< Isaya 37 >

1 Ikawa siku hiyo mfalme Hezekia aliposika taarifa zao, alichana mavazi yake, na kujifunika nguo za magunia, na akaenda kwenye nyumba ya Yahwe.
Lorsque le roi Ézéchias les eut ouïs, il déchira ses vêtements, se couvrit d'un cilice, et alla au temple du Seigneur.
2 Na alimtuma Eliakimu, ambae ni kiongozi wa kaya na Shebna mwandishi, na wazee wa makuhani, wote walijifunika nguo za magunia, kwa Isaya mtoto wa Amozi, nabii.
Et il envoya, couverts de cilices, l'économe Éliacim, et le scribe Somna, et les anciens des prêtres, auprès du prophète Isaïe, fils d'Amos.
3 Wakamwambia yeye, Hezekia akasema hivi, 'Siku hii ni siku ya dhiki, kukemewa, na aibu, ni kama mtoto aliye tayari kuzaliwa lakini mama yake hana nguvu za kumsukuma mtoto.
Et ils lui dirent: Voici ce que dit Ézéchias: Ce jour est un jour d'affliction et d'opprobre, de reproches et de colère; car les douleurs de l'enfantement sont venues à la femme, mais elle n'a pas la force d'enfanter.
4 Itakuwa Yahwe Mungu wenu atasikia maneno ya kamanda mkuu, ambao mfalme wa Asira Bwana wake alimtuma kumpinga Mungu anayeishi, na atakemea maneno ambayo Yahwe Mungu wenu ameyasikia. Sasa inueni maombi yenu juu mabaki yaliyoobakia hapa.''
Puisse le Seigneur ton Dieu entendre les paroles de Rabsacès, que le roi des Assyriens a envoyé pour outrager le Dieu vivant et le blasphémer par les paroles que le Seigneur ton Dieu a entendues; et prie le Seigneur ton Dieu pour ce qui reste encore des siens.
5 Sasa watumishi wa mfalme Hezekia walikuja kwa Isaya,
Et les serviteurs du roi Ézéchias vinrent auprès d'Isaïe;
6 na Isaya akawambia, ''Mwambieni Bwana wenu: 'Yahwe amesma, ''Msiogope kwa maneno mliyoyasikia, maneno ambayo mfalme wa Asiria amenitusi mimi.
Et le prophète leur dit: Dites à votre maître: Voici ce que dit le Seigneur: Ne crains pas les paroles de blasphème que tu as entendues des envoyés du roi des Assyriens.
7 Tazama nitaiweka roho yangu ndani yake na atasikiliiza taarifa fulani na atarudi kwenye nchi yake mwenyewe. Na nitamfanya anguke kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.''
Voilà que je mets en lui un esprit; il va apprendre une nouvelle, et il retournera en son royaume, et il périra par le glaive en son royaume.
8 Basi kamanda mkuu alirudi na kumkuta mfalme wa Asira anapigana dhidi ya Libna, Maana aliskia kwamba mfalme amekwenda mbali kutoka Lachishi.
Et Rabsacès s'en retourna, et il rejoignit le roi des Assyriens qui assiégeait Lobna, et il avait oui dire qu'il était parti de Lachis.
9 Halafu Sennacheribi alisikia kwamba Tirkhaka mfalme wa Ethiopia na Misri wamehamasishana kupigna dhidi yake. Hivyo akamtuma mjumbe mara nyingine kwa Hezekia apeleke ujumbe:
Et Tharaca, roi d'Éthiopie, se mit en campagne pour le combattre; et l'ayant su, il partit, et il envoya des messagers à Ézéchias, disant:
10 ''Mwambie Hezekia, mfalme wa Yuda, 'Usimruhusu Mungu unayemwamini akudanganye, ''Yerusalemu haitatiwa mikononi mwa mfalme wa Asiria.''
Voici ce que vous direz à Ézéchias, roi de la Judée: Que ton Dieu, en qui tu as mis ta confiance, ne te trompe pas, en te disant: Jérusalem ne sera pas livrée au roi des Assyriens.
11 umesikia kitu ambacho mfalme wa Asiria alichokifanya kwa nchi yote kwa kuiangamiza kabisa. Je utawaokoa?
Ne sais-tu pas de quelle manière les rois des Assyriens ont traité toutes les contrées qu'ils ont détruites? Et toi, tu leur échapperais!
12 Je miungu ya mataifa imewakomboa? taifa ambalo baba yangu aliliangamiza: Gozani, Harani, Rezefi na watu wa Edeni katika Telassari?
Est-ce que les dieux des nations, que nos pères ont anéanties, les ont sauvés? ont-ils sauvé Gozan, Harran et Rapheth, qui sont dans la terre de Théémath?
