< Isaya 47 >
1 Njoo chini na ukae kwenye mavumbi, binti bikira wa Babeli; kaa juu ya aridhi pasipo enzi, ewe binti wa Wakaldayo. Hautaitwa tena mpenda anasa na maisha ya anasa.
Down—and sit in the dust, O virgin Daughter of Babylon, Sit on the ground—throneless, Daughter of the Chaldeans; For thou shalt no more be called Tender and Dainty.
2 Chukua jiwe la kusagia na usage unga; ondoa pazia lako, ondoa mavazi yako, ondoa viatu miguuni, na vuka mkondo wa maji.
Take millstones, and grind meal, —Put back thy veil—tuck up thy train Bare the leg, wade through streams:
3 Uchi wako utafunuliwa, ndio, na aibu yako itaonekana; Nitachukua kizazi na sitamuacha mtu,
Bared shall be thy shame, Yea seen thy reproach, —An avenging, will I take, And will accept no son of earth.
4 Mkombozi, Yahwe wa majeshi ndilo jina lake, Mtakatifu wa Israeli.
Our Redeemer, Yahweh of hosts, is his name! The Holy One of Israel.
5 Kaa kimya na nenda katika giza, ewe binti wa Wakaldoyo; maana hautaitwa tena malikia wa falme.
Sit silent, and get into darkness, Daughter of the Chaldeans! For thou shalt no more be called Mistress of Kingdoms.
6 Nilikuwa na hasira na watu wangu; Nimeunajisi urithi wangu na kuwakabidhi nyie katika mkono wenu, lakini hamkuomyesha huruma; umeweka nira kubwa kwa wazee.
I had been provoked with my people, Had profaned mine inheritance, And given them into thy hand, …Thou shewedst them no compassion, Upon the elder, madest thou very heavy thy yoke.
7 Umesema, ''Nitaongoza daima kama malikia huru.'' Haukuvichukua vitu hivi katika moyo, wala hakutafakari jinsi hivi vitu vitakavyojeuka.
And thou saidst, Unto times age-abiding, shall I be Mistress, —Insomuch that thou laidst not these things to thy heart, Didst not keep in mind the issue thereof,
8 Hivyo sasa sikiliza hili, Ewe upendae anasa na kukaa salama; ewe usemae katika moyo wako, 'Ninaishi, na hakuna mwingine kama mimi; Sitakaa kama mjane wala sitazoea kufiwa na watoto.
Now, therefore hear this, Thou Lady of pleasure Who dwelleth securely, Who saith in her heart, —I, [am], and there is no one besides, I shall not sit a widow, Nor know loss of children.
9 ''Lakini vitu hivi vitakuja kwako siku moja katika kipindi cha siku moja; kwa nguvu za kutosha yatakuja kwako, japo uchawi wako na dua zako na hirizi.
Yet shall there come to thee—both these, in a moment, in one day, Loss of children and widowhood, —To their full, have they come on thee, Spite of the mass of thine incantations, Spite of the great throng of thy spells.
10 Umeweka imani katika mapungufu yako; na kusema, ''Hakuna anayeniona mimi''; hekima na maarifa yako yanakupoteza, lakini unasema katika moyo wako, ''Nipo na hakuna hata mmoja kama mimi.''
And so thou didst trust in thy wickedness, Thou saidst, no one, seeth me, Thy wisdom and knowledge, the same, seduced thee, —Therefore saidst thou in thy heart, I [am], and there is no one besides.
11 Maafa yatakuzidi wewe; hautaweza kuyaondoa kwa dua zako mwenyewe. Uharibifu utakuwa juu yako; hautaweza kuukata. Maafa yatakuangamiza ghafla, kabla haujajua kitu.
Therefore shall come on thee—Mischief, Thou shalt not know how to charm it away Yea there shall fall on thee, Ruin, Thou shalt not be able to appease it, —And there shall come on thee suddenly. Desolation. Thou shalt not know.
12 Endeleni kutoa uganga wako na wachawi wengi ambao mlioaminishwa kusoma toka utotoni mwao; labda utafanikiwa, labda utayashinda maafa.
Take thy stand, I pray thee, With thy spells. And with the throng of thine incantations wherein thou hast wearied thyself from thy youth, —Peradventure thou mayest be able to profit Peradventure thou mayest strike me with terror.
13 Umejaribu sana kwa kushauriwa sana; waache hao watu wasimame na kukuokoa wewe- wale wanaoangalia mbingu na wanoangalia nyota, wale wanotangaza mwenzi mpya- waache wawaokoe nyie kutoka kwenye yaliyowapata.
Thou hast worn thyself out with the mass of thy consultations, —Let them take their stand I pray thee that they may save thee—The dividers of the heavens—The gazers at the stars, They who make known by new moons, Somewhat of the things which shall come upon thee.
14 Tazama, watakuwa kama mabua. Moto utayachoma juu. Hayataweza kujisaidia yenyewe kutoka kwenye mkono wa moto. Hakuna makaa kuwapa joto wao na hakuna moto uliowekwa pembeni kwa ajili yao!
Lo! they have become as straw—a fire, hath burned them up, They shall not deliver their own soul from the grasp of the flame, —There is, no live coal to warm them, nor blaze to sit before.
15 Hivi ndio wamekuwa kwako, wale unaofanya nao kazi, na unauza na kununua na wao toka ulipo kuwa mdogo, na wale wanaendelea kufanya mambo yao ya kijinga; na unapolia kuhitaji msaada, hakuna hata mmjoa ambaye atakukomboa wewe.''
Such, have they become to thee, with whom thou hast wearied thyself, —Thy merchants—from thy youth, will every man stagger straight onwards—There is none to save thee.