< Isaya 64 >

1 ''Oh, ikiwa umeigawa kwa kuifungua mbingu na kushuka chini! Milima inetikisika mbele yako,
Did You not tear the heavens? You came down, Mountains flowed from Your presence,
2 ni kama vile moto uunguzao vichaka, moto uchemshao maji. Oh, jina lako lingejulikana kwa maadui wako, na ya kwamba mataifa yangetetemeka mbele yako!
(As fire kindles stubble—Fire causes water to boil), To make Your Name known to Your adversaries, Nations tremble from Your presence.
3 Awali, ulipofanya mambo ya ajabu ambayo hatukuyategemea, ulishuka chini, milima ikatetemeka mbele zako.
In Your doing fearful things [that] we do not expect, You came down, Mountains flowed from Your presence.
4 Tangu nyakati za kale hakuna hata mmoja aliyesikia au kujua, wala jicho kuona Mungu yeyote karibu yake, ni nani afanyae mambo haya kwake anayemsubiri yeye.
Even from antiquity [men] have not heard, They have not given ear, Eye has not seen a God except You, He works for those waiting for Him.
5 Umekuja kuwasidia wale wanaofurahia kutenda yaliyo ya haki, wale wanaowaita kuwakumbusha njia zake na kumheshimu yeye. Ulipatwa na hasira tulipotenda dhambi. Katika njia zako daima tutakombolewa.
You have met with the rejoicer And the doer of righteousness, In Your ways they remember You, Behold, You have been angry when we sin, By them [is] continuance, and we are saved.
6 Maana sote tumekuwa kama mmoja aliye na unajisi, na matendo yetu ya haki yamekuwa kama hedhi kali. Sote tumenyauka kama majani; maovu yetu, ni kama upepo, unaotupeperusha sisi mbali.
And we are as unclean—all of us, And all our righteous acts [are] as garments of menstruation; And we fade as a leaf—all of us. And our iniquities take us away as wind.
7 Hakuna hata mmoja anayeita jina lako, hakuna anayefanya jitihada za kukushika wewe; maana umeuficha uso wako mbali na sisi na kutufanya sisi kuwa takataka katika mkono wa maovu yetu.
And there is none calling on Your Name, Stirring himself up to lay hold on You, For You have hid Your face from us, And You melt us away by our iniquities.
8 Na lakini, Yahwe, wewe ni baba yetu; sisi ni udongo. Wewe ni mfinyanzi wetu; sisi ni kazi ya mkono wako.
And now, O YHWH, You [are] our Father, We [are] the clay, and You [are] our Framer, And the work of Your hand—all of us.
9 Usiwe na hasira kubwa, Yahwe, wala daima usikumbuke maovu dhidi yetu, tafadhali sisi sote, watu wako.
Do not be angry, O YHWH, very severely, Nor remember iniquity forever, Behold, look attentively, we implore You, We [are] all Your people.
10 Miji yenu mitakatifu imekuwa jangwa; Sayuni imekuwa jangwa, Yerusalemu imekuwa ukiwa.
Your holy cities have been a wilderness, Zion has been a wilderness, Jerusalem a desolation.
11 Hekalu letu takatifu na zuri. mahali ambapo baba zetu walikusifu wewe, limeangamizwa kwa moto, na kila kilichokuwa karibu kiliharibiwa.
Our holy and our beautiful house, Where our fathers praised You, Has become burned with fire, And all our desirable things have become a ruin.
12 Je unawezaje kuendelea kumshika, Yahwe? Unawezaje kutulia kimya na kuendelea kutufedhehesha sisi?''
Do You refrain Yourself for these, YHWH? You are silent, and afflict us very severely!

< Isaya 64 >