< Isaya 41 >
1 ''Sikilizeni mbele yangu kwa ukimya, enyi mkao pwani; wacha mataifa yapate nguvu kwa upya; waache waje karibu na kuzungumza; na tusogee karibu tujadili mgogoro.
Keep silent toward Me, O islands, And the peoples pass on [to] power, They come near, then they speak, “Together we draw near to judgment.”
2 Nani aliyechochea juu mmoja kutoka mashariki, anamuita katika haki yake kwenye huduma yake? Amemkabidhi mataifa juu yake ili amsaidie yeye kuwaangamiza wafalme. Aliwajeuza kuwa mavumbi kwa neno lake, kama upepo unaovuma kwenye mabua kwa upinde wake.
Who stirred up a righteous one from the east? He calls him to His foot, He gives nations before him, And He causes him to rule kings, He gives [them] as dust [to] his sword, As driven stubble [to] his bow.
3 Aliwachukuwa wao na kuwapitisha salama, katika njia nyepesi ambayo miguu yake imegusa shida.
He pursues them, he passes over in safety A path he does not enter with his feet.
4 Ni nani aliyeyafanya na kukamilisha matendo haya? Ni nanialiyechagua kizazi kutoka mwanzo? Mimi, Yahwe ni mwanzo na mwisho, mimi ndiye.
Who has worked and done, Calling the generations from the first? I, YHWH, the first, and with the last I [am] He.
5 Visiwa vimeona na kuogopa; miisho ya dunia yatetemeka; walikaribia n kuja.
Islands have seen and fear, The ends of the earth tremble, They have drawn near, indeed, they come.
6 Kila mmoja amsaidie jirani yake, na kila mmoja asemezane na mwenzake, 'Kuwa mfariji;
They each help his neighbor, And to his brother he says, “Be strong.”
7 Hivyo basi seremala anamfariji mfua dhahabu, na yule anayefanya kazi kwa kutumia nyundo anamfariji anayefanya kazi kwa chuma, akisema kwa msemo wa kurehemu, ''Ni mizuri; Naye ataupigilia kwa makini misumari ili isipinduke.
And an artisan strengthens the refiner, A smoother [with] a hammer, Him who is beating [on] an anvil, saying, “For joining it [is] good,” And he strengthens it with nails, it is not moved!
8 Lakini wewe, Israeli mtumishi wangu, Yakobo niliyekuchagua, mtoto wa Ibrahimu rafiki yangu,
And you, O Israel, My servant, Jacob, whom I have chosen, Seed of Abraham, My lover,
9 wewe ambaye ninakurudisha kutoka miisho ya nchi, na ambaye niliyekuita kutoka sehemu ya mbali, na kwako niliyekuambia, 'Wewe ni mtumishi wangu; 'Nimekuchagua wewe na sijakukataa.
Whom I have taken hold of, from the ends of the earth, And from its near places I have called you, And I say to you, You [are] My servant, I have chosen you, and not rejected you.
10 Usiogope maana mimi niko pamoja na wewe. Usiwe na wasiwasi, maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu, na nitakusaidia, wewe, na Nitakushika kwa mkono wa haki yangu.
Do not be afraid, for I [am] with you, do not look around, for I [am] your God, I have strengthened you, Indeed, I have helped you, indeed, I upheld you, With the right hand of My righteousness.
11 Tazama, watakuwa na aibu na hawataheshimiwa, wale wote waliokuwa na hasira na wewe; watakuwa si kitu na watatokomea, wale watakao kupinga wewe.
Behold, all those displeased with you, They are ashamed and blush, They are as nothing, indeed, The men who strive with you perish.
12 Utawatafuta na wala hautawapata wale wanaopingana na wewe; wale wafanyao vita dhidi yako watakuwa kama si kitu, si kitu kabisa.
You seek them, and do not find them, The men who debate with you, They are as nothing, indeed, as nothing, The men who war with you.
13 Maana mimi Yahwe Mungu wako, nitawashika mkono wako wa kiume, nikikuambia wewe, 'Usiogope; Nitakusaidia wewe.
For I, your God YHWH, Am strengthening your right hand, He who is saying to you, “Do not fear, I have helped you.”
14 Usiogope, Yakobo wewe mdudu, na enyi watu wa Israeli; Nitawasaidia''- hili ni tamko la Yahwe, Mkombozi wako, Mtakatifu wa Israeli.
Do not fear, O worm Jacob, You men of Israel, I helped you, a declaration of YHWH, Even your redeemer, the Holy One of Israel.
15 Tazama, ninakufanya wewe kuwa chombo kikali cha kuparulia chenye makali pande mbili; utaparua milima na kuiponda; utafanya vilima kama makapi.
