< Isaya 60 >

1 Nyanyuka, uangaze; maana mwanga wako umekuja, na utukufu wa Yahwe umekuja kwako.
Arise, shine! for thy light is come, And the glory of Jehovah is risen upon thee.
2 Japokuwa giza litatanda katika nchi, na giza nene katika mataifa; Lakini Yahwe atakuja juu yenu, na utukufu wake utaonekana kwenu.
For, behold, darkness shall cover the earth, And gross darkness the nations; But upon thee shall Jehovah arise, And his glory shall be seen upon thee.
3 Mataifa yatakuja kwenye mwanga wako, na wafalme katika mwanga wako mkali uliokuja
Nations shall come to thy light, And kings to the brightness that riseth upon thee.
4 Tazama na angalia pande zote. Wamekusanyika wao wenyewe kwa pamoja na wanakuja kwako. Watoto wako watatoka mbali, na binti zao watabebwa katika mikono yenu.
Lift up thine eyes round about and see! They all gather themselves together, and come to thee; Thy sons come from afar, And thy daughters are carried at thy side.
5 Halafu wataangalia na kuwa furaha, na moyo wako utafurahia na kufurika, maana wingi wa maji utamwagwa juu yenu, utajiri wa mataifa utakuja kwenu.
Then shalt thou see, and be bright with joy; Thy heart shall throb, and swell with delight, When the riches of the sea shall be turned toward thee, And the wealth of the nations shall come to thee.
6 Msafara wa ngamia utawafunika ninyi, na ngamia wa Midiani na Efa; wote watakuja kutoka Sheba; wataleta dhahabu na ubani, wataimba sifa kwa Yahwe.
A multitude of camels shall cover thee, Dromedaries from Midian and Ephah; From Sheba shall they all come. Gold and frankincense shall they bring, And proclaim the praises of Jehovah.
7 Makundi yote ya Kedari yatakusanika kwa pamoja kwako, kondoo wa Nebaioti watabeba mahitaji yako; watakubalika kutolewa sadaka katika madhebau yangu; na nitaitukuza nyumba yangu takatifu.
All the flocks of Kedar shall be gathered to thee, And the rams of Nebaioth shall minister to thee; They shall ascend mine altar, an acceptable offering, And my glorious house I will adorn.
8 Ni nani hawa wanopaa wenyewe kama mawingu, na kama njiwa kwenye makazi yao?
Who are these that fly like clouds, And like doves to their habitations?
9 Pwani itanitafuta mimi, na meli ya Tarshishi huwaongoza, huwaleta watoto wenu kutoka mbali, pamoja na fedha zao na dhahabu zao, maana jina la Yahwe Mungu wenu, na Mtakatifu wa Israeli, maana amekuheshimu wewe.
Behold, the distant coasts shall wait for me, And the ships of Tarshish among the first, To bring thy sons from afar, And their silver and their gold with them, Because of the name of Jehovah thy God, Of the Holy One of Israel, for he glorifieth thee.
10 Watoto wa wageni watajenga tena kuta zenu, n awafalme wao watawatumikia ninyi; japo katika laana yangu nimewaadhibu ninyi, lakini kwa neema yangu nitawahurumia ninyi.
The sons of the stranger shall build up thy walls, And their kings shall minister to thee; For in my wrath I smote thee, But in my mercy will I have pity upon thee.
11 Milango yenu itaendelea kuwa wazi; haitafungwa mchana au usiku, hivyo utajiri wa mataifa ili uweze kuletwa, pamoja na viongozi wanowaongoza.
Thy gates shall be open continually; They shall not be shut by day or by night, That the treasures of the nations may be brought to thee, And that their kings may come with their retinues.
12 Kweli, mataifa na falme ambayo hayatakutumikia wewe yatatoweka; mataifa hayo yataangamizwa kabisa.
For that nation and that kingdom Which will not serve thee shall perish; Yea, those nations shall be utterly destroyed.
13 Utukufu wa Lebanoni utakuja kwako, mti wa msonobari, mtidhari, pamoja na msonobari ili kupamba madhebau yangu; na Nitalitukuza eneo la miguu yangu.
The glory of Lebanon shall come to thee, The cypress, the plane-tree, and the larch together, To adorn the place of my sanctuary, That I may make the place where my feet rest glorious.
14 Watakuja kwako kukusujudia wewe, watoto wa wale wanaokunyenyekea wewe; wataisujudia miguu yako; watakuita wewe mji wa Yahwe, sayani ya Mtakatifu wa Israeli.
The sons of thine oppressors shall come bending before thee; They that despised thee shall fall down at thy feet; And they shall call thee the city of Jehovah, The Zion of the Holy One of Israel.
15 Badala yake uwepo wenu umetelekezwa na kuchukiwa, kwa kuwa hakuna hata mmoja anayepita ndani yenu, nitawafanya kuwa kitu cha kiburi milele, furaha kutoka kizazi hata kizazi.
Instead of being forsaken and hated, So that no one passed through thee, I will make thee an everlasting glory; The joy of many generations.
16 Pia utakunywa maziwa ya mataifa, utatunzwa katika kifua cha wafalme; utajua kwamba Mimi Yahwe, Mimi ni mwokozi na mkombozi wenu, aliye Mkuu wa Israeli.
Thou shalt also suck the milk of the nations, And be nursed from the breast of kings; And thou shalt know that I, Jehovah, am thy saviour, That thy redeemer is the Mighty One of Jacob.
17 Badala ya shaba Nitaleta dhahabu, badaia ya chuma nitaleta fedha; badala ya mbao, shabana badala ya jiwe, chuma. Nitachagua amani kwa kiongozi wenu, na haki kiongozi wenu.
Instead of brass will I bring gold; And instead of iron will I bring silver, And instead of wood, brass, And instead of stones, iron; I will make thine officers peace, And thy magistrates righteousness.
18 Vurugu hazitasikika katika aridhi yenu, uharibifu wala uvunjaji katika mipaka yenu; lakini mtaita kuta zenu wokovu, na malngo yenu mtayaita sifa.
Violence shall no more be heard in thy land, Wasting or destruction within thy borders; Thou shalt call thy walls Salvation, And thy gates Praise.
19 Jua halitakuwa mwanga wenu wakati wa mchana, wala mwanga wa mwenzi wakati wa usiku hautawawakia ninyi; Lakini Yahwe atakuwa mwanga wenu wa milele, na Mungu wenu na utukufu wenu.
No more shall the sun be thy light by day, Nor with her brightness shall the moon enlighten thee: But Jehovah shall be to thee an everlasting light, And thy God thy glory.
20 Jua lenu halitakuewepo wala mweni utaondoshwa na kutoweka; maana Yahwe atakuwa mwanga wenu daima, na siku za maombolezo zitakwisha.
Thy sun shall no more go down, Neither shall thy moon be hid; For Jehovah shall be thine everlasting light, And the days of thy mourning shall be ended.
21 Watu wako wote watakuwa wenye haki; watachukuwa urithi wa nchi kwa mda wote, tawi la mazao yangu, kazi ya mikono yangu, ili niweze kuitukuza.
Thy people shall be all righteous; Forever shall they possess the land, The scion of my planting, The work of my hands, that I may be glorified.
22 Mtoto atakuwa maelfu, na mdogo atakuwa taifa la wenye nguvu; Mimi Yahwe Nitayatimiza hayo mda utakapowadia.
The little one shall become a thousand, And the small one a strong nation; I, Jehovah, will hasten it in its time.

< Isaya 60 >