< Isaya 39 >

1 Katika mda ule Merodaki mtoto wa Baladani, mfalme wa Babeli, alituma zawadi na barua kwa Hezekia; maana alisikia Hezekia alikuwa anaumwa na amepona.
At that time Merodach Baladan, the son of Baladan, king of Babylon, sent a letter and a present to Hezekiah, for he had heard that he had been sick and was recovered.
2 Hezekia alifurahishwa na hivi vitu; alimuonyesha mjumbe nyumba ya ghala la vitu vya thamani- vitu kama fedha, dhahabu, viungo, na mafuta ya thamani, ghala la kuwekea silaha zake, na vitu vyote vilivyopatikana kwenye stoo yake. Hapakuwa na kitu katika nyumba yake, wala ufalme wake wote, Hezekia hakuwaonyesha wao.
And Hezekiah was delighted with them, and showed the embassy his treasure-house, the silver, and the gold, and the spices, and the precious oil, and his whole armory, and all that was found in his treasures. There was nothing in his house, nor in all his dominion, which Hezekiah did not show them.
3 Basi Isaya nabii alikuja kwa mfalme Hezekia na kumuuliza, ''Je watu hawa wamekuambia nini? wametoka wapi?, ''Wamekuja kwangu kutoka mbali nchi ya Babeli.''
Then came Isaiah the prophet to King Hezekiah, and said to him, What did these men say, and whence did they come to thee? And Hezekiah said, They came to me from a distant country, from Babylon.
4 Isaya akamuuliza je ni vitu gani walivyoviona katika nyumba yako? Hezekia akajibu, ''Wameona kila kitu katika nyumba nyangu. Hakuna kitu miongoni mwa vitu vyangu vya thamani ambavyo sijawaonyesha.''
Then said he, What have they seen in thy house? And Hezekiah answered: All that is in my house have they seen. There is nothing in my treasures which I have not shown them.
5 Basi Isaya akamwambia Hezekia, ''Sikiliza neno la Yahwe wa majeshi:
Then said Isaiah to Hezekiah, hear the word of Jehovah of hosts,
6 'Tazama siku inakaribia kuja pale kila kitu katika nyumba yako, vitu ambavyo mababu zako wamevihifadhi mbali mpaka mda huu wa sasa Vitapelekwa Babeli. Hakuna kitakachobakizwa, asema Yahwe.
Behold, the days shall come, when all that is in thy house, and that thy fathers have treasured up to this day, shall be carried away to Babylon. Nothing shall be left, saith Jehovah.
7 Na watoto watazaliwa kutoka kwako, ambao wewe mwenyewe utawazaa- watachukuliwa mbali, na watakuwa matoashi katika jumba la mfalme wa Babeli.''
And of thy sons, which shall issue from thee, which thou shalt beget, shall they take away, and they shall he eunuchs in the palace of the king of Babylon.
8 Basi Hezekia akamwambia Isaya, ''Neno la Yahwe alilolizunumza ni zuri.'' Maana alifikiria, ''Patakuwa na amani na utulivu katika siku zangu.''
Then said Hezekiah to Isaiah, Good is the word of Jehovah, which thou hast spoken. For, said he, there shall be peace and security in my days.

< Isaya 39 >