< Isaya 37 >

1 Ikawa siku hiyo mfalme Hezekia aliposika taarifa zao, alichana mavazi yake, na kujifunika nguo za magunia, na akaenda kwenye nyumba ya Yahwe.
And it happened that, when king Hezekiah had heard this, he rent his garments, and he wrapped himself in sackcloth, and he entered the house of the Lord.
2 Na alimtuma Eliakimu, ambae ni kiongozi wa kaya na Shebna mwandishi, na wazee wa makuhani, wote walijifunika nguo za magunia, kwa Isaya mtoto wa Amozi, nabii.
And he sent Eliakim, who was over the house, and Shebna, the scribe, and the elders of the priests, covered with sackcloth, to Isaiah, the son of Amoz, the prophet.
3 Wakamwambia yeye, Hezekia akasema hivi, 'Siku hii ni siku ya dhiki, kukemewa, na aibu, ni kama mtoto aliye tayari kuzaliwa lakini mama yake hana nguvu za kumsukuma mtoto.
And they said to him: “Thus says Hezekiah: This day is a day of tribulation, and of rebuke, and of blasphemy. For the sons have arrived at the time for birth, but there is not enough strength to bring them forth.
4 Itakuwa Yahwe Mungu wenu atasikia maneno ya kamanda mkuu, ambao mfalme wa Asira Bwana wake alimtuma kumpinga Mungu anayeishi, na atakemea maneno ambayo Yahwe Mungu wenu ameyasikia. Sasa inueni maombi yenu juu mabaki yaliyoobakia hapa.''
Perhaps, somehow, the Lord your God will hear the words of Rabshakeh, whom the king of the Assyrians, his lord, has sent to blaspheme the living God, and will rebuke the words that the Lord your God has heard. Therefore, lift up your prayers on behalf of the remnant which has been left behind.”
5 Sasa watumishi wa mfalme Hezekia walikuja kwa Isaya,
And so the servants of king Hezekiah went to Isaiah.
6 na Isaya akawambia, ''Mwambieni Bwana wenu: 'Yahwe amesma, ''Msiogope kwa maneno mliyoyasikia, maneno ambayo mfalme wa Asiria amenitusi mimi.
And Isaiah said to them: “You shall say this to your lord: Thus says the Lord: Do not be afraid to face the words that you have heard, by which the servants of the king of the Assyrians blasphemed me.
7 Tazama nitaiweka roho yangu ndani yake na atasikiliiza taarifa fulani na atarudi kwenye nchi yake mwenyewe. Na nitamfanya anguke kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.''
Behold, I will send a spirit to him, and he will hear a message, and he will return to his own land. And I will cause him to fall by the sword, in his own land.”
8 Basi kamanda mkuu alirudi na kumkuta mfalme wa Asira anapigana dhidi ya Libna, Maana aliskia kwamba mfalme amekwenda mbali kutoka Lachishi.
Then Rabshakeh returned, and he found the king of the Assyrians fighting against Libnah. For he had heard that he had set out from Lachish.
9 Halafu Sennacheribi alisikia kwamba Tirkhaka mfalme wa Ethiopia na Misri wamehamasishana kupigna dhidi yake. Hivyo akamtuma mjumbe mara nyingine kwa Hezekia apeleke ujumbe:
And he heard from Tirhakah, the king of Ethiopia: “He has gone forth so that he may fight against you.” And when he had heard this, he sent messengers to Hezekiah, saying:
10 ''Mwambie Hezekia, mfalme wa Yuda, 'Usimruhusu Mungu unayemwamini akudanganye, ''Yerusalemu haitatiwa mikononi mwa mfalme wa Asiria.''
“You shall say this to Hezekiah, the king of Judah, saying: Do not let your God, in whom you trust, deceive you by saying: ‘Jerusalem will not be given into the hands of the king of the Assyrians.’
11 umesikia kitu ambacho mfalme wa Asiria alichokifanya kwa nchi yote kwa kuiangamiza kabisa. Je utawaokoa?
Behold, you have heard about all that the kings of the Assyrians have done to all the lands that they have conquered, and so, how can you be delivered?
12 Je miungu ya mataifa imewakomboa? taifa ambalo baba yangu aliliangamiza: Gozani, Harani, Rezefi na watu wa Edeni katika Telassari?
Have the gods of the nations rescued those whom my fathers have conquered: Gozan, and Haran, and Rezeph, and the sons of Eden who were at Telassar?
