< Isaya 26 >

1 Siku hiyo wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda: Tuna mji imara; Mungu amefanya wokovu katika kuta na ngome zake.
In that day shall this song be sung in the land of Iudah, We haue a strong citie: saluation shall God set for walles and bulwarkes.
2 Fungua lango, ili mataifa yenye haki yaweze na yenye kutunza imani yaweze kuingia ndani.
Open ye the gates that the righteous nation, which keepeth the trueth, may enter in.
3 Akili mlionayo, mtamuhifadhi yeye katika amani kamili, maana anawamini ninyi.
By an assured purpose wilt thou preserue perfite peace, because they trusted in thee.
4 Mwamini Yahwe daima; maana Yaha, Yahwe, ni mwamba wa milele.
Trust in the Lord for euer: for in the Lord God is strength for euermore.
5 Maana atawashusha wale wote wenye kiburi; mji ulio juu atushusha chini, ataushusha chini kwenye aridhi; na ataulinganisha na mavumbi.
For hee will bring downe them that dwell on hie: the hie citie he will abase: euen vnto the ground wil he cast it downe, and bring it vnto dust.
6 Utakanyagwakanyagwa chini na miguu ya walio masikini na wahitaji.
The foote shall treade it downe, euen the feete of the poore, and the steppes of the needie.
7 Mapito ya mwenye haki yamenyooka, Wenye haki; mapito ya wenye haki umeyanyoosha.
The way of the iust is righteousnesse: thou wilt make equall the righteous path of the iust.
8 Ndio, kaika mapito ya hukumu yako, Yahwe, tunakusubiri wewe; jina lako na sifa zako ni matamanio yetu.
Also we, O Lord, haue waited for thee in the way of thy iudgemets: the desire of our soule is to thy Name, and to the remembrance of thee.
9 Nimekutamani wewe wakati wa usiku; ndio, roho iliyo ndani yangu ina kutafuta kwa bidii. Pindi hukumu yako itakapokuja duniani, wenyeji wa duniani watajua kuhusu haki.
With my soule haue I desired thee in the night, and with my spirit within mee will I seeke thee in the morning: for seeing thy iudgements are in the earth, the inhabitants of the world shall learne righteousnesse.
10 Na tuonyeshe upendeleo kwa waovu, lakini hawatajifunza haki. katika nchi ya wanyofu anatenda maovu na haoni ukuu wa Yahwe.
Let mercie bee shewed to the wicked, yet hee will not learne righteousnesse: in the land of vprightnesse will he do wickedly, and will not beholde the maiestie of the Lord.
11 Yahwe, mkono wako umenyanyuliwa juu, lakini hawapati hizo taarifa. Lakini wataona bidii kwa watu na wataona aibu, kwa sababu idadi ya maadui watawatafuna.
O Lord, they will not beholde thine hie hande: but they shall see it, and bee confounded with the zeale of the people, and the fire of thine enemies shall deuoure them.
12 Yahwe, utaleta amani kwetu, maana kweli, umekamilisha kazi zetu zote.
Lord, vnto vs thou wilt ordeine peace: for thou also hast wrought all our workes for vs.
13 Yahwe Mungu wetu, viongozi wengine badala yako wametutawala sisi; Lakini tunalitukuza jina lako.
O Lord our God, other lords beside thee, haue ruled vs, but we will remember thee onely, and thy Name.
14 Wamekufa, hawataishi tena; ni maremu hao, hawatafufuka tena. Kweli, umekuja kuwahukumu na kuwaharibu wao, na umefanya kila kumbukumbu kutoweka.
The dead shall not liue, neither shall the dead arise, because thou hast visited and scattered them, and destroyed all their memorie.
15 Umeliongeza taifa, Yahwe, umeliongeza taifa; umeheshimiwa; umeinuliwa katika mipaka yote ya nchi.
Thou hast increased the nation, O Lord: thou hast increased the nation: thou art made glorious: thou hast enlarged all the coastes of the earth.
16 Yahwe, katika mateso yao walikuangalia wewe; walipatwa na wasiwasi katika maombi yao maana adhabu yako ilikuwa juu yao.
Lord, in trouble haue they visited thee: they powred out a prayer when thy chastening was vpon them.
17 Kama mwanamke mjamzito anayekaribia kujifungua, hupatwa na uchungu na hulia kwa uchungu, hivyo ndivyo tulivyokuwa kabla, Bwana.
Like as a woman with childe, that draweth neere to the trauaile, is in sorow, and cryeth in her paines, so haue we bene in thy sight, O Lord.
18 Tulikuwa wajawazito, tumekuwa katika mateso, lakini ni kama tumeshajifungua katika akili zetu. Hatujauleta wokovu duniani, na wakazi wa duniani hawakuanguka.
We haue coceiued, we haue borne in paine, as though we should haue brought forth winde: there was no helpe in the earth, neither did the inhabitants of the world fall.
19 Wafu wenu wataishi; watu wenu walio kufa watafufuka. Amka na uimbe kwa furaha, njie muishio mavumbini; maana umande wenu ni umande wa mwanga, na dunia itawaleta mbele wafu wake.
Thy dead men shall liue: euen with my body shall they rise. Awake, and sing, ye that dwel in dust: for thy dewe is as the dew of herbes, and the earth shall cast out the dead.
20 Enendeni, watu wangu, ingieni katika vyumba vyenu na mfunge mlango nyuma yenu; jificheni kwa mda mfupi, mpaka hasira itakapopita.
Come, my people: enter thou into thy chambers, and shut thy doores after thee: hide thy selfe for a very litle while, vntill the indignation passe ouer.
21 Maana, angalia, Yahwe anakaribia kutoka katika eneo lake kuwahadhibu watu waishio duniani kwa ajili ya makosa yao; dunia itaachia umwagaji wa damu, na hawatawaficha tena waliokufa.
For lo, the Lord commeth out of his place, to visite the iniquitie of the inhabitants of the earth vpon them: and the earth shall disclose her blood, and shall no more hide her slaine.

< Isaya 26 >