< Isaya 60 >
1 Nyanyuka, uangaze; maana mwanga wako umekuja, na utukufu wa Yahwe umekuja kwako.
Arise—shine, For thy light, hath come, —And, the glory of Yahweh, on thee, hath beamed;
2 Japokuwa giza litatanda katika nchi, na giza nene katika mataifa; Lakini Yahwe atakuja juu yenu, na utukufu wake utaonekana kwenu.
For lo! darkness, covereth the earth, And, deep gloom the peoples, —But, on thee, beameth Yahweh, And, his glory, on thee is seen.
3 Mataifa yatakuja kwenye mwanga wako, na wafalme katika mwanga wako mkali uliokuja
So shall nations come to thy light, And kings to the brightness of thy dawning.
4 Tazama na angalia pande zote. Wamekusanyika wao wenyewe kwa pamoja na wanakuja kwako. Watoto wako watatoka mbali, na binti zao watabebwa katika mikono yenu.
Lift up—round about—thine eyes and see, They all, have gathered themselves together—have come to thee, —Thy sons, from afar shall come, And thy daughters, on the side, shall be carried.
5 Halafu wataangalia na kuwa furaha, na moyo wako utafurahia na kufurika, maana wingi wa maji utamwagwa juu yenu, utajiri wa mataifa utakuja kwenu.
Then, shalt thou see and be radiant, And thy heart, shall throb and be enlarged, —For there shall be turned upon thee the fulness of the sea, The riches of the nations, shall come unto thee;
6 Msafara wa ngamia utawafunika ninyi, na ngamia wa Midiani na Efa; wote watakuja kutoka Sheba; wataleta dhahabu na ubani, wataimba sifa kwa Yahwe.
The multitude of camels, shall cover thee The young camels of Midian and Ephah, All they of Sheba, shall come, —Gold and frankincense, shall they bring, And, the praises of Yahweh, shall they joyfully tell:
7 Makundi yote ya Kedari yatakusanika kwa pamoja kwako, kondoo wa Nebaioti watabeba mahitaji yako; watakubalika kutolewa sadaka katika madhebau yangu; na nitaitukuza nyumba yangu takatifu.
All the flocks of Kedar, shall be gathered unto thee, The rams of Nebaioth, shall wait upon thee, —They shall come up, with acceptance, on mine altar, And my beautiful house, will I adorn.
8 Ni nani hawa wanopaa wenyewe kama mawingu, na kama njiwa kwenye makazi yao?
Who are these that, As a cloud, do fly? and, As doves to their cotes?
9 Pwani itanitafuta mimi, na meli ya Tarshishi huwaongoza, huwaleta watoto wenu kutoka mbali, pamoja na fedha zao na dhahabu zao, maana jina la Yahwe Mungu wenu, na Mtakatifu wa Israeli, maana amekuheshimu wewe.
Surely for me, shall, Coastlands, wait, And the ships of Tarshish first, To bring in thy sons, from far, Their silver and their gold with them, —Unto the name of Yahweh, thy God, And unto the Holy One of Israel Because he hath adorned thee.
10 Watoto wa wageni watajenga tena kuta zenu, n awafalme wao watawatumikia ninyi; japo katika laana yangu nimewaadhibu ninyi, lakini kwa neema yangu nitawahurumia ninyi.
So shall the sons of the foreigner, build thy walls, And their kings, shall wait upon thee, —For in my vexation, I smote thee, But in my favour, have I had compassion upon thee.
11 Milango yenu itaendelea kuwa wazi; haitafungwa mchana au usiku, hivyo utajiri wa mataifa ili uweze kuletwa, pamoja na viongozi wanowaongoza.
So shall thy gates be open—continually, Neither day nor night, shall they be shut, —That they may bring unto thee the riches of the nations, And their kings, be led.
12 Kweli, mataifa na falme ambayo hayatakutumikia wewe yatatoweka; mataifa hayo yataangamizwa kabisa.
For, the nation and the kingdom that will not serve thee, shall perish, —Yea the nations, shall be utterly wasted.
