< Isaya 63 >

1 Ni nani ajaye kutoka Edomu, aliyevaa mavazi rangi nyekundu kutoka Bozra? Ni nani aliye katika mavazi ya kifahari, anayetembea kwa kujiamini kwa sababu ya ukuu wa nguvu zake? Ndiye mimi, nizungumzae haki na uwezo mkubwa wa kuokoa.
Who is this that commeth from Edom, with red garments from Bozrah? hee is glorious in his apparel and walketh in his great strength: I speake in righteousnesse, and am mightie to saue.
2 Kwa nini umevaa mavazi ya rangi nyekundu, na kwan nini wanaonekana kama akanyagae mizabibu katika vyombo vyake.
Wherefore is thine apparel red, and thy garments like him that treadeth in ye wine presse?
3 Nimekanyaga zabibu lililoko katika vyombo vyenyewe, na hakuna hata mmoja kutoka mataifa aliyeungana na mimi. Niliwakanyaga kwa hasira yangu na niliwakanyaga wao kwa hasira yangu. Damu zao zimeruka katika nguo zangu na kuweka madoa nguo zangu zote.
I haue troden the wine presse alone, and of all people there was none with mee: for I will treade them in mine anger, and tread them vnder foote in my wrath, and their blood shalbe sprinkled vpon my garments, and I will staine all my raiment.
4 Maana niliangalia mbele katika siku ya kisasi, na mwaka wa ukombozi ulikwishawadia.
For the day of vengeance is in mine heart, and the yeere of my redeemed is come.
5 Mimi nilitazama, na hapo hapakuwa na mtu mmoja hata wa kutoa msaada, lakini mkono wangu mwenywe uliniletea ushindi mimi, na hasira yangu kubwa iliniongoza mimi.
And I looked, and there was none to helpe, and I wondered that there was none to vpholde: therefore mine owne arme helped me, and my wrath it selfe sustained me.
6 Niliwakanyaga watu wangu chini kwa hasira yangu na kuwafanya wao wanywe laana yangu, na nilimwaga damu zao juu ya nchi.
Therefore I wil tread downe the people in my wrath, and make them drunken in mine indignation, and wil bring downe their strength to the earth.
7 Nitakusimulia matendo ya agano la Yahwe lenye kuaminika, matendo ya kusifu ya Yahwe. Nitawasimulia yote ambayo Yahwe ametutendea sisi, na ukuu wa uzuri wake katika nyumba ya Israeli. Huruma hii aliyetuonyesha sisi kwa sababu ya rehema zake na matendo ya agano lake la kuaminika.
I wil remember the mercies of the Lord and the prayses of the Lord according vnto all that the Lord hath giuen vs, and for the great goodnesse toward the house of Israel, which hee hath giuen them according to his tender loue, and according to his great mercies.
8 Maana alisema, ''Baadhi yao ni watu wangu, watoto ambao sio waaminifu.'' Amekuwa mwokozi wao.
For he saide, Surely they are my people, children that wil not lie: so he was their Sauiour.
9 Kupitia mateso yao yote, aliteseka pia, na malaika kutoka mbele yake aliwaokoa wao. Katika upendo wake na rehema aliwakomboa wao, na aliwanyanyua juu na aliwabeba wote katika kipindi chote cha kale.
In all their troubles he was troubled, and the Angel of his presence saued them: in his loue and in his mercie he redeemed them, and he bare them and caried them alwayes continually.
10 Lakini walimuasi na kumuuzunisha roho mtakatifu. Hivyo basi akkawa adui wao na kupigana dhidi yao.
But they rebelled and vexed his holy Spirit: therefore was hee turned to be their enemie and he fought against them.
11 Watu wake walifikiri kuhushu nyakati za kale za Musa. Walisema, ''Yuko wapi Mungu, aliyewaleta juu nje ya bahari pamoja na mchungaji wa kundi lake? Yuko wapi Mungu, ambaye aliyeweka roho mtakatifu mwiongoni mwenu?
Then he remembred the olde time of Moses and his people, saying, Where is hee that brought them vp out of the Sea with the shepheard of his sheepe? where is he that put his holy Spirit within him?
12 Yuko wapi Mungu, aliyeufanya wingi wa utukufu wake kwenda katika mkono wa kuume wa Musa, na ukaganya maji mbele yao, kulifanya jina lake milele yeye mwenyewe?
He led them by the right hand of Moses with his owne glorious arme, deuiding the water before them, to make himselfe an euerlasting Name.
13 Yuko wapi Mungu, aliyewaongoza katika maji mengi? Kama farasi anayekimbia kwenye aridhi ambayo ni tambarare, hawakua na mashaka.
Hee led them through the deepe, as an horse in the wildernesse, that they should not stumble,
14 Kama ng'ombe anayeshuka chini kwenye bonde, Roho ya Yahwe imewapa punziko. Hivyo umewaongoza watu wako, kufanya wewe mwenyewe jina la kusifu.
As the beast goeth downe into the valley, the Spirite of the Lord gaue them rest: so diddest thou leade thy people, to make thy selfe a glorious Name.
15 Tazama chini kutoka mbinguni na pata taarifa kutoka kwenye makao ya utukufu wako. Iko wapi bidii yenu na matendo makuu? Uruatendo yako ya uruma yamezuiliwaa kutoka kwetu.
Looke downe from heauen, and beholde from the dwelling place of thine holines, and of thy glory. Where is thy zeale and thy strength, the multitude of thy mercies, and of thy compassions? they are restrained from me.
16 Maana wewe n baba yetu, Japokuwa Ibrahimu hatujui sisi, na Israeli haitutambui sisi, wewe, Yahwe, wewe ni baba yetu. Mkombozi wetu limekuwa jina lako kutoka nyakati za kale.
Doutles thou art our Father: though Abraham be ignorant of vs, and Israel knowe vs not, yet thou, O Lord, art our Father, and our redeemer: thy Name is for euer.
17 Yahwe, kwa nini unatufanya tangetange na kuifanya mioyo yetu kuwa migumu, hivyo hatukukuheshimu wewe? Rudi kwa niaba ya watumishi wako, kabila la urithi wako.
O Lord, why hast thou made vs to erre from thy wayes? and hardened our heart from thy feare? Returne for thy seruants sake, and for the tribes of thine inheritance.
18 Watu wako walirithi mahali patakatifu kwa mda mfupi, halafu maadui zetu waliwakanyaga.
The people of thine holinesse haue possessed it, but a litle while: for our aduersaries haue troden downe thy Sanctuarie.
19 Tumekuwa kama juu ya wale ambao hawajawai kuongoza, kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.
We haue bene as they, ouer whome thou neuer barest rule, and vpon whom thy Name was not called.

< Isaya 63 >