< Isaya 32 >
1 Tazama, mfalme atatawala kwa haki, wakuu wataongoza kwa haki.
Look, a king will reign in righteousness, and princes will rule in justice.
2 Kila mmoja atakuwa kama makazi kutoka kwenye upepo na kimbilio kutoka kwenye dhoruba, kama mifereji kwenye sehemu kavu, kama kivuli kwenye mwamba mkubwa katika nchi iliyochoka.
Each one will be like a shelter from the wind and a refuge from the storm, like streams of water in a dry place, like the shade of a great rock in a land of weariness.
3 Halafu macho ya waie wanaoona hayataona giza, na masikio ya wale wanosikia yatasikia vizuri.
Then the eyes of those who see will not be dim, and the ears of those who hear will hear attentively.
4 Wenye upele watafikiria kwa makini kwa uelewa wao, na wenye kigugumizi watazungumza dhahiri na kwa urahisi.
The rash will think carefully with understanding, and the stutterer will speak distinctly and with ease.
5 Mjinga hataitwa tena muheshimiwa, wala muongo hataitwa mkuu.
The fool will no longer be called honorable, nor the deceiver called principled.
6 Maana mjinga anazungumza ujinga, na moyo wake unapanga maovu na matendo ya wasiomcha Mungu, na anaongea mambo mabaya kuhusu Yahwe. Na anawafanya wenye njaa kuwa tupu na wenye kiu kukosa maji
For the fool speaks folly, and his heart plans evil and godless actions, and he speaks wrongly against Yahweh. He makes the hungry empty, and the thirsty he causes to lack drink.
7 Njia ya muongo ni maovu. Anajua kubuni mipango mibaya ya kuwalagai masikini kwa uongo, na hata kama masikini atazungumza ukweli.
The deceiver's methods are evil. He devises wicked schemes to ruin the poor with lies, even when the poor say what is right.
8 Lakini watu wa heshima wanapanga mipango ya kuheshimika; na kwa sabaubau ya matendo ya wenye heshima tuatasimama.
But the honorable man makes honorable plans; and because of his honorable actions he will stand.
9 Nyanyukeni juu, enyi wanawake mlio wepesi, na sikilizeni sauti yangu; enyi mabinti msiowangalifu, nisikilizeni mimi.
Rise up, you women who are at ease, and listen to my voice; you carefree daughters, listen to me.
10 Maana kwa mda mfupi zaidi ya mwaka ujasiri wenu utavunjika, nyie wanawake msiojali, maana mavuno ya zabibu yatakwama, mavuno hayatakuwepo.
For in a little more than a year your confidence will be broken, you carefree women, for the grape harvest will fail, the ingathering will not come.
11 Tetemekeni, enyi wanawake, mliowadhaifu; taabikeni enyi msikuwa wangalifu; ondoeni nguo zenu nzuri mbaki wazi;
Tremble, you women who are at ease; be troubled, you confident ones; take off your fine clothes and make yourselves bare; put on sackcloth around your waists.
12 Vaeni nguo za magunia katika viuno vyenu. Ole watakaojichukulia mashamba mazuri, kwa mzabibu ulio zaa sana.
You will wail for the pleasant fields, for the fruitful vines.
13 Kwenye aridhi ya watu wangu kutamea miiba na mbigiri, hata juu ya nyumba za furaha na mji ulio na shangwe.
The land of my people will be overgrown with thorns and briers, even in all the once joyful houses in the city of revelry.
14 Maana jumba litaachwa, mji uliosongamana utakuwa faragha; kilima na mnara vitakuwa mapango daima, furaha ya punda, malisho ya mifugo;
For the palace will be forsaken, the crowded city will be deserted; the hill and the watchtower will become caves forever, a joy of wild donkeys, a pasture of flocks;
15 mpaka roho itushukie sisi kutoka juu, na jangwa litakuwa shamba linalozaa, na shamba linalozaa litachukuliwa kama msitu.
until the Spirit is poured on us from on high, and the wilderness becomes a fruitful field, and the fruitful field is considered as a forest.
16 Wenye haki wataishi jangwani; na wenye haki wataishi katika shamba linalozaa matunda.
Then justice will reside in the wilderness; and righteousness will live in the fruitful field.
17 Kazi ya mwenye haki itakuwa ni ya amani; na matokeo ya wenye haki, ni utulivu na kujiamini daima.
The work of righteousness will be peace; and the result of righteousness, quietness and confidence forever.
18 Watu wangu wataishi katika makao ya amani, na katika nyumba salama na mahali tulivu pa kupumzikia.
My people will live in a peaceful habitation, in secure homes, and in quiet resting places.
19 Lakini hata kama ni mvua ya mawe na msitu umeharibiwa, na mji umeteketezwa,
But even if it hails and the forest is destroyed, and the city is completely annihilated,
20 yule ambae anaye panda pembezoni mwa mifereji atabarikiwa, na yule atakaye wapeleka ng'ombe na punda kuchunga.
you who sow beside all the streams will be blessed, you who send out your ox and donkey to graze.