13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa miji ya Sefarvaaimi, wa Hema na Ivva?''
Où sont les rois d'Émath? Où sont ceux d'Arphath et de la ville d'Eppharvam, et d'Anagougana?
14 Hezekia alipokea barua hii kutoka mikononi mwa mjumbe na kisoma. Halafu akaenda juu kwenye nyumba ya Yahwe na kuusoma mbele yake.
Et Ézéchias prit la lettre de Sennachérib des mains des messagers, et il l'ouvrit devant le Seigneur.
15 Hezekia alimuomba Mungu:
Et Ézéchias pria le Seigneur, disant:
16 Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, wewe ambae uko juu ya makerubi, wewe ni Mungu mwenywe juu falme zote za dunia. umezifanya mbingu na nchi.
Seigneur des armées, Dieu d'Israël, qui êtes assis sur les chérubins, vous êtes le seul Dieu de tous les royaumes de la terre; vous avez créé le ciel et la terre.
17 Jeuza masikio yako, Yahwe, na sikiliza. Fungua macho yako, Ee Yahwe na uone, na usikilize maneno ya Sanacheribi, ambayo ameyatuma kumfanyia mzadha Mungu anayeishi.
Seigneur, inclinez votre oreille; Seigneur, écoutez; Seigneur, ouvrez les yeux, regardez et voyez les paroles que Sennachérib envoie pour outrager le Dieu vivant.
18 Ni kweli Yahwe, mfalme wa Asiria ameangamiza mataifa yote na aridhi yao.
Il est vrai, Seigneur, que les Assyriens ont dépeuplé toute la terre et les contrées des nations,
19 Wameiweka miungu yao katika moto, maana haikuwa miungu lakini kazi ya mikono ya wanadamu, ni kuni na jiwe tu.
Et qu'ils ont jeté au feu leurs idoles; car ce n'étaient pas des dieux, mais des œuvres de la main des hommes, du bois, de la pierre, et ils les ont répudiées.
20 Hivyo Waasira wameawaangamiza wao. hivyo saa Yahwe Mungu wetu, tuokoe kwa nguvu zako, ili falme zote za duniani zijue kwamba wewe ni Yahwe peke yako.''
Maintenant, Seigneur notre Dieu, délivrez-nous des mains de Sennachérib, afin que tout royaume de la terre sache que vous êtes le seul Dieu.
21 Basi Isaya mtoto wa Amozi alituma ujumbe kwa Hezekia, na kusema, Yahwe Mungu wa Israeli amesema, Kwa sababu umeomba kwangu kuhusu Sannacheribi mfalme wa Asiria,
Et Isaie, fils d'Amos, envoya un messager chez Ézéchias, disant: Voici ce que dit le Seigneur Dieu d'Israël J'ai entendu la prière que tu m'as faite au sujet de Sennachérib, roi des Assyriens;
22 Haya ndiyo maneno ambayo Yahwe amezungumza kuhusu yeye, ''Binti bikira wa Sayuni wanakudharau na kukucheka kwa dharau; mabinti wa Yerusalemu wanatingisha vichwa vyao kwa ajili yako.
Or voici les paroles que Dieu a dites sur lui: il t'a méprisée, ô vierge, fille de Sion, il t'a raillée; il a secoué la tête sur toi, fille de Jérusalem.
23 Ni nani unayempinga na kumtusi? na dhidi ya nani unayenyanyua sauti yako na kunyanyua macho yako kwa kiburi? dhidi ya mtakatifu wa Israeli.
Qui as-tu outragé et irrité? Contre qui as-tu élevé la voix? N'as-tu pas levé tes regards hautains contre le Saint d'Israël?
24 Kwa kupitia watumishi wako umempinga Bwana na amesema, 'Kwa wingi wa gari nimepanda juu kwenye kilele cha milima, katika kilele cha mwuinuko wa Lebanoni. Nitaikata mierezi yake na kuchagua miti ya miseprasi pale, ni msitu uzao sana.
Tu as outragé le Seigneur par tes messagers, et tu as dit: Avec la multitude de mes chars je suis monté sur la cime des montagnes et sur les pics du Liban; j'ai abattu ses grands cèdres et ses plus beaux cyprès, et je suis venu au plus haut de la forêt de chênes.
25 Nimechimba kisima na kunywa maji; nimechimba mito yote ya Misri chini ya nyayo za miguu yangu.'
Et j'ai fait une digue, et j'ai desséché les eaux et tous les rassemblements d'eau.
26 Je haujasikia jinsi nilivyoamua toka siku nyingi na nimelifanyia kazi toka kipindi cha kale? ninayaleta sasa ili yaweze kutimia. Mko hapa kuhiaribu miji imara na yenye ulinzi wa kutosha na kuwa chungu cha uharibifu.
