< Isaya 39 >
1 Katika mda ule Merodaki mtoto wa Baladani, mfalme wa Babeli, alituma zawadi na barua kwa Hezekia; maana alisikia Hezekia alikuwa anaumwa na amepona.
At that time, Merodach-baladan son of Baladan, king of Babylon, sent letters and a present unto Hezekiah, —for he had heard that Hezekiah had been sick, and had recovered.
2 Hezekia alifurahishwa na hivi vitu; alimuonyesha mjumbe nyumba ya ghala la vitu vya thamani- vitu kama fedha, dhahabu, viungo, na mafuta ya thamani, ghala la kuwekea silaha zake, na vitu vyote vilivyopatikana kwenye stoo yake. Hapakuwa na kitu katika nyumba yake, wala ufalme wake wote, Hezekia hakuwaonyesha wao.
And Hezekiah, rejoiced over them, and showed them his house of precious things—the silver and the gold and the spices and the precious ointment and all his armoury—and all that was found among his treasures, —there was nothing, which Hezekiah, did not show them—in his house or in all his dominion.
3 Basi Isaya nabii alikuja kwa mfalme Hezekia na kumuuliza, ''Je watu hawa wamekuambia nini? wametoka wapi?, ''Wamekuja kwangu kutoka mbali nchi ya Babeli.''
Then came Isaiah the prophet, unto King Hezekiah, —and said unto him—What said these men? and whence came they unto thee? And Hezekiah said, From a land far away, came they unto me, from Babylon!
4 Isaya akamuuliza je ni vitu gani walivyoviona katika nyumba yako? Hezekia akajibu, ''Wameona kila kitu katika nyumba nyangu. Hakuna kitu miongoni mwa vitu vyangu vya thamani ambavyo sijawaonyesha.''
And he said, What have they seen in thy house? Then said Hezekiah, —All that is in my house, have they seen, there is nothing which I shewed them not among my treasures.
5 Basi Isaya akamwambia Hezekia, ''Sikiliza neno la Yahwe wa majeshi:
Then said Isaiah unto Hezekiah, —Hear thou the word of Yahweh of hosts:
6 'Tazama siku inakaribia kuja pale kila kitu katika nyumba yako, vitu ambavyo mababu zako wamevihifadhi mbali mpaka mda huu wa sasa Vitapelekwa Babeli. Hakuna kitakachobakizwa, asema Yahwe.
Lo! days are coming, when all that is in thy house, and that which thy fathers have treasured up until this day, shall be carried away unto Babylon, —nothing, shall be left, Saith Yahweh.
7 Na watoto watazaliwa kutoka kwako, ambao wewe mwenyewe utawazaa- watachukuliwa mbali, na watakuwa matoashi katika jumba la mfalme wa Babeli.''
And of thy sons who shall issue from thee whom thou shalt beget, shall they take away, —and they shall become eunuchs in the palace of the king of Babylon.
8 Basi Hezekia akamwambia Isaya, ''Neno la Yahwe alilolizunumza ni zuri.'' Maana alifikiria, ''Patakuwa na amani na utulivu katika siku zangu.''
And Hezekiah said unto Isaiah, Good is the word of Yahweh, which thou hast spoken. And he said, Surely, there shall be peace and stability in my days.