< Isaya 53 >

1 Ni nani angeweza kuamini tuliyasikia? Na mkono wa Yahwe, kwake uliojidhihirisha?
Who has believed our message? To whom has the arm of Adonai been revealed?
2 Maana amekuwa mbele za Yahwe kama sampuli, na kama chipukizikatika aridhi kavu; hakuna maajabu yalionekana au mapambo; tulipo muona yeye, hapakuwa na uzuri kutuvutia sisi.
For he grew up before him as a tender plant, and as a root out of dry ground. He has no good looks or majesty. When we see him, there is no beauty that we should desire him.
3 Alidharauliwa na kukataliwa na watu; mtu wa huzuni, na mwenye maumivu. Kama mmoja aliyetoka kwa watu wafichao nyuso zao, alidharauliwa; na kujfikiria kuwa asiye na faida.
He was despised, and rejected by men; a man of suffering, and acquainted with disease. He was despised as one from whom men hide their face; and we didn’t respect him.
4 Lakini hakika amezaliwa ugonjwa wetu na kubeba huzuni yetu; tulidhani aliadhibiwa na Mungu, amepigwa na Mungu, na kutaabishwa.
Surely he has borne our sickness, and carried our suffering; yet we considered him plagued, struck by God, and afflicted.
5 Lakini alichomwa kwa sababu ya uaasi wa matendo yetu; aliangamizwa kwa sababu ya dhambi zetu. Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, na kwa majeraha yake sisi tumepona.
But he was pierced for our transgressions. He was crushed for our iniquities. The punishment that brought our peace was on him; and by his stripes and wounds we are healed and made whole.
6 Sisi ni kama kondoo tumepotoka; kila mmoja amejeuka katika njia yake, na Yahwe amemueka juu yake maovu kwetu sisi sote.
All we like sheep have gone astray. Everyone has turned to his own way; and Adonai has laid on him the iniquity of us all.
7 Aliteswa; lakini alinyenyekea mwenyewe, hakufungua mdomo wake; kama kondooendae kuchinjwa, na kama kondoo mbele ya mtu anayemkata mnyoa yake taratibu, hivyo hakufungua mdomo wake.
He was oppressed, yet when he was afflicted he didn’t open his mouth. As a lamb that is led to the slaughter, and as a sheep that before its shearers is silent, so he didn’t open his mouth.
8 Kwa kutumia nguvu na hukumu yeye aliyelaaniwa; ni katika kizazi hicho atafikiria zaidi kuhusu yeye? Lakini aliondolewa katika aridhi ya walio hai; kwa sababu ya makosa ya watu wangu na adhabu ilikuwa juu yake.
After forcible arrest and sentencing, he was taken away; and none of his generation protested his being cut off out of the land of the living for the crimes of my people, who deserved the punishment themselves.
9 Wameliweka kaburi lake pamoja nawahalifu, kwa utajiri wa mtu katika kifo chake ingawa hakuwa na vurugu wala udanganyifu wowote katika mdomo wake.
They made his grave with the wicked, and with a rich man in his death; although he had done no violence, nor was any deceit in his mouth.
10 Lakini yalikuwa ni mapenzi ya Yahwe kumponda yeye na kumfanya yeye apone. Alipoyafanya maisha yake kuwa sadaka kwa ajili ya dhambi, ataona watoto wake, ataongeza siku zao, na mapenzi ya Yahwe yatatimizwa kupitia yeye.
Yet it pleased Adonai to bruise him. He has caused him to suffer. To see if he would present himself as a guilt offering. If he does, he will see his offspring, and he will prolong his days, and Adonai’s pleasure will prosper in his hand.
11 Baada ya mateso ya maisha yake, ataona mwanga na ataridhika kwa maarifa yake.
After this ordeal, he will see satisfaction “By his knowing [pain and sacrifice]. My righteous servant will justify many; for it is their sins that he suffers.
12 Hivyo basi Je ninaweza kumpa yeye sehemu yake miongoni mwa wengi, naye atatawnya mateka kwa wengi, kwa sabubu amejionyesha yeye mwenye kwenye kifo na amehesabiwa na wahalifu. Amezaa dhambi za wengi na kufanya maombolezo kwa wahalifu.
Therefore will I give him a portion with the great, and he will divide the spoils with the strong; because he exposed himself to death, and was counted with the transgressors; while actually bearing the sin of many, and interceding for the offenders.

< Isaya 53 >