13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa miji ya Sefarvaaimi, wa Hema na Ivva?''
Where is the king of Hamath and the king of Arpad, or the king of the city of Sepharvaim, or of Hena and Ivvah?”
14 Hezekia alipokea barua hii kutoka mikononi mwa mjumbe na kisoma. Halafu akaenda juu kwenye nyumba ya Yahwe na kuusoma mbele yake.
And Hezekiah took the letter from the hand of the messengers, and he read it, and he went up to the house of the Lord, and Hezekiah spread it out in the sight of the Lord.
15 Hezekia alimuomba Mungu:
And Hezekiah prayed to the Lord, saying:
16 Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, wewe ambae uko juu ya makerubi, wewe ni Mungu mwenywe juu falme zote za dunia. umezifanya mbingu na nchi.
“O Lord of hosts, the God of Israel who sits upon the Cherubim: you alone are God of all the kingdoms of the earth. You have made heaven and earth.
17 Jeuza masikio yako, Yahwe, na sikiliza. Fungua macho yako, Ee Yahwe na uone, na usikilize maneno ya Sanacheribi, ambayo ameyatuma kumfanyia mzadha Mungu anayeishi.
O Lord, incline your ear and listen. O Lord, open your eyes and see. And hear all the words of Sennacherib, which he has sent to blaspheme the living God.
18 Ni kweli Yahwe, mfalme wa Asiria ameangamiza mataifa yote na aridhi yao.
For truly, O Lord, the kings of the Assyrians have laid waste to countries and territories.
19 Wameiweka miungu yao katika moto, maana haikuwa miungu lakini kazi ya mikono ya wanadamu, ni kuni na jiwe tu.
And they have cast their gods into the fire. For these were not gods, but the works of men’s hands, of wood and of stone. And they broke them into pieces.
20 Hivyo Waasira wameawaangamiza wao. hivyo saa Yahwe Mungu wetu, tuokoe kwa nguvu zako, ili falme zote za duniani zijue kwamba wewe ni Yahwe peke yako.''
And now, O Lord our God, save us from his hand. And let all the kingdoms of the earth acknowledge that you alone are Lord.”
21 Basi Isaya mtoto wa Amozi alituma ujumbe kwa Hezekia, na kusema, Yahwe Mungu wa Israeli amesema, Kwa sababu umeomba kwangu kuhusu Sannacheribi mfalme wa Asiria,
And Isaiah, the son of Amoz, sent to Hezekiah, saying: “Thus says the Lord, the God of Israel: Because of what you have prayed to me about Sennacherib, the king of the Assyrians,
22 Haya ndiyo maneno ambayo Yahwe amezungumza kuhusu yeye, ''Binti bikira wa Sayuni wanakudharau na kukucheka kwa dharau; mabinti wa Yerusalemu wanatingisha vichwa vyao kwa ajili yako.
this is the word that the Lord has spoken over him: The virgin daughter of Zion has despised you and mocked you. The daughter of Jerusalem has shaken her head at you.
23 Ni nani unayempinga na kumtusi? na dhidi ya nani unayenyanyua sauti yako na kunyanyua macho yako kwa kiburi? dhidi ya mtakatifu wa Israeli.
Whom have you insulted? And whom have you blasphemed? And against whom have you lifted up your voice and raised up your eyes on high? Against the Holy One of Israel!
24 Kwa kupitia watumishi wako umempinga Bwana na amesema, 'Kwa wingi wa gari nimepanda juu kwenye kilele cha milima, katika kilele cha mwuinuko wa Lebanoni. Nitaikata mierezi yake na kuchagua miti ya miseprasi pale, ni msitu uzao sana.
By the hand of your servants, you have reproached the Lord. And you have said: ‘With a multitude of my four-horse chariots, I have ascended the heights of the mountains adjoining Lebanon. And I will cut down its lofty cedars and its choice pine trees. And I will reach the top of its summit, to the forest of its Carmel.
25 Nimechimba kisima na kunywa maji; nimechimba mito yote ya Misri chini ya nyayo za miguu yangu.'
I dug deep, and I drank water, and I dried up all the river banks with the sole of my foot.’
26 Je haujasikia jinsi nilivyoamua toka siku nyingi na nimelifanyia kazi toka kipindi cha kale? ninayaleta sasa ili yaweze kutimia. Mko hapa kuhiaribu miji imara na yenye ulinzi wa kutosha na kuwa chungu cha uharibifu.
