< Isaya 37 >

1 Ikawa siku hiyo mfalme Hezekia aliposika taarifa zao, alichana mavazi yake, na kujifunika nguo za magunia, na akaenda kwenye nyumba ya Yahwe.
And it came to pass, when king Hezekiah heard it, that he rent his clothes, and covered himself with sackcloth, and went into the house of the Lord.
2 Na alimtuma Eliakimu, ambae ni kiongozi wa kaya na Shebna mwandishi, na wazee wa makuhani, wote walijifunika nguo za magunia, kwa Isaya mtoto wa Amozi, nabii.
And he sent Elyakim, who was superintendent over the house, and Shebna the scribe, and the elders of the priests, covered with sackcloth, to Isaiah the son of Amoz, the prophet.
3 Wakamwambia yeye, Hezekia akasema hivi, 'Siku hii ni siku ya dhiki, kukemewa, na aibu, ni kama mtoto aliye tayari kuzaliwa lakini mama yake hana nguvu za kumsukuma mtoto.
And they said unto him, Thus hath said Hezekiah, A day of trouble, and of rebuke, and of derision is this day; for the children are come to the birth, and there is not strength to bring forth.
4 Itakuwa Yahwe Mungu wenu atasikia maneno ya kamanda mkuu, ambao mfalme wa Asira Bwana wake alimtuma kumpinga Mungu anayeishi, na atakemea maneno ambayo Yahwe Mungu wenu ameyasikia. Sasa inueni maombi yenu juu mabaki yaliyoobakia hapa.''
Perhaps the Lord thy God will hear the words of Rabshakeh, whom the king of Assyria his master hath sent to blaspheme the living God, and who hath reproached with the words which the Lord thy God hath heard: wherefore lift up a prayer for the remnant that is still found here.
5 Sasa watumishi wa mfalme Hezekia walikuja kwa Isaya,
And the servants of king Hezekiah came to Isaiah.
6 na Isaya akawambia, ''Mwambieni Bwana wenu: 'Yahwe amesma, ''Msiogope kwa maneno mliyoyasikia, maneno ambayo mfalme wa Asiria amenitusi mimi.
And Isaiah said unto them, Thus shall ye say unto your master, Thus hath said the Lord, Be not afraid because of the words which thou hast heard, with which the boys of the king of Assyria have blasphemed me.
7 Tazama nitaiweka roho yangu ndani yake na atasikiliiza taarifa fulani na atarudi kwenye nchi yake mwenyewe. Na nitamfanya anguke kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.''
Behold, I will put an [other] spirit in him, and when he will hear a rumor, he shall return to his own land; and I will cause him to fall by the sword in his own land.
8 Basi kamanda mkuu alirudi na kumkuta mfalme wa Asira anapigana dhidi ya Libna, Maana aliskia kwamba mfalme amekwenda mbali kutoka Lachishi.
And Rabshakeh returned, and found the king of Assyria warring against Libnah; for he had heard that he was departed from Lachish.
9 Halafu Sennacheribi alisikia kwamba Tirkhaka mfalme wa Ethiopia na Misri wamehamasishana kupigna dhidi yake. Hivyo akamtuma mjumbe mara nyingine kwa Hezekia apeleke ujumbe:
And he heard it said of Thirhakah the king of Ethiopia, He is come out to fight with thee. And when he had heard it, he sent messengers to Hezekiah, saying,
10 ''Mwambie Hezekia, mfalme wa Yuda, 'Usimruhusu Mungu unayemwamini akudanganye, ''Yerusalemu haitatiwa mikononi mwa mfalme wa Asiria.''
Thus shall ye say to Hezekiah the king of Judah, as followeth, Let not thy God, in whom thou trustest, deceive thee, saying, Jerusalem shall not be given up into the hand of the king of Assyria.
11 umesikia kitu ambacho mfalme wa Asiria alichokifanya kwa nchi yote kwa kuiangamiza kabisa. Je utawaokoa?
Behold, thou thyself hast heard what the kings of Assyria have done to all the lands by destroying them utterly: and thou alone shouldst be delivered?
12 Je miungu ya mataifa imewakomboa? taifa ambalo baba yangu aliliangamiza: Gozani, Harani, Rezefi na watu wa Edeni katika Telassari?
Have the gods of the nations which my fathers destroyed delivered them, as Gozan, and Charan, and Rezeph, and the children of 'Eden, who were in Thelassar?
