< Isaya 38 >
1 Siku zile Hezekia alikuwa anaumwa karibia na kufa. Hivyo Isaya mtoto wa Amozi, nabii alikuja kwake na kumwambia, ''Yahwe amesema, 'panga mambo yako maana utakufa, hautaishi.'
In those days Hezekiah was sick to death. And Isaiah the prophet the son of Amoz came to him, and said to him, Thus says Jehovah, Set thy house in order, for thou shall die, and not live.
2 'Halafu Hezekia akaugeukia ukuta na akamuomba Yahwe.
Then Hezekiah turned his face to the wall, and prayed to Jehovah,
3 Na akasema, ''samahani Yahwe, kumbuka jinsi nilivyoenenda kwa uaminifu mbele zako kwa moyo wangu wote, na jinsi nilivyofanya matendo mema katika macho yako.'' Na Hezekia akalia kwa sauti.
and said, Remember now, O Jehovah, I beseech thee, how I have walked before thee in truth and with a perfect heart, and have done that which is good in thy sight. And Hezekiah wept greatly.
4 Basi neno la Yawe likamjia Isaya, na kusema,
Then the word of Jehovah came to Isaiah, saying,
5 ''Nenda ukamwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, ''Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Daudi babu yenu, amesema: Nimeyasikiliza maombi yako, na nimeyaona machozi yako. Ona ninakaribia kuongeza miaka kumi na tano katika maisha yako.
Go, and say to Hezekiah, Thus says Jehovah, the God of David thy father. I have heard thy prayer. I have seen thy tears. Behold, I will add to thy days fifteen years.
6 Na nitakukomboa wewe pamoja mji huu kutoka kwenye mkono wamfalme wa Asiria, na nitaulinda huu mji.
And I will deliver thee and this city out of the hand of the king of Assyria, and I will defend this city.
7 Na hii itakuwa alama kwako kutoka kwangu, Yahwe, kwamba nitafanya nilichokisema:
And this shall be the sign to thee from Jehovah, that Jehovah will do this thing that he has spoken:
8 Angalia, nitasababisha kimvuli katika nyumba ya Ahazi kwenda nyuma hautua kumi.'' hivvyo basi kivuli kilirudi nyuma hatua kumi juu ya nyumba iliyopanda juu.
Behold, I will cause the shadow on the steps, which has gone down on the dial of Ahaz with the sun, to return backward ten steps. So the sun returned ten steps on the dial on which it had gone down.
9 Haya ndiyo maandishi ya maombi ya Hezekia mfalme wa Yuda, alipokuwa anaumwa halafu akapona:
The writing of Hezekiah king of Judah when he had been sick, and was recovered of his sickness:
10 ''Nimesema kwamba nusu ya maisha yangu nitapita katika mlango wa kuzimu; Nilitumwa pale miaka yangu yote. (Sheol )
I said, In the noontide of my days I shall go into the gates of Sheol. I am deprived of the residue of my years. (Sheol )
11 Nikasema sitamuona tena Yahwe, Yahwe kaika nchi ninayoishi; sitaangalia watu tena au wenyeji wa dunia hii.
I said, I shall not see Jehovah, even Jehovah in the land of the living. I shall behold man no more with the inhabitants of the world.
12 Maisha yangu yameondolea na kupelekwa mbali na mimi kama hema la mchungaji; Niliyakunja maisha yangu juu kama mfumaji; ameniondoa katika kifungo; kati ya mchana na usiku ameyakomesha maisha yangu.
My dwelling is removed, and is carried away from me as a shepherd's tent. I have rolled up, like a weaver, my life. He will cut me off from the loom. From day even to night thou will make an end of me.
13 Nililia mpaka asubuhi; kama simba anaivunja mifupa yangu. Kati ya usiku na mchana ameyakomesha maisha yangu.
I quieted myself until morning. As a lion, so he breaks all my bones. From day even to night will thou make an end of me.
14 Kama mbayuwayu ndivyo nilivyolia; nililia kama njiwa; macho yangu yalichoka kuangalia juu. Bwana ninateseka; nisaidie mimi.
Like a swallow or a crane, so I chattered. I moaned as a dove. My eyes fail with looking upward. O Lord, I am oppressed, be thou my surety.
15 Niseme nini? wote wameongea na mimi na amefanya hivyo; Nitatembea taratibu miaka yangu yote maana ninayashinda kwa huzuni.
What shall I say? He has both spoken to me, and himself has done it. I shall go softly all my years because of the bitterness of my soul.
16 Bwana, mateso uliyoyatuma ni mazuri kwangu; ikiwezekana nirudishiwe tena maisha yangu; umeyahifadhi maisha maisha yangu na afya yangu.
O Lord, by these things men live, and wholly therein is the life of my spirit. Therefore recover thou me, and make me to live.
17 Ni kwa faida yangu kwamba nimwpitia huzuni kama hii. Umenikomboa kutoka kwenye shimo la uharibifu; maana umetupa dhambi zangu nyuma yako.
Behold, for peace I had great bitterness. But thou have by love for my soul delivered it from the pit of corruption. For thou have cast all my sins behind thy back.
18 Maana kuzimu hapata kushukuru wewe; kifo hakikusifu wewe; wale wote waendao ndani ya shimo hawana matumaini ya uaminifu wako. (Sheol )
For Sheol cannot praise thee, death cannot celebrate thee. Those who go down into the pit cannot hope for thy truth. (Sheol )
19 Mtu anayeishi, mtu anayeishi, ndiye anayekushukuru wewe, kama ninavyofanya leo; baba atawjulisha watoto uaminifu wako.
The living, the living, he shall praise thee, as I do this day. The father to the sons shall make known thy truth.
20 Yahwe anakarbia kunikomboa mimi, na tutasherekea kwa mziki siku zote za maisha yetu katika nyumba ya Yahwe.''
Jehovah is ready to save me. Therefore we will sing my songs with stringed instruments all the days of our life in the house of Jehovah.
21 Sasa Isaya alisema, ''Waacheni wachukue donge mitini na kuliweka kweye jipu naye atapona.
Now Isaiah had said, Let them take a cake of figs, and lay it for a plaster upon the boil, and he shall recover.
22 ''Hezekia pia alisema, ''Je ni ishara gan ya kwamba nitaiende juu katika nyumba ya Yahwe?''
Hezekiah also had said, What is the sign that I shall go up to the house of Jehovah?