< Isaya 37 >

1 Ikawa siku hiyo mfalme Hezekia aliposika taarifa zao, alichana mavazi yake, na kujifunika nguo za magunia, na akaenda kwenye nyumba ya Yahwe.
And when the King Hezekiah heard it, he rent his clothes, and put on sackcloth and came into the House of the Lord.
2 Na alimtuma Eliakimu, ambae ni kiongozi wa kaya na Shebna mwandishi, na wazee wa makuhani, wote walijifunika nguo za magunia, kwa Isaya mtoto wa Amozi, nabii.
And he sent Eliakim the stewarde of the house, aud Shebna the chanceller, with the Elders of the Priestes, clothed in sackcloth vnto Isaiah the Prophet, the sonne of Amoz.
3 Wakamwambia yeye, Hezekia akasema hivi, 'Siku hii ni siku ya dhiki, kukemewa, na aibu, ni kama mtoto aliye tayari kuzaliwa lakini mama yake hana nguvu za kumsukuma mtoto.
And they sayd vnto him, Thus saith Hezekiah, This day is a day of tribulation and of rebuke and blasphemie: for the children are come to the birth, and there is no strength to bring foorth.
4 Itakuwa Yahwe Mungu wenu atasikia maneno ya kamanda mkuu, ambao mfalme wa Asira Bwana wake alimtuma kumpinga Mungu anayeishi, na atakemea maneno ambayo Yahwe Mungu wenu ameyasikia. Sasa inueni maombi yenu juu mabaki yaliyoobakia hapa.''
If so be the Lord thy God hath heard the wordes of Rabshakeh, whom the King of Asshur his master hath sent to raile on the liuing God, and to reproch him with wordes which the Lord thy God hath heard, then lift thou vp thy prayer for the remnant that are left.
5 Sasa watumishi wa mfalme Hezekia walikuja kwa Isaya,
So the seruants of the King Hezekiah came to Isaiah.
6 na Isaya akawambia, ''Mwambieni Bwana wenu: 'Yahwe amesma, ''Msiogope kwa maneno mliyoyasikia, maneno ambayo mfalme wa Asiria amenitusi mimi.
And Isaiah sayde vnto them, Thus say vnto your master, Thus saith the Lord, Be not afrayd of the wordes that thou hast heard, wherewith the seruants of the king of Asshur haue blasphemed me.
7 Tazama nitaiweka roho yangu ndani yake na atasikiliiza taarifa fulani na atarudi kwenye nchi yake mwenyewe. Na nitamfanya anguke kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.''
Beholde, I wil send a blast vpon him, and he shall heare a noyse, and returne to his owne land, and I will cause him to fall by the sword in his owne land.
8 Basi kamanda mkuu alirudi na kumkuta mfalme wa Asira anapigana dhidi ya Libna, Maana aliskia kwamba mfalme amekwenda mbali kutoka Lachishi.
So Rabshakeh returned, and found the King of Asshur fighting against Libnah: for he had heard that he was departed from Lachish.
9 Halafu Sennacheribi alisikia kwamba Tirkhaka mfalme wa Ethiopia na Misri wamehamasishana kupigna dhidi yake. Hivyo akamtuma mjumbe mara nyingine kwa Hezekia apeleke ujumbe:
He heard also men say of Tirhakah, King of Ethiopia, Beholde, he is come out to fight against thee: and when he heard it, he sent other messengers to Hezekiah, saying,
10 ''Mwambie Hezekia, mfalme wa Yuda, 'Usimruhusu Mungu unayemwamini akudanganye, ''Yerusalemu haitatiwa mikononi mwa mfalme wa Asiria.''
Thus shall ye speake to Hezekiah King of Iudah, saying, Let not thy God deceiue thee, in whom thou trustest, saying, Ierusalem shall not be giuen into the hand of the King of Asshur.
11 umesikia kitu ambacho mfalme wa Asiria alichokifanya kwa nchi yote kwa kuiangamiza kabisa. Je utawaokoa?
Beholde, thou hast heard what the Kings of Asshur haue done to all lands in destroying them, and shalt thou be deliuered?
12 Je miungu ya mataifa imewakomboa? taifa ambalo baba yangu aliliangamiza: Gozani, Harani, Rezefi na watu wa Edeni katika Telassari?
Haue the gods of the nations deliuered them, which my fathers haue destroyed? as Gozan, and Haran, and Rezeph, and the children of Eden, which were at Telassar?