13 Utukufu wa Lebanoni utakuja kwako, mti wa msonobari, mtidhari, pamoja na msonobari ili kupamba madhebau yangu; na Nitalitukuza eneo la miguu yangu.
The glory of Lebanon, unto thee, shall come, The fir-tree the holm-oak, and the sherbin-cedar, together, To adorn the place of my sanctuary, And the place of my feet, will I make glorious.
14 Watakuja kwako kukusujudia wewe, watoto wa wale wanaokunyenyekea wewe; wataisujudia miguu yako; watakuita wewe mji wa Yahwe, sayani ya Mtakatifu wa Israeli.
Then shall come unto thee bending low, The sons of them who had humbled thee, Then shall bow down, unto the soles of thy feet, All they who had despised thee; And they shall call thee—The city of Yahweh, The Zion of the Holy One of Israel.
15 Badala yake uwepo wenu umetelekezwa na kuchukiwa, kwa kuwa hakuna hata mmoja anayepita ndani yenu, nitawafanya kuwa kitu cha kiburi milele, furaha kutoka kizazi hata kizazi.
Instead of thy being forsaken and hated so that none used to pass through thee, I will make of thee—An excellency age-abiding, The joy of generation after generation.
16 Pia utakunywa maziwa ya mataifa, utatunzwa katika kifua cha wafalme; utajua kwamba Mimi Yahwe, Mimi ni mwokozi na mkombozi wenu, aliye Mkuu wa Israeli.
And thou shalt derive sweet nourishment from the nations, Yea on the bounty of kings, shalt thou be sustained, —So shalt thou know—That, I, Yahweh, am thy Saviour, and That, thy Redeemer, is the Mighty One of Jacob.
17 Badala ya shaba Nitaleta dhahabu, badaia ya chuma nitaleta fedha; badala ya mbao, shabana badala ya jiwe, chuma. Nitachagua amani kwa kiongozi wenu, na haki kiongozi wenu.
Instead of bronze, I will bring in, gold, and Instead of iron, I will bring in silver, and Instead of wood, bronze, and Instead of stones, iron, —And I will appoint the oversight of thee to Prosperity, And the setting of thy tasks to Righteousness.
18 Vurugu hazitasikika katika aridhi yenu, uharibifu wala uvunjaji katika mipaka yenu; lakini mtaita kuta zenu wokovu, na malngo yenu mtayaita sifa.
Violence, shall no more be heard, in thy land, Wasting nor destruction within thy boundaries, —But thou shalt call Thy walls, Victory, and Thy gates, Praise.
19 Jua halitakuwa mwanga wenu wakati wa mchana, wala mwanga wa mwenzi wakati wa usiku hautawawakia ninyi; Lakini Yahwe atakuwa mwanga wenu wa milele, na Mungu wenu na utukufu wenu.
Thou shalt no more have the sun, for light by day, neither for brightness, shall the moon, give light unto thee, —But Yahweh shall become thine age-abiding light, And thy God thine adorning:
20 Jua lenu halitakuewepo wala mweni utaondoshwa na kutoweka; maana Yahwe atakuwa mwanga wenu daima, na siku za maombolezo zitakwisha.
No more shall go in, thy sun, Nor thy moon, withdraw itself, —For, Yahweh, will become to thee an age-abiding light, So shall be ended the days of thy mourning.
21 Watu wako wote watakuwa wenye haki; watachukuwa urithi wa nchi kwa mda wote, tawi la mazao yangu, kazi ya mikono yangu, ili niweze kuitukuza.
And, thy people, shall all of them, be righteous, To times age-abiding, shall they possess, the land, —The sprout of mine own planting, The work of mine own hands, —That I may get myself glory.
22 Mtoto atakuwa maelfu, na mdogo atakuwa taifa la wenye nguvu; Mimi Yahwe Nitayatimiza hayo mda utakapowadia.
The little one, shall become a thousand, and the small one, a mighty nation: I—Yahweh, in its own season, will hasten it.