13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa miji ya Sefarvaaimi, wa Hema na Ivva?''
Where is the king of Chamath, and the king of Arpad, and the king of the city of Sepharvayim, of Hena', and 'Ivvah?
14 Hezekia alipokea barua hii kutoka mikononi mwa mjumbe na kisoma. Halafu akaenda juu kwenye nyumba ya Yahwe na kuusoma mbele yake.
And Hezekiah took the letter out of the hand of the messengers, and read it: and Hezekiah went up unto the house of the Lord, and spread it out before the Lord.
15 Hezekia alimuomba Mungu:
And Hezekiah prayed unto the Lord, saying,
16 Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, wewe ambae uko juu ya makerubi, wewe ni Mungu mwenywe juu falme zote za dunia. umezifanya mbingu na nchi.
O Lord of hosts, the God of Israel, who dwellest between the cherubim, thou art the [true] God, thou alone, for all the kingdoms of the earth; [for] it is thou who hast made the heavens and earth.
17 Jeuza masikio yako, Yahwe, na sikiliza. Fungua macho yako, Ee Yahwe na uone, na usikilize maneno ya Sanacheribi, ambayo ameyatuma kumfanyia mzadha Mungu anayeishi.
Bend down, O Lord, thy ear, and hear; open, O Lord, thy eye, and see: and hear all the words of Sennacherib, which he hath sent to blaspheme the living God.
18 Ni kweli Yahwe, mfalme wa Asiria ameangamiza mataifa yote na aridhi yao.
Truly, Lord, the kings of Assyria have devastated all the nations, and their land;
19 Wameiweka miungu yao katika moto, maana haikuwa miungu lakini kazi ya mikono ya wanadamu, ni kuni na jiwe tu.
And they have placed their gods into the fire; for they are no gods, but the work of man's hands, wood and stone; and these have they destroyed.
20 Hivyo Waasira wameawaangamiza wao. hivyo saa Yahwe Mungu wetu, tuokoe kwa nguvu zako, ili falme zote za duniani zijue kwamba wewe ni Yahwe peke yako.''
And now, O Lord our God, save us out of his hand, that all the kingdoms of the earth may know that thou art the Lord, thou alone.
21 Basi Isaya mtoto wa Amozi alituma ujumbe kwa Hezekia, na kusema, Yahwe Mungu wa Israeli amesema, Kwa sababu umeomba kwangu kuhusu Sannacheribi mfalme wa Asiria,
Then sent Isaiah the son of Amoz unto Hezekiah, saying, Thus hath said the Lord the God of Israel, Whereas thou hast prayed to me concerning Sennacherib the king of Assyria:
22 Haya ndiyo maneno ambayo Yahwe amezungumza kuhusu yeye, ''Binti bikira wa Sayuni wanakudharau na kukucheka kwa dharau; mabinti wa Yerusalemu wanatingisha vichwa vyao kwa ajili yako.
This is the word that the Lord hath spoken over him: She despiseth thee, she laugheth thee to scorn, the virgin daughter of Zion; behind she shaketh her head, the daughter of Jerusalem.
23 Ni nani unayempinga na kumtusi? na dhidi ya nani unayenyanyua sauti yako na kunyanyua macho yako kwa kiburi? dhidi ya mtakatifu wa Israeli.
Whom hast thou blasphemed, and [whom] hast thou scorned? and against whom hast thou raised thy voice, and lifted up thy eyes on high? against the Holy One of Israel.
24 Kwa kupitia watumishi wako umempinga Bwana na amesema, 'Kwa wingi wa gari nimepanda juu kwenye kilele cha milima, katika kilele cha mwuinuko wa Lebanoni. Nitaikata mierezi yake na kuchagua miti ya miseprasi pale, ni msitu uzao sana.
Through thy servants hast thou blasphemed the Lord, and hast said, With the multitude of my chariots am I indeed come up to the height of the mountains, to the sides of Lebanon; and I will cut down its tall cedars, the choice of its fir-trees: and I will enter into the height of its summit, the forest of its fruitful soil.
25 Nimechimba kisima na kunywa maji; nimechimba mito yote ya Misri chini ya nyayo za miguu yangu.'
I have dug, and drunk water; and I will dry up with the sole of my feet all the streams of besieged places.
26 Je haujasikia jinsi nilivyoamua toka siku nyingi na nimelifanyia kazi toka kipindi cha kale? ninayaleta sasa ili yaweze kutimia. Mko hapa kuhiaribu miji imara na yenye ulinzi wa kutosha na kuwa chungu cha uharibifu.
