house of David, that the Syrians had encamped in Ephraim, his heart was moved, and the hearts of his people, as the trees of the forest are moved with the wind.
3 Ndipo Yahwe akamwambia Isaya, ''Nenda nje na kijana wako, Sheari Jashubu ukaonane na Ahazi mwisho wa mfereji wa birika la juu, katika njia kuu ya uwanja Dobi.
Then said Jehovah to Isaiah, Go forth to meet Ahaz, thou and Shear-Jashub thy son, at the end of the aqueduct of the upper pool, in the way to the fuller's field;
4 Mwambie, 'awe makini, awe mtulivu, asiogope au vitisho kwa sababu ya mikia hii miwili ya vingi hivi vitokavyo moshi, kwa sababu ya hasira kubwa ya Resini na Amramu, na mtoto wa Remalia.
and say to him: Take heed, and be quiet! Fear not, neither let thy heart he faint On account of the two tails of these smoking firebrands, On account of the fierce wrath of Rezin with the Syrians, and of the son of Remaliah,
5 Amramu, Ephraimu, na mtoto wa Remaeli wamepanga mabaya juu yako; wamesema, '' njooni tuwavamie Yuda na kuwaogopesha,
Because Syria deviseth evil against thee, Ephraim and the son of Remaliah, saying,
6 njooni tujipange na tumueweke mfalme wetu ndani ya Yuda, mtoto wa Tabaeli.''
“Let us go up against Judah, and besiege the city, And take it, And set a king in the midst of it, Even the son of Tabeal.”
7 Bwana Yahwe asema, ''haitatokea; haitaonekana,
Thus saith the Lord Jehovah: “It shall not stand, neither shall it be;
8 maana kichwa cha Amramu ni Damaskasi, na kishwa cha Damaskasi ni Rezini. Ndani ya miaka sitini na tano, ndoto za Ephraimu zitasambaratishwa na hapatakuwa na watu.
But the head of Syria shall still be Damascus, And the head of Damascus, Rezin; [[And within threescore and five years shall Ephraim be broken, that he be no more a people.]]
9 Efraimu ni kichwa Samaria, na kishwa cha Samaria ni mtoto wa Remaria. Na kama hamtasimama imara katika imani yenu, hakika hamtakuwa salama''.
And the head of Ephraim shall still be Samaria, And the head of Samaria, the son of Remaliah. If ye will not believe, neither shall ye thrive.”
10 Bwana akaongea tena na Ahazi,
Jehovah spake also again to Ahaz:
11 ''Omba ishara ya Yahwe Mungu wako; omba juu ya hilo kwa kina au kwa kiwango cha juu.'' (Sheol h7585)
“Ask thee a sign of Jehovah, thy God; Ask it from below, or in the height above!” (Sheol h7585)
12 Lakini Ahazi anasema, sintomba wala kumjaribu Yahwe.''
And Ahaz said, I will not ask; I will not tempt Jehovah!
13 Hivyo Isaya akajibu, ''sikilizen, nyumba ya Daudi. Je haijatosha kwa watu kuujaribu uvumilivu wa watu? Je ni lazima kuujaribu uvumilivu wa Mungu?
Then he said, Hear ye now, O house of David! Is it too small a thing for you to weary men, That ye should weary my God also?
14 Hivyo basi Mungu mwenyewe atawapa yeye mwenywe ishara: ona, mwanamke bikira atapata mimba na kumzaa mtoto, na atamwita Emanueli.
Therefore shall Jehovah himself give you a sign: Behold, the damsel shall conceive, and bear a son, And she shall call his name Immanuel.
15 Atakula siagi na asali na wakati anapojua kuyakataa maovu na kuchagua mema.
Milk and honey shall he eat, Until he learn to refuse the evil, and choose the good;
16 Maana kabla mtoto ajajua kuyakataa maovu na kuchagua mema, nchi ambayo wewe unawachukia wafalme itakuwa ukiwa.
For before this child shall have learned to refuse the evil and choose the good, The land shall become desolate, On account of whose two kings thou art in terror.
17 Yahwe ataleta juu yako, juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako siku hazijatimmia tangu Efraimu alipompokea Yuda- atamleta mfalme wa Asiria.''
Yet Jehovah shall bring upon thee, and upon thy people, and upon thy father's house, Days such as have not been Since Ephraim revolted from Judah. [[Even the king of Assyria.]]
18 Mda huo Yahwe atapuliza filimbikwa ajili ya kupaa kutoka mkondo wa umbali wa Misri, na maana nyuki kutoka nchi ya Asiria.
And it shall come to pass in that day That Jehovah shall whistle for the fly that is at the end of the streams of Egypt, And the bee that is in the land of Assyria,
19 Zitakuja na kukaa chini ya korongo, ndani ya mapango ya miamba, kwenye vichaka vya miba, na kwenye malisho.
And they shall come, and light all of them In the desolate valleys, and fissures of the rocks, And upon all hedges, and upon all pastures.
20 Katika mda huo Bwana atamnyoa kichwani kichwani na nywele za miguuni kwa wembe ulioazimwa mto Efrarate— mfalme wa Asiria - na vilevile utasafisha ndevu zote.
In that day shall Jehovah shave, with a razor hired beyond the river, [[with the king of Assyria, ]] The head, and the hair of the feet; Yea, even the beard shall he take away.
21 Siku hiyo, mtu atahifadhi ndama na na kondoo wawili,
And it shall come to pass in that day, That a man shall keep a young cow, and two sheep;
22 na kwasababu ya maziwa yatakayo patikana ni mengi, atakula siagi, maana kila atakaye bakia kwnye nchi atakula siagi na asali.
And for the abundance of milk which they produce, shall he eat cheese; For milk and honey shall all eat Who are left in the land,
23 Mda huo, kutakuwa na maelfu ya mizabibu na thamani elfu za shekeli, hakutakuwa na kitu zaidi ya kuzalisha mbigiri na miiba.
And it shall come to pass in that day, That every place where stood a thousand vines, worth a thousand shekels of silver, Shall be covered with briers and thorns.
24 Watu watenda pale kuwinda kwa upinde, kwa sababu nchi yote itazalisha mbigiri na miiba.
With arrows and with bows shall men go thither; For all the land shall become briers and thorns.
25 Watakaa mbali na vilima vitalimwa kwa jembe, kwa sababu ya hofu ya mbigiri na miiba, lakini hapo patakuwa mahali pa kuchungia ngo'mbe na kondoo
All the hills that were digged with the mattock Shall no one approach through fear of briers and thorns; They shall be for the pasturage of oxen, And the trampling of sheep.

< Isaya 7 >