< Isaya 36 >

1 Katika mwaka wa kumi na nne wa mfalme Hezekia, Senacherebi, mfalme wa Asiria, alivamia miji yote ya Yuda na kuwakamata.
Now in the fourteenth year of king Hezekiah, Sennacherib king of Assyria [Level plain] attacked all of the fortified cities of Judah [Praised], and captured them.
2 Halafu mfalme wa Asiria akamtuma kamanda mkuu na jeshi kubwa kutoka Lachishi mpaka Yerusalemu kwa mfalme Hezekia. Alipofika kwenye mfereji katika kisima cha juu, katika njia kuu na katika shamba la dobi na akasimama pale.
The king of Assyria [Level plain] sent Rabshakeh from Lachish to Jerusalem [City of peace] to king Hezekiah with a large army. He stood by the aqueduct from the upper pool in the fuller’s field highway.
3 Maofisa wa Israeli waliotumwa kuzungumza nao walikuwa ni Eliakimu mtoto wa Hilkia, kiongozi wa jumba, Shebna katibu wa mfalme, na Joa mtoto wa Asapha, anayeandika makubaliano ya serekali.
Then Eliakim the son of Hilkiah, who was over the household, and Shebna the scribe, and Joah, the son of Asaph, the recorder came out to him.
4 Kamanda mkuu wa jeshi akawaambia wao, ''Mwambieni Hezekia kwamba mfalme mkuu, mfalme Asiria, asema, 'Nini chanzo cha ujasiri wako?
Rabshakeh said to them, “Now tell Hezekiah, ‘Thus says the great king, the king of Assyria [Level plain], “What confidence is this in which you trust?
5 Unaongea maneno yasiyo na maana tu, nasema kama kuna shauri na nguvu za vita. Sasa ni nani unayemuamini? na ni nani aliyekupa ujasiri wa kuniasi mimi.
I say that your counsel and strength for the war are only vain words. Now in whom do you trust, that you have rebelled against me?
6 Tazama, umeweka imani yako Misri, maana banzi la mwanzi unalolitumia kama fimbo ya kutembelea, ikiwa mtu ataiegemea na kuishika kwenye mkono wake itamchoma. Hivyo ndovyo jinsi Farao mfalme wa Misri alivyo kwa yeyote anayemuamini.
Behold, you trust in the staff of this bruised reed, even in Egypt [Abode of slavery], which if a man leans on it, it will go into his hand and pierce it. So is Pharaoh king of Egypt [Abode of slavery] to all who trust in him.
7 Lakini ikiwa utasema nami, ''Tunamwamini Yahwe Mungu wetu,''Je sio yeye ambaye Hezekia ameondosha mahali palipoinuka na madhebau, asema kwa Yuda na Yerusalemu, ''Lazima tuabudu mbele ya madhebau hii katika Yerusalemu''?
But if you tell me, ‘We trust in Yahweh Eloheikhem [Yahweh our God],’ is not that he whose high places and whose altars Hezekiah has taken away, and has said to Judah [Praised] and to Jerusalem [City of peace], ‘You shall worship before this altar?’”
8 Hivyo sasa, nataka kukufanya wewe kuwa zawadi nzuri kwa Bwana mfalme Asiria. Nitakupa farasi elfu mbili, kama utaweza kuwatafutia dereva.
Now therefore, please make a pledge to my master the king of Assyria [Level plain], and I will give you two thousand horses, if you are able on your part to set riders on them.
9 Ni kwa jinsi gani unaweza kumpinga moja kati ya nahodha aliye mdogo katika watumishi wa Bwana wangu? Mmeweka imani yenu Misri katika gari na farasi!
How then can you turn away the face of one captain of the least of my master’s servants, and put your trust on Egypt [Abode of slavery] for chariots and for horsemen?
10 Halafu sasa, Je nimewezaje kusafiri mpaka hapa pasipo Yahwe kupigana dhidi ya nchi hii na kuhiaribu? Yahwe asema nami, Vamia nchi hii na uhiharibu.
Have I come up now without Adonai against this land to destroy it? Adonai said to me, “Go up against this land, and destroy it.”’”
11 Halafu Eliakimu mtoto wa Hilkia, na Shebna na Joa asema kwa kamanda mkuu, Tafadhali zungumza na watu wako kwa lugha ya kiashuru, maana kiashuru tunakielewa. Usiongee na sisi kwa lugha kiyahudi katika masikio ya watu ambao wako ukutani.''