Behold, I have set you for a new sharp threshing instrument, Possessing teeth, you thresh mountains, And beat small, and make hills as chaff.
16 Utawatawanya wao, na upepo utawabeba na kuwapeka mbali; upepo utawatanya wao. Utashanglia katika Yahwe, utashangiliakatika mtakatifu wa Israeli
You winnow them, and a wind lifts them up, And a whirlwind scatters them, And you rejoice in YHWH, [And] boast yourself in the Holy One of Israel.
17 Waliodhulumiwa na masikini wanatafuta maji, lakini hakuna kitu, ndimi zao zimekauka kwa kiu; Mimi Yahwe, nitajibu maombi yao; Mimi Mungu wa Israeli, sitawacha wao.
The poor and the needy are seeking water, And there is none, Their tongue has failed with thirst, I, YHWH, answer them, The God of Israel—I do not forsake them.
18 Nitatengeneza mikondo ya maji kushusha chini, na chemichem katikati ya mabonde; nitalifanya jangwa kuwa kisima cha maji, na aridhi kavu kuwa chemichem ya maji.
I open rivers on high places, And fountains in midst of valleys, I make a wilderness become a pond of water, And a dry land becomes springs of water.
19 Katika jangwa nitapanda mierezi, mshita, mhadisi, na mti wa mizeituni. Nitaotesha mberoshi katika uwazi wa jangwa, pamoja na mbono nitapanda mberoshi kitika jangwa lililowazi.
I give in a wilderness the cedar, Shittah, and myrtle, and oil-tree, I set in a desert the fir-pine and box-wood together.
20 Nitayafanya haya ili waweze kuona, kutambua na kuelewa kwa pamoja, kwamba mkono wa Yahwe umetenda haya, kama Mtakatifu wa Israeli aliyeliumba.
So that they see, and know, And regard, and act wisely together, For the hand of YHWH has done this, And the Holy One of Israel has created it.
21 Wakilisha keshi yako, '' asema Yahwe; ''wakilisha hoja zenu nzuri kwa sanamu yenu,'' asema Mfalme wa Yakobo.
Bring your cause near, says YHWH, Bring your mighty ones near, says the King of Jacob.
22 Waache walete hoja zao wenyewe; waache waje mbele na watutangazie sisi nini kitakachotokea, ili tuweze kuelewa haya mambo vizuri. Tuawaache watupe tamko mapema, ili tuweze kulitafakari na tuweze kujua n kwa jinsi gani litatimia.
They bring [them] near, and declare to us that which happens, Declare the first things—what they [are], And we set our heart, and know their latter end, Or cause us to hear the coming things.
23 Wajulishe kitu kuhusu baadaye, ili tujue kuwa ninyi ni miungu; fanya kitu kizuri au kibaya, ambacho kitatutisha na kutushangaza.
Declare the things that are coming hereafter, And we know that you [are] gods, Indeed, you may do good or do evil, And we look around and see [it] together.
24 Tazama sanamu zenu si kitu na matendo yenu si kitu; aliyewachagua ni machukizo.
Behold, you [are] of nothing, and your work of nothing, An abomination—it fixes on you.
25 Nimemnyanyua mmoja kutoka kaskazini, naye amekuja kutoka mawio ya jua nimemchagua yeye alitajae jina langu, na atawakanyaga viongozi kama matope, kama mfinyanzi akanyagavyo udongo.
I have stirred up [one] from the north, And he comes, From the rising of the sun he calls in My Name, And he comes in [on] prefects as [on] clay, And as a potter treads down mire.
26 Ni nani aliyetangaza hili tangu mwanzo, ili tuweze kujua? na kabla ya mda, ili tuseme, ''Yuko sawasawa''? Kweli hakuna hata mmoja aliyekiri hili, ndio hakuna hata mmoja aliyekusikia ukisema chochote.
Who has declared from the first, and we know? And formerly, and we say, “Righteous?” Indeed, there is none declaring, Indeed, there is none proclaiming, Indeed, there is none hearing your sayings.
27 Kwanza nilizungumza na Sayuni, ''Tazama hapo walipo;'' Nimemtuma mhubiri Yerusalemu.
First to Zion, Behold, behold them, And to Jerusalem I give one proclaiming tidings,
28 Nilipoangalia, hakuna hata mmoja, hakuna hata miongoni mwao ambaye anaweza kutoa ushauri mzuri, nani, lini nimulize, awezaye kunijibu neno.
And I see that there is no man, Indeed, of these that there is no counselor, And I ask them, and they return word:
29 Tazama, matendo yao si kitu; sanamu zao za chuma zilizotupwa ni upepo na utupu.
“Behold, all of them [are] vanity, Their works [are] nothing, Their molten images [are] wind and emptiness!”