< Isaya 27 >

1 Katika siku hiyo Yahwe kwa upanga wake ulio mgumu, mkubwa na mkali, atamadhibu Leviathani na nyoka yule anayetambaa kwa kupenya, na atamuua mnyama anayeishi baharini.
In the day that he will visit [judgment] Yahweh with sword his fierce and great and mighty on Leviathan a snake fleeing and on Leviathan a snake twisting and he will slay the sea monster which [is] in the sea.
2 Siku hiyo: Shamba la zabibu, litawaimbia.
In the day that a vineyard of (delight *LB(AH)*) sing of it.
3 ''Mimi Yahwe ni mlinzi wake; Ninalimwagia maji kila wakati; hivyo hakuna anayelimiza, Ninalilinda usiku na mchana.
I Yahweh [am] keeper its to moments I water it lest someone should injure it night and day I guard it.
4 Sina hasira, Oh, kama mbigiri na miiba! Katika vita nitatembea dhidi yao; Nitawachoma wote kwa pamoja;
Rage not [belongs] to me who? will he give me thorn[s] bush[es] in battle I will march against it I will burn it altogether.
5 labda wafahamu ulinzi wangu na wafanye amani na mimi, waache wafanye amani na mimi.
Or let anyone take hold on protection my let anyone make peace to me peace let anyone make to me.
6 Kwa siku inayokuja, Yakobo atachukua mzizi; Israeli itatoa maua na kuchipua; na itaijaza aridhi yote kwa matunda.''
The coming [times] it will take root Jacob it will blossom and it will bud Israel and they will fill [the] surface of [the] world fruit.
7 Je Yahwe alimshambulia Yakobo na Israeli na hayo mataifa yaliyomshambulia? Je Yakobo na Israeli waliuliwa na wao kama mliowachinja katika mataifa mliowauwa wao?
¿ Like [the] striking? of [the] [one who] struck it has he struck it or? like [the] slaughter of slain [ones] its has it been slain.
8 Kitika kipimo halisi cha kuridhisha, watume Yakobo na Israeli mbali; aliwaondosha mbali kwa upepo mkali, katika siku ya upepo wa mashariki.
(By startling *L(abh)*) by sending away it you will conduct a case with it he drove out by wind his fierce in [the] day of [the] east wind.
9 Hivyo kwa njia hii, maovu ya Yakobo yatalipiwa, maana hii itakuwa matunda yote yakuomdolewa dhambi zake: pale atakapofanya mathebau ya mawe kama chokaa na kuviangamiza katika vipande vipande, na hakuna nguzo za Ashera au madhebau itakayoachwa imesimama.
Therefore by this it will be atoned for [the] iniquity of Jacob and this [is] all [the] fruit of [the] removing of sin its when makes he - all [the] stones of [the] altar like stones of chalk pulverized not they will stand Asherah poles and incense altars.
10 Maana mji imara umeharibiwa, makao yake na faragha yake yameachwa kama jangwa. Kuna ndama wanachungwa, na huko ndiko atakapo lala na kuyala matawi yake.
For a city fortified [is] alone a habitation [is] deserted and forsaken like the wilderness there it will graze a calf and there it will lie down and it will bring to an end branches its.
11 Matawi yake yatakaponyauka yatanguka. Wanawake watakuja na kuyatumia kutengeneza moto, maana hawa sio watu waelewa. Hivyo basi Muumba wao hatakuwa na huruma juu yao, na yeye aliyewaumba atakuwa na huruma juu yao.
When dry up branch[es] its they are broken off women [are] coming [are] setting light to it for not [is] a people of understanding it there-fore not he will have compassion on it [the] [one who] made it and [the] [one who] formed it not he will show favor to it.
12 Na siku hiyo itakuwa kwamba Yahwe atapururua kutoka mto Efrate mpaka Wadi ya Misri na njie, watu wa Israeli, tutakusanyika mahali pamoja mmoja mmoja.
And it will be in the day that he will beat out Yahweh from [the] flowing stream of the River to [the] wadi of Egypt and you you will be gathered to one one O people of Israel.
13 Siku hiyo tarumbeta kubwa litapulizwa; na watu waliopotea katika nchi ya Asiria watakuja, na waliotupwa katika nchi ya Misri, watamuabudu Yahwe katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.
And it will be - in the day that it will be blown on a trumpet great and they will come those [who] were lost in [the] land of Assyria and the outcasts in [the] land of Egypt and they will bow down to Yahweh on [the] mountain of holiness in Jerusalem.

< Isaya 27 >