Then Eliakim, Shebna and Joah said to Rabshakeh, “Please speak to your servants in Aramaic [Elevated], for we sh'ma ·hear understand obey· it; and don’t speak to us in the Jews’ language in the hearing of the people who are on the wall.”
12 Lakini kamanda mkuu akasema, ''Je bwana wenu ametuma kwa bwana wako na kuzungumza haya maneno? Je hajanituma kwa watu walio kaa kwenye ukuta, ili wale kinyesi chaao mwenyewe na kunywa mkojo waomwenyewe?
But Rabshakeh said, “Has my master sent me only to your master and to you, to speak these words, and not to the men who sit on the wall, who will eat their own dung and drink their own urine with you?”
13 Halafu kamanda mkuu akasimama na kupiga kelele kwa sauti kubwa kwa lugha ya kiyahudi, na akisema,
Then Rabshakeh stood, and called out with a loud voice in the Jews’ language, and said, “Sh'ma ·Hear obey· the words of the great king, the king of Assyria [Level plain]!
14 ''Mfalme asema, ' Msimruhusu Hezekia awadanganye ninyi, maana hataweza kuwaokoa ninyi.
Thus says the king, ‘Don’t let Hezekiah deceive you; for he will not be able to deliver you.
15 Msimruhusu Hezekia awafanye muumuamini Yahwe, Nawambieni Hakika Yahwe atatukomboa sisi; mjii huu hautachukuliwa na mfalme wa Asiria.''
Don’t let Hezekiah make you trust in Adonai, saying, “Adonai will surely deliver us. This city won’t be given into the hand of the king of Assyria [Level plain].”’
16 Msimsikilize Hezekia, maana hivi ndivyo mfalme wa Asiria anavyosema: 'Fanyeni amani na mimi na mje kwangu. Halafu kila mmoja wenu atakula kwenye mzabibu wake mwenyewe na tunda la mti wake mwenyewe, na kunjwa maji ya kisima chake mwenyewe.
Don’t sh'ma ·hear obey· Hezekiah, for thus says the king of Assyria [Level plain], ‘Make your peace with me, and come out to me; and each of you eat from his vine, and each one from his fig tree, and each one of you drink the waters of his own cistern;
17 Mtafanya hivi mpaka nije kuwachukua na kuwapeleka kwenye nchi kama ya kwenu. nchi ya mavuno na mvinyo mpya, nchi ya mkate na shamba.
until I come and take you away to a land like your own land, a land of grain and new wine, a land of bread and vineyards.
18 Msimruhusu Hezekia awapotoshe nyie, akisema, Yahwe atatuokoa nyie; Je kuna miungu ya aina yeyote ya watu iliyowakomboa kutoka mikononi mwa mfalme wa Asiria?
Beware lest Hezekiah persuade you, saying, “Adonai will deliver us.” Have any of the deities of the nations delivered their lands from the hand of the king of Assyria [Level plain]?
19 Wako wapi miungu wa Hamathi na Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je wameikomboa Samaria kutoka kwenye nguvu zangu?
Where are the deities of Hamath and Arpad? Where are the deities of Sepharvaim? Have they delivered Samaria from my hand?
20 Miongoni mwa miungu yote ya nchi hii, Je kuna miungu ya aina yeyote iliyoikomboa nchi yao kutoka kwenye nguvu yangu, ni kama Yahwe anaweza kuawokoa Yerusalemu kutoka kwenye nguvu yangu?''
Who are they among all the deities of these countries that have delivered their country out of my hand, that Adonai should deliver Jerusalem [City of peace] out of my hand?’”
21 Lakini watu wanabaki kimya na hawataki kujibu, maana amri ya mfalme ilikuwa, ''Msimjibu''.
But they remained silent, and said nothing in reply, for the king’s order was, “Don’t answer him.”
22 Halafu Eliakimu mtoto wa Hilkia, yeye aliye juu ya kaya, Shebna mwandishi, na Joa mtoto wa Asafu, na mtunza kumbukumbu, walikuja kwa Hezekia na nguo zilizotoboka na wakapeleka maneno ya kamanda mkuu.
Then Eliakim the son of Hilkiah, who was over the household, and Shebna the scribe, and Joah, the son of Asaph, the recorder, came to Hezekiah with their clothes torn, and told him the words of Rabshakeh.

< Isaya 36 >