13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa miji ya Sefarvaaimi, wa Hema na Ivva?''
Where is the King of Hamath, and the King of Arpad, and the King of the citie of Sepharuaim, Hena and Iuah?
14 Hezekia alipokea barua hii kutoka mikononi mwa mjumbe na kisoma. Halafu akaenda juu kwenye nyumba ya Yahwe na kuusoma mbele yake.
So Hezekiah receiued the letter of the hand of the messengers and read it, and he went vp into the House of the Lord, and Hezekiah spread it before the Lord.
15 Hezekia alimuomba Mungu:
And Hezekiah prayed vnto the Lord, saying,
16 Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, wewe ambae uko juu ya makerubi, wewe ni Mungu mwenywe juu falme zote za dunia. umezifanya mbingu na nchi.
O Lord of hostes, God of Israel, which dwellest betweene the Cherubims, thou art very God alone ouer all the kingdomes of the earth: thou hast made the heauen and the earth.
17 Jeuza masikio yako, Yahwe, na sikiliza. Fungua macho yako, Ee Yahwe na uone, na usikilize maneno ya Sanacheribi, ambayo ameyatuma kumfanyia mzadha Mungu anayeishi.
Encline thine eare, O Lord, and heare: open thine eyes, O Lord, and see, and heare all the wordes of Saneherib, who hath sent to blaspheme the liuing God.
18 Ni kweli Yahwe, mfalme wa Asiria ameangamiza mataifa yote na aridhi yao.
Trueth it is, O Lord, that the Kings of Asshur haue destroyed all lands, and their countrey,
19 Wameiweka miungu yao katika moto, maana haikuwa miungu lakini kazi ya mikono ya wanadamu, ni kuni na jiwe tu.
And haue cast their gods in ye fire: for they were no gods, but the worke of mans hands, euen wood or stone: therefore they destroyed them.
20 Hivyo Waasira wameawaangamiza wao. hivyo saa Yahwe Mungu wetu, tuokoe kwa nguvu zako, ili falme zote za duniani zijue kwamba wewe ni Yahwe peke yako.''
Nowe therefore, O Lord our God, saue thou vs out of his hand, that all the kingdomes of the earth may knowe, that thou onely art the Lord.
21 Basi Isaya mtoto wa Amozi alituma ujumbe kwa Hezekia, na kusema, Yahwe Mungu wa Israeli amesema, Kwa sababu umeomba kwangu kuhusu Sannacheribi mfalme wa Asiria,
Then Isaiah the sonne of Amoz sent vnto Hezekiah, saying, Thus sayth the Lord God of Israel, Because thou hast prayed vnto me, concerning Saneherib king of Asshur,
22 Haya ndiyo maneno ambayo Yahwe amezungumza kuhusu yeye, ''Binti bikira wa Sayuni wanakudharau na kukucheka kwa dharau; mabinti wa Yerusalemu wanatingisha vichwa vyao kwa ajili yako.
This is the worde that the Lord hath spoken against him, the virgine, the daughter of Zion, hath despised thee, and laughed thee to scorne: the daughter of Ierusalem, hath shaken her head at thee.
23 Ni nani unayempinga na kumtusi? na dhidi ya nani unayenyanyua sauti yako na kunyanyua macho yako kwa kiburi? dhidi ya mtakatifu wa Israeli.
Whome hast thou railed on and blasphemed? and against whome hast thou exalted thy voyce, and lifted vp thine eyes on hie? euen against the holy one of Israel.
24 Kwa kupitia watumishi wako umempinga Bwana na amesema, 'Kwa wingi wa gari nimepanda juu kwenye kilele cha milima, katika kilele cha mwuinuko wa Lebanoni. Nitaikata mierezi yake na kuchagua miti ya miseprasi pale, ni msitu uzao sana.
By thy seruants hast thou railed on the Lord, and sayd, By the multitude of my charets I am come vp to the top of the mountaines to the sides of Lebanon, and will cut downe the hie cedars thereof, and the faire firre trees thereof, and I will goe vp to the heightes of his top and to the forest of his fruitfull places.
25 Nimechimba kisima na kunywa maji; nimechimba mito yote ya Misri chini ya nyayo za miguu yangu.'
I haue digged and drunke the waters, and with the plant of my feete haue I dryed all the riuers closed in.
26 Je haujasikia jinsi nilivyoamua toka siku nyingi na nimelifanyia kazi toka kipindi cha kale? ninayaleta sasa ili yaweze kutimia. Mko hapa kuhiaribu miji imara na yenye ulinzi wa kutosha na kuwa chungu cha uharibifu.
