< Isaya 46 >

1 Beli huaguka chini, Nebo husujudu; miungu yao imebebwa na wanyama na mzigo wa mnyama. Sanamu hizi mlizobeba ni mzigo mzito kwa wanyama kuchoka.
Bel is bowed down, Nebo sinketh, their idols are [delivered] unto the beasts, and unto the cattle; those which were once carried by you are now laden up a burden to the weary beasts.
2 Kwa pamoja wanashuka chini; hawawezi kuziokoa sanamu zao, na wao wenyewe wameenda uhamishoni.
They are sunk, they are bowed down together; they could not deliver the burden, but they themselves are gone into captivity.
3 Nisikilizeni mimi, nyumba ya Yakobo, wote mliobaki kwenye nyumba ya Israeli mliochukuliwa na mimi kutoka kabla amjazaliwa, mlichukuliwa mkiwa tumboni.
Hearken unto me, O house of Jacob, and all the remnant of the house of Israel, who are borne [by me] from their birth, who are carried from the womb;
4 Hata kwa njie wazee Mimi ndiye, mpaka mmeshapata mvi nitawachukua. Nimewaumba ninyi na nitawabeba ninyi; Nitwachukua nyie na nitawakomboa nyie.
And even unto old age I am the same; and even unto the time of hoary hairs will I bear: l have done it, and I will carry [you]; even I will bear, and deliver you.
5 Je utanifananisha mimi na nani? na mimi nimefanana na nani, ili utulinganishe?
To whom will ye liken and assimilate me, and compare me, that we may be like?
6 Watu humwaga dhahabu kutoka kwenye mabegi yao na uzito wa fedha kwenye uzani. Humuajiri mfua dhahabu, na hutengeneza kuwa dhahabu; na huinama chini na kuzisuju.
[There are those] that lavish gold out of the bag, and weigh silver in the balance; that hire a melter, that he may make of it a god; they [then] bend the knee, yea, they bow themselves down;
7 Wanazinyanyua juu ya mabega yao na kuzibeba; wanaziweka katika sehemu yake, na itasimama katika eneo lake na alitasogea kutoka pale, hulilia, lakini haiwezi kujibu wala kumuokoa yeyote kwenye matatizo.
They carry him, upon the shoulder they bear him, and set up him in his spot, and he remaineth standing, from his place he doth not move: yea, though one should cry unto him, he cannot answer, out of his trouble he cannot help him.
8 Tafakari kuhusu hivi vitu; katu usivipuuzie, enyi waasi!
Remember this, and take courage: take it again to heart, O ye transgressors.
9 Tafakari kuhusu vitu vya awali, nyakati zile zilizopita, Maana mimi ni Mungu, na hakuna mwingine, Mimi ni Mungu na hakuna kama mimi.
Remember the former things of olden times; for I am God, and there is no one else; I am God, and there is nothing like me.
10 Mimi ninatangaza mwisho kutoka mwanzo, na kabla ya kitu ambacho hakijatokea; Ninasema, ''Mpango wangu utatokea na nitafanya kama ninavyotamani.''
Declaring from the beginning the end, and from the earliest days the things that have not yet been done, saying, My counsel shall stand firm, and all my pleasure will I do:
11 Nitamuita ndege wa mawindo kutoka mashariki, Mtu ambaye ni chaguo langu kutoka nchi ya mbali; Ndio nimesema; na pia nitayatimiza haya, nimekusudia, na pia nitafanya hivyo.
Calling from the east the eagle, from a far-off country the man of my counsel; yea, I have spoken it, I will also bring it to pass; I have purposed it, I will also execute it.
12 Nisikilize mimi, enyi watu makaidi, ambao mko mbali na kutenda mema.
Hearken unto me, ye stout of heart, that are far from righteousness:
13 Ninaileta haki yangu karibu; na wala sio mbali, na wokovu wangu hausubiri; na nitatoa wokovu wangu kwa Sayuni na uzuri wangu kwa Israeli.
I have brought near my righteousness; it shall not be far off, and my salvation shall not tarry: and I will grant unto Zion salvation, unto Israel my glory.

< Isaya 46 >