Hadst thou not heard, that in distant ages I had prepared this? in the times of antiquity when I formed it? now have I brought it along, and it came to pass to desolate into ruinous heaps fortified cities.
27 Wakazi wake, waliowadhaifu, waliokata tamaa na wenye aibu. Wanaotesha shambani, majani mabichi, majani juu paa au kwenye shamba kabla ya upepo wa mashariki.
And thus their inhabitants were of short power, they were discouraged and confounded: they were as the herbs of the field, and as the green grass; as the moss on the housetops, and as corn blasted before the ear appeareth.
28 Lakini najua kukaa kwenu chini, kutoka kwenu nje, mnapoingia ndani, na mnapokuwa wakali dhidi yangu.
But thy abiding, and thy going out, and thy coming in do I know, and thy raging against me.
29 Kwa sababu mnakuwa wakali dhidi yangu, maana kiburi chenu kimeyafikia masikio yangu, Nitaweka ndoano katika pua zenu, na sauti katika midomo yenu; Nitawageuza nyuma kwenye njia mliyokuja nayo.
Because of thy raging against me, and thy tumult, that is come up into my ears, will I put my hook in thy nose, and my bridle between thy lips, and I will cause thee to turn back on the way by which thou camest.
30 Hii itakuwa wimbo kwenu: mwaka huu mtakula kinachoota porini na mwaka pili mtakula kinachoota hapo hapo. Lakini mwaka wa tatu lazima mpande na mvune, pandeni mizabibu na mle matunda yake.
And this shall be unto thee the sign, Ye shall eat this year what groweth of itself, and in the second year what springeth after the same; and in the third year sow, and reap, and plant vineyards, and eat their fruit.
31 Mabaki ya nyumba ya Yuda ambao wanaishi watachukua mzizi tena na kuzalisha matunda.
And the remnant of the house of Judah that is escaped shall yet strike root downward, and bear fruit upward.
32 Maana katika Yerusalemu waliobaki watatoka; Kutoka kwenye mlima Sayuni waliobaki watakuja. Bidii ya Yahwe wa majeshi itafanikisha hili.''
For out of Jerusalem shall go forth a remnant, and that which escapeth out of Mount Zion: the zeal of the Lord of hosts will do this.
33 Hivyo basi Yahwe asema hivi kuhusu Asiria: ''Atakuja katika miji, wala kurusha mkuki hapa. Wala atakuja hapa mbele kwa ngao au kujenga uzio njia panda dhidi yao.
Therefore thus hath said the Lord concerning the king of Assyria, He shall not come into this city, and he shall not shoot an arrow thereon, nor come before it with shields, nor cast up an embankment against it.
34 Njia atakayojia itakuwa njia hiyo hiyo atakayorudia; ataingia katika mji huu. Hili ni Tamko ya Yahwe.
On the way by which he came, by the same shall he return, and into this city shall he not come, saith the Lord.
35 Maana nitaulinda huu mji na kuuokoa, kwa niaba yangu mimi mwenyewe na kwa niaba Daudi mtumishi wangu.''
And I will shield this city to save it for my own sake, and for the sake of David my servant.
36 Halafu malaika wa Yahwe alienda nje na kuvamia kambi ya Waasiria, na kuwauwa askari 185, 000. Watu walipoamka asubuhi na mapema, miili iliyokufa imelala kila mahali.
Then went out an angel of the Lord, and smote in the camp of the Assyrians one hundred and eighty and five thousand men; and when people arose early in the morning, behold, they were all dead corpses.
37 Hivyo Sennacheribi mfalme wa Asiria aliiacha Israeli na kwenda nyumbani na akakaa Ninewi.
And Sennacherib the king of Assyria departed, and went and returned, and dwelt at Nineveh.
38 Baadaye, na alipokuwa anabudu katika nyumba ya Nisrochi mungu wake, mtoto wake Adramaleki na Shareza alimuua kwa upanga. Halafu wakakimbilia kwenye nchi ya Ararati. Halafu Esarhadoni mtoto wake akatawala katika sehemu ya baba yake.
And it came to pass, as he was prostrating himself in the house of Nisroch his god, that Adrammelech and Sharezer his sons smote him with the sword; and they escaped into the land of Ararat. And Essar-chaddon his son became king in his stead.

< Isaya 37 >