Hast thou not heard howe I haue of olde time made it, and haue formed it long ago? and should I now bring it, that it should be destroyed, and layde on ruinous heapes, as cities defensed?
27 Wakazi wake, waliowadhaifu, waliokata tamaa na wenye aibu. Wanaotesha shambani, majani mabichi, majani juu paa au kwenye shamba kabla ya upepo wa mashariki.
Whose inhabitants haue small power, and are afrayd and confounded: they are like the grasse of the field and greene herbe, or grasse on the house tops, or corne blassed afore it be growen.
28 Lakini najua kukaa kwenu chini, kutoka kwenu nje, mnapoingia ndani, na mnapokuwa wakali dhidi yangu.
But I know thy dwelling, and thy going out, and thy comming in, and thy fury against me.
29 Kwa sababu mnakuwa wakali dhidi yangu, maana kiburi chenu kimeyafikia masikio yangu, Nitaweka ndoano katika pua zenu, na sauti katika midomo yenu; Nitawageuza nyuma kwenye njia mliyokuja nayo.
Because thou ragest against me, and thy tumult is come vnto mine eares, therefore will I put mine hooke in thy nostrels, and my bridle in thy lips, and wil bring thee backe againe the same way thou camest.
30 Hii itakuwa wimbo kwenu: mwaka huu mtakula kinachoota porini na mwaka pili mtakula kinachoota hapo hapo. Lakini mwaka wa tatu lazima mpande na mvune, pandeni mizabibu na mle matunda yake.
And this shalbe a signe vnto thee, O Hezekiah, Thou shalt eate this yeere such as groweth of it selfe: and the second yeere, such things as growe without sowing: and in the third yeere, sowe ye and reape, and plant vineyards, and eate the fruite thereof.
31 Mabaki ya nyumba ya Yuda ambao wanaishi watachukua mzizi tena na kuzalisha matunda.
And the remnant that is escaped of the house of Iudah, shall againe take roote downward and beare fruite vpward.
32 Maana katika Yerusalemu waliobaki watatoka; Kutoka kwenye mlima Sayuni waliobaki watakuja. Bidii ya Yahwe wa majeshi itafanikisha hili.''
For out of Ierusalem shall goe a remnant, and they that escape out of mount Zion: the zeale of the Lord of hostes shall doe this.
33 Hivyo basi Yahwe asema hivi kuhusu Asiria: ''Atakuja katika miji, wala kurusha mkuki hapa. Wala atakuja hapa mbele kwa ngao au kujenga uzio njia panda dhidi yao.
Therefore thus sayth the Lord, concerning the King of Asshur, He shall not enter into this citie, nor shoote an arrow there, nor come before it with shield, nor cast a mount against it.
34 Njia atakayojia itakuwa njia hiyo hiyo atakayorudia; ataingia katika mji huu. Hili ni Tamko ya Yahwe.
By the same way that he came, he shall returne, and not come into this citie, saith the Lord.
35 Maana nitaulinda huu mji na kuuokoa, kwa niaba yangu mimi mwenyewe na kwa niaba Daudi mtumishi wangu.''
For I will defend this citie to saue it, for mine owne sake, and for my seruant Dauids sake.
36 Halafu malaika wa Yahwe alienda nje na kuvamia kambi ya Waasiria, na kuwauwa askari 185, 000. Watu walipoamka asubuhi na mapema, miili iliyokufa imelala kila mahali.
Then the Angel of the Lord went out, and smote in the campe of Asshur an hundreth, fourescore, and fiue thousand: so when they arose early in the morning, beholde, they were all dead corpses.
37 Hivyo Sennacheribi mfalme wa Asiria aliiacha Israeli na kwenda nyumbani na akakaa Ninewi.
So Saneherib king of Asshur departed, and went away and returned and dwelt at Nineueh.
38 Baadaye, na alipokuwa anabudu katika nyumba ya Nisrochi mungu wake, mtoto wake Adramaleki na Shareza alimuua kwa upanga. Halafu wakakimbilia kwenye nchi ya Ararati. Halafu Esarhadoni mtoto wake akatawala katika sehemu ya baba yake.
And as he was in the temple worshipping of Nisroch his god, Adramelech and Sharezer his sonnes slewe him with the sword, and they escaped into the land of Ararat: and Esarhaddon his sonne reigned in his steade.

< Isaya 37 >