Have you not heard what I have done to it in past times? In ancient times, I formed it. And now I have brought it forth. And it has been made so that the hills and the fortified cities would fight together, unto its destruction.
27 Wakazi wake, waliowadhaifu, waliokata tamaa na wenye aibu. Wanaotesha shambani, majani mabichi, majani juu paa au kwenye shamba kabla ya upepo wa mashariki.
Their inhabitants had unsteady hands. They trembled and were confused. They became like the plants of the field, and the grass of the pastures, and like the weeds on the rooftops, which wither before they are mature.
28 Lakini najua kukaa kwenu chini, kutoka kwenu nje, mnapoingia ndani, na mnapokuwa wakali dhidi yangu.
I know your habitation, and your arrival, and your departure, and your madness against me.
29 Kwa sababu mnakuwa wakali dhidi yangu, maana kiburi chenu kimeyafikia masikio yangu, Nitaweka ndoano katika pua zenu, na sauti katika midomo yenu; Nitawageuza nyuma kwenye njia mliyokuja nayo.
When you became angry against me, your arrogance rose up to my ears. Therefore, I will place a ring in your nose, and a bit between your lips. And I will turn you back on the road by which you arrived.
30 Hii itakuwa wimbo kwenu: mwaka huu mtakula kinachoota porini na mwaka pili mtakula kinachoota hapo hapo. Lakini mwaka wa tatu lazima mpande na mvune, pandeni mizabibu na mle matunda yake.
But this shall be a sign for you: Eat, in this year, whatever springs up on its own. And in the second year, eat fruits. But in the third year, sow and reap, and plant vineyards, and eat their fruit.
31 Mabaki ya nyumba ya Yuda ambao wanaishi watachukua mzizi tena na kuzalisha matunda.
And what will be saved from the house of Judah, and what is left behind, will form deep roots, and will bear high fruits.
32 Maana katika Yerusalemu waliobaki watatoka; Kutoka kwenye mlima Sayuni waliobaki watakuja. Bidii ya Yahwe wa majeshi itafanikisha hili.''
For from Jerusalem, a remnant shall go forth, and salvation from mount Zion. The zeal of the Lord of hosts will accomplish this.
33 Hivyo basi Yahwe asema hivi kuhusu Asiria: ''Atakuja katika miji, wala kurusha mkuki hapa. Wala atakuja hapa mbele kwa ngao au kujenga uzio njia panda dhidi yao.
For this reason, thus says the Lord about the king of the Assyrians: He will not enter this city, nor shoot an arrow into it, nor overtake it with a shield, nor dig a rampart all around it.
34 Njia atakayojia itakuwa njia hiyo hiyo atakayorudia; ataingia katika mji huu. Hili ni Tamko ya Yahwe.
He will return on the road by which he arrived. And into this city, he will not enter, says the Lord.
35 Maana nitaulinda huu mji na kuuokoa, kwa niaba yangu mimi mwenyewe na kwa niaba Daudi mtumishi wangu.''
And I will protect this city, so that I may save it for my own sake, and for the sake of David, my servant.”
36 Halafu malaika wa Yahwe alienda nje na kuvamia kambi ya Waasiria, na kuwauwa askari 185, 000. Watu walipoamka asubuhi na mapema, miili iliyokufa imelala kila mahali.
Then the Angel of the Lord went forth and struck down, in the camp of the Assyrians, one hundred eighty-five thousand. And they arose in the morning, and behold, all these were dead bodies.
37 Hivyo Sennacheribi mfalme wa Asiria aliiacha Israeli na kwenda nyumbani na akakaa Ninewi.
And Sennacherib, the king of the Assyrians, departed and went away. And he returned and lived at Nineveh.
38 Baadaye, na alipokuwa anabudu katika nyumba ya Nisrochi mungu wake, mtoto wake Adramaleki na Shareza alimuua kwa upanga. Halafu wakakimbilia kwenye nchi ya Ararati. Halafu Esarhadoni mtoto wake akatawala katika sehemu ya baba yake.
And it happened that, as he was adoring his god in the temple of Nisroch, his sons, Adramelech and Sharezer, struck him with the sword. And they fled into the land of Ararat. And Esarhaddon, his son, reigned in his place.

< Isaya 37 >