N'as-tu pas ouï parler des choses que j'ai faites jadis? Dès les anciens jours je les ai ordonnées; et aujourd'hui j'ai montré mon dessein de désoler des nations dans leurs forteresses et les habitants des villes fortes.
27 Wakazi wake, waliowadhaifu, waliokata tamaa na wenye aibu. Wanaotesha shambani, majani mabichi, majani juu paa au kwenye shamba kabla ya upepo wa mashariki.
J'ai énervé leurs mains, et ils se sont flétris, ils sont devenus comme le gazon des terrasses.
28 Lakini najua kukaa kwenu chini, kutoka kwenu nje, mnapoingia ndani, na mnapokuwa wakali dhidi yangu.
Et maintenant je connais ta demeure, ton départ et ton arrivée.
29 Kwa sababu mnakuwa wakali dhidi yangu, maana kiburi chenu kimeyafikia masikio yangu, Nitaweka ndoano katika pua zenu, na sauti katika midomo yenu; Nitawageuza nyuma kwenye njia mliyokuja nayo.
Ta fureur, tes paroles superbes sont parvenues jusqu'à moi; mais je mettrai un harpon dans tes narines et un mors à tes lèvres, et je te renverrai par le chemin que tu as pris en venant.
30 Hii itakuwa wimbo kwenu: mwaka huu mtakula kinachoota porini na mwaka pili mtakula kinachoota hapo hapo. Lakini mwaka wa tatu lazima mpande na mvune, pandeni mizabibu na mle matunda yake.
Pour toi, Ezéchias, voici mon signe: Mange cette année ce que tu auras semé, et la seconde année, les restes; mais, la troisième année, semez et moissonnez; plantez vos vignes, et vous en mangerez les fruits.
31 Mabaki ya nyumba ya Yuda ambao wanaishi watachukua mzizi tena na kuzalisha matunda.
Et ceux qui seront restés en Judée enfonceront leurs racines dans le sol, et produiront des fruits jusqu'au haut des branches.
32 Maana katika Yerusalemu waliobaki watatoka; Kutoka kwenye mlima Sayuni waliobaki watakuja. Bidii ya Yahwe wa majeshi itafanikisha hili.''
Car il sortira de Jérusalem des restes, et de la montagne de Sion des hommes sauvés. Et c'est l'amour du Seigneur des armées qui fera ces choses.
33 Hivyo basi Yahwe asema hivi kuhusu Asiria: ''Atakuja katika miji, wala kurusha mkuki hapa. Wala atakuja hapa mbele kwa ngao au kujenga uzio njia panda dhidi yao.
A cause de cela, voici ce que dit le Seigneur sur le roi des Assyriens: Il n'entrera point en cette ville; il ne lancera pas contre elle une flèche; il ne poussera pas contre elle un bouclier; il ne l'entourera point de palissades.
34 Njia atakayojia itakuwa njia hiyo hiyo atakayorudia; ataingia katika mji huu. Hili ni Tamko ya Yahwe.
Il s'en retournera par le chemin qu'il a pris, et il n'entrera point en cette ville: voilà ce que dit le Seigneur.
35 Maana nitaulinda huu mji na kuuokoa, kwa niaba yangu mimi mwenyewe na kwa niaba Daudi mtumishi wangu.''
J'étendrai mon bouclier sur cette ville pour la sauver à cause de moi, et à cause de David, mon serviteur.
36 Halafu malaika wa Yahwe alienda nje na kuvamia kambi ya Waasiria, na kuwauwa askari 185, 000. Watu walipoamka asubuhi na mapema, miili iliyokufa imelala kila mahali.
Et l'ange du Seigneur s'avança, et il extermina dans le camp des Assyriens cent quatre-vingt-cinq mille hommes; et les survivants se levèrent dès l'aurore, et ils ne trouvèrent que des cadavres.
37 Hivyo Sennacheribi mfalme wa Asiria aliiacha Israeli na kwenda nyumbani na akakaa Ninewi.
Et Sennachérib, roi des Assyriens, partit et il s'en retourna, et il ne sortit plus de Ninive.
38 Baadaye, na alipokuwa anabudu katika nyumba ya Nisrochi mungu wake, mtoto wake Adramaleki na Shareza alimuua kwa upanga. Halafu wakakimbilia kwenye nchi ya Ararati. Halafu Esarhadoni mtoto wake akatawala katika sehemu ya baba yake.
Et comme il adorait, dans le temple de Nasarach, le premier de ses dieux, ses fils Adramélech et Sarasar le tuèrent de leurs épées; puis ils se sauvèrent en Arménie, et Asordan, son fils, régna à sa place.

< Isaya 37 >