< Isaya 63 >

1 Ni nani ajaye kutoka Edomu, aliyevaa mavazi rangi nyekundu kutoka Bozra? Ni nani aliye katika mavazi ya kifahari, anayetembea kwa kujiamini kwa sababu ya ukuu wa nguvu zake? Ndiye mimi, nizungumzae haki na uwezo mkubwa wa kuokoa.
Who [is] this coming from Edom? With dyed garments from Bozrah? This that is honorable in His clothing, Traveling in the abundance of His power? “I, speaking in righteousness, mighty to save.”
2 Kwa nini umevaa mavazi ya rangi nyekundu, na kwan nini wanaonekana kama akanyagae mizabibu katika vyombo vyake.
Why [is] Your clothing red? And Your garments as treading in a winepress?
3 Nimekanyaga zabibu lililoko katika vyombo vyenyewe, na hakuna hata mmoja kutoka mataifa aliyeungana na mimi. Niliwakanyaga kwa hasira yangu na niliwakanyaga wao kwa hasira yangu. Damu zao zimeruka katika nguo zangu na kuweka madoa nguo zangu zote.
“I have trodden a wine vat by Myself, And of the peoples there is no one with Me, And I tread them in My anger, And I trample them in My fury, Their strength is sprinkled on My garments, And I have defiled all My clothing.
4 Maana niliangalia mbele katika siku ya kisasi, na mwaka wa ukombozi ulikwishawadia.
For the day of vengeance [is] in My heart, And the year of My redeemed has come.
5 Mimi nilitazama, na hapo hapakuwa na mtu mmoja hata wa kutoa msaada, lakini mkono wangu mwenywe uliniletea ushindi mimi, na hasira yangu kubwa iliniongoza mimi.
And I look attentively, and there is none helping, And I am astonished that there is none supporting, And My own arm gives salvation to Me. And My wrath—it has supported Me.
6 Niliwakanyaga watu wangu chini kwa hasira yangu na kuwafanya wao wanywe laana yangu, na nilimwaga damu zao juu ya nchi.
And I tread down peoples in My anger, And I make them drunk in My fury, And I bring down their strength to earth.”
7 Nitakusimulia matendo ya agano la Yahwe lenye kuaminika, matendo ya kusifu ya Yahwe. Nitawasimulia yote ambayo Yahwe ametutendea sisi, na ukuu wa uzuri wake katika nyumba ya Israeli. Huruma hii aliyetuonyesha sisi kwa sababu ya rehema zake na matendo ya agano lake la kuaminika.
I make mention of the kind acts of YHWH, The praises of YHWH, According to all that YHWH has done for us, And the abundance of the goodness to the house of Israel, That He has done for them, According to His mercies, And according to the abundance of His kind acts.
8 Maana alisema, ''Baadhi yao ni watu wangu, watoto ambao sio waaminifu.'' Amekuwa mwokozi wao.
And He says, “Surely they [are] My people, Sons—they do not lie,” and He is to them for a Savior.
9 Kupitia mateso yao yote, aliteseka pia, na malaika kutoka mbele yake aliwaokoa wao. Katika upendo wake na rehema aliwakomboa wao, na aliwanyanyua juu na aliwabeba wote katika kipindi chote cha kale.
In all their distress [He is] no adversary, And the Messenger of His Presence saved them, In His love and in His pity He redeemed them, And He lifts them up, And carries them all the days of old.
10 Lakini walimuasi na kumuuzunisha roho mtakatifu. Hivyo basi akkawa adui wao na kupigana dhidi yao.
And they have been rebellious and have grieved His Holy Spirit, And He turns to them for an enemy, He Himself has fought against them.
11 Watu wake walifikiri kuhushu nyakati za kale za Musa. Walisema, ''Yuko wapi Mungu, aliyewaleta juu nje ya bahari pamoja na mchungaji wa kundi lake? Yuko wapi Mungu, ambaye aliyeweka roho mtakatifu mwiongoni mwenu?
And He remembers the days of old, Moses—his people. Where [is] He who is bringing them up from the sea, The shepherd of His flock? Where [is] He who is putting in its midst His Holy Spirit?
12 Yuko wapi Mungu, aliyeufanya wingi wa utukufu wake kwenda katika mkono wa kuume wa Musa, na ukaganya maji mbele yao, kulifanya jina lake milele yeye mwenyewe?
Leading by the right hand of Moses, the arm of His glory, Cleaving waters from before them, To make to Himself a continuous Name.
13 Yuko wapi Mungu, aliyewaongoza katika maji mengi? Kama farasi anayekimbia kwenye aridhi ambayo ni tambarare, hawakua na mashaka.
Leading them through the depths, They do not stumble as a horse in a plain.
14 Kama ng'ombe anayeshuka chini kwenye bonde, Roho ya Yahwe imewapa punziko. Hivyo umewaongoza watu wako, kufanya wewe mwenyewe jina la kusifu.
As a beast goes down into a valley, The Spirit of YHWH causes him to rest, So You have led Your people, To make to Yourself a glorious Name.
15 Tazama chini kutoka mbinguni na pata taarifa kutoka kwenye makao ya utukufu wako. Iko wapi bidii yenu na matendo makuu? Uruatendo yako ya uruma yamezuiliwaa kutoka kwetu.
Look attentively from the heavens, And see from Your holy and beautiful habitation, Where [is] Your zeal and Your might? The multitude of Your bowels and Your mercies—Are they restrained?
16 Maana wewe n baba yetu, Japokuwa Ibrahimu hatujui sisi, na Israeli haitutambui sisi, wewe, Yahwe, wewe ni baba yetu. Mkombozi wetu limekuwa jina lako kutoka nyakati za kale.
For You [are] our Father, For Abraham has not known us, And Israel does not acknowledge us, You, O YHWH, [are] our Father, Our Redeemer from the Age, [is] Your Name.
17 Yahwe, kwa nini unatufanya tangetange na kuifanya mioyo yetu kuwa migumu, hivyo hatukukuheshimu wewe? Rudi kwa niaba ya watumishi wako, kabila la urithi wako.
Why cause us to wander, O YHWH, from Your ways? You harden our heart from Your fear, Turn back for Your servants’ sake, The tribes of Your inheritance.
18 Watu wako walirithi mahali patakatifu kwa mda mfupi, halafu maadui zetu waliwakanyaga.
For a little while Your holy people possessed, Our adversaries have trodden down Your sanctuary.
19 Tumekuwa kama juu ya wale ambao hawajawai kuongoza, kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.
We have been from of old, You have not ruled over them, Your Name is not called on them!

< Isaya 63 >