< Isaya 47 >

1 Njoo chini na ukae kwenye mavumbi, binti bikira wa Babeli; kaa juu ya aridhi pasipo enzi, ewe binti wa Wakaldayo. Hautaitwa tena mpenda anasa na maisha ya anasa.
Descend, sit in the dust, O virgin daughter of Babylon! Sit on the ground. There is no throne for the daughter of the Chaldeans. For you shall no longer be called delicate and tender.
2 Chukua jiwe la kusagia na usage unga; ondoa pazia lako, ondoa mavazi yako, ondoa viatu miguuni, na vuka mkondo wa maji.
Take a millstone and grind meal. Uncover your shame, bare your shoulder, reveal your legs, cross the streams.
3 Uchi wako utafunuliwa, ndio, na aibu yako itaonekana; Nitachukua kizazi na sitamuacha mtu,
Your disgrace will be revealed, and your shame will be seen. I will seize vengeance, and no man will withstand me.
4 Mkombozi, Yahwe wa majeshi ndilo jina lake, Mtakatifu wa Israeli.
Our Redeemer, the Lord of hosts is his name, the Holy One of Israel.
5 Kaa kimya na nenda katika giza, ewe binti wa Wakaldoyo; maana hautaitwa tena malikia wa falme.
Sit in silence, and enter into darkness, O daughter of the Chaldeans! For you shall no longer be called the noblewoman of kingdoms.
6 Nilikuwa na hasira na watu wangu; Nimeunajisi urithi wangu na kuwakabidhi nyie katika mkono wenu, lakini hamkuomyesha huruma; umeweka nira kubwa kwa wazee.
I was angry with my people. I have polluted my inheritance, and I have given them into your hand. You have not shown mercy to them. You have greatly increased the burden of your yoke upon the elders.
7 Umesema, ''Nitaongoza daima kama malikia huru.'' Haukuvichukua vitu hivi katika moyo, wala hakutafakari jinsi hivi vitu vitakavyojeuka.
And you have said: “I will be a noblewoman forever.” You have not set these things upon your heart, and you have not remembered your end.
8 Hivyo sasa sikiliza hili, Ewe upendae anasa na kukaa salama; ewe usemae katika moyo wako, 'Ninaishi, na hakuna mwingine kama mimi; Sitakaa kama mjane wala sitazoea kufiwa na watoto.
And now, hear these things, you who are delicate and have confidence, who say in your heart: “I am, and there is no one greater than me. I will not sit as a widow, and I will not know barrenness.”
9 ''Lakini vitu hivi vitakuja kwako siku moja katika kipindi cha siku moja; kwa nguvu za kutosha yatakuja kwako, japo uchawi wako na dua zako na hirizi.
These two things will suddenly overwhelm you in one day: barrenness and widowhood. All things shall overwhelm you, because of the multitude of your sorceries and because of the great cruelty of your enchantments.
10 Umeweka imani katika mapungufu yako; na kusema, ''Hakuna anayeniona mimi''; hekima na maarifa yako yanakupoteza, lakini unasema katika moyo wako, ''Nipo na hakuna hata mmoja kama mimi.''
And you have trusted in your malice, and you have said: “There is no one who sees me.” Your wisdom and your knowledge, these have deceived you. And you have said in your heart: “I am, and beside me there is no other.”
11 Maafa yatakuzidi wewe; hautaweza kuyaondoa kwa dua zako mwenyewe. Uharibifu utakuwa juu yako; hautaweza kuukata. Maafa yatakuangamiza ghafla, kabla haujajua kitu.
Evil will overwhelm you, and you will not notice its rising. And calamity will fall violently over you, and you will not be able to avert it. You will suddenly be overwhelmed by a misery such as you have never known.
12 Endeleni kutoa uganga wako na wachawi wengi ambao mlioaminishwa kusoma toka utotoni mwao; labda utafanikiwa, labda utayashinda maafa.
Stand with your incantations, and with the multitude of your sorceries, in which you have labored from your youth, as if somehow it might benefit you, or as if it were able to make you stronger.
13 Umejaribu sana kwa kushauriwa sana; waache hao watu wasimame na kukuokoa wewe- wale wanaoangalia mbingu na wanoangalia nyota, wale wanotangaza mwenzi mpya- waache wawaokoe nyie kutoka kwenye yaliyowapata.
You have failed in the multitude of your plans! Let the seers stand and save you, those who were contemplating the stars, and figuring the months, so that from these they might announce to you the things to come.
14 Tazama, watakuwa kama mabua. Moto utayachoma juu. Hayataweza kujisaidia yenyewe kutoka kwenye mkono wa moto. Hakuna makaa kuwapa joto wao na hakuna moto uliowekwa pembeni kwa ajili yao!
Behold, they have become like stubble. Fire has consumed them. They will not free themselves from the power of the flames. These are not coals by which they may be warmed, nor is this a fire which they may sit beside.
15 Hivi ndio wamekuwa kwako, wale unaofanya nao kazi, na unauza na kununua na wao toka ulipo kuwa mdogo, na wale wanaendelea kufanya mambo yao ya kijinga; na unapolia kuhitaji msaada, hakuna hata mmjoa ambaye atakukomboa wewe.''
So have all these things, in which you have labored, become to you. Your merchants from your youth, each one has erred in his own way. There is no one who can save you.

